Sunday, 9 September 2018

Je, Twahitaji Ufufuo au Mageuzi?

Kila mmoja anafikiria juu ya kuubadili ulimwengu, lakini hakuna anayefikiria kujibadili yeye mwenyewe. Jimmy J

Wakati kitu fulani kinapofufuliwa, mambo  ya  zamani  yanaletwa tena kuwa hai, mawazo  mapya yanaletwa  yanaletwa kuwa kitu. Wakati jamii inaposhuhudia  maslahi  mapya  ya  kidini,  huo  huitwa ufufuo. Kamusi ya  MerrianWebster Collegiate inaelezea  ufufuo kama “mkutano wa hisia za juu  sana wa kiinjilisti  au msururu wa  mikutano.”  Katika  maisha  yangu  ya utu uzima kama  Mkristo, nimewasikia  watu wakiongea  kuuhusu  na kuombea ufufuo. Lakini sina  hakika  kwamba  ufufuo  ndio tunaohitaji.  


Nafikiri twahitaji  kitu kikubwa  zaidi. Nafikiri  twahitaji  Mageuzi. Kamusi  ya Webster inaelezea neno hili  mageuzi kuwa “mabadiliko ya ghafla, makubwa, au makamilifu.” Kwa  kawaida  hatuna  shida kushughulikia mambo  ya  zamani kuliko   mabadiliko  makubwa.  Lakini  je, ufufuo  uliopita  umelibadili kanisa  na ulimwengu? Umekuwa na manufaa  wakati huo;  lakini ni nini  tunachohitaji  sasa  katika kanisa ili  tuweze kuwa na utendaji ufaao  katika  ulimwengu? Itatuchukua  nini  ili tuwe nuru ambayo Kristo alitaka tuwe? Katika  kitabu chake  The  Barbarian Way,  Erwin McManus anaandika,  “Wacha  Ukristo wa  usafi utuondokee  na turejelee  imani ya  kale yenye nguvu inayochagua  mageuzi badala  ya  kushawishika, hatari  badala  ya  usalama,  na huruma badala  ya  kuwa  vuguvugu na dini  zilizo majimaji.”  

Huruma ya  Kristo ilimfanya   asulubishwe msalabani.  Je,  yetu itatufanya  tujitolee baadhi  ya  njia zetu za  zamani ili kizazi  kijacho  kishuhudie nguvu ya  mabadiliko  ya  Mageuzi ya Upendo? Yesu alikuwa  mpenda  mageuzi,  na  alikuwa  hatetei utamaduni. Alikuja ili  kuleta mabadiliko, na yakawakasirisha  watu wa  kidini wa  siku  hiyo. Mungu  habadiliki,  lakini  Huwabadilisha wengine. Nimepata  kwamba  Anapenda ubunifu  na  mambo  mapya  na  huweka mambo kuwa mapya na yakiwaka moto. 

Baadhi  ya makanisa  hayatafikiria kubadilisha kitu kama  vile mtindo wa  muziki  wao. Wataimba  nyimbo za  kitabu cha  nyimbo na  kucheza  kinanda pekee ikiwa  wataendelea kuwepo.  Wanapuuza ukweli  kwamba  waumini wao  huendelea  kupungua kiwango chao na hawawaathiri jamii yao  hata  kidogo. Wanahitaji kuchunguza Jumapili asubuhi na  wajiulize ni kwanini kila mtu katika  jengo  hilo ni wa  makamu  au  mtu mzima.  Vijana  wako  wapi?  Iwapi  furaha? Uwapi uhai? Miaka  kadhaa  iliyopita,  Nilianza   kushuhudia  kupungua kwa mikutano katika kanisa letu  na nikagundua kwamba wengi wa  waliokuwa  wakihudhuria  walikuwa  watu wa  makamu, ndugu wakaribu(wafanyakazi)wa washirika/au  watu  wazima.

Niliongea na rafiki yangu wa  kiume,  aliyekuwa  na  umri wa miaka ishirini  na minne   wakati huo alianza  kunihimiza tufanye mabadiliko makubwa  katika mtindo  wa  muziki,  taa,  mapambo  na aina ya nguo wanazovaa wahubiri. Alisema kwamba  kizazi  chake kinahitaji kufikiwa na  injili  ya  Yesu Kristo,  lakini kinasinywa  na  mtindo wa zamani  wa  dini wenye sifa  ya  kuzingatia  sheria na  unaochosha.  Kwa karibu mwaka  mzima, mimi  na mchungaji mmoja tulipinga  sana  jambo  hilo. 

Ulisema kile  ambacho  watu wengi husema wanapokuwa  hawataki mabadiliko:  “Mungu habadiliki.”  "Sisi pia tulionelea  kile  tulichofanya kufikia  hapo  kimeendelea  vyema. Kwanini ukibadilishe?  Majivuno mengi yalihusika,  na  ilikuwa  vigumu kumfanya  kijana  Jimmy J mwenye umri wa miaka ishirini  ambaye  alikuwa ameanza  tu kufanya kazi  nasi kutuambia kile  tunachopaswa  kufanya.... Lakini mwaka ulipoendelea  tulianza kuwasikiliza vijana wengine, na tukatambua kwamba hatukuhitaji mbinu za kuabudu. Ujumbe  wetu haungebadilika,  lakini njia unayotokea  ujumbe huo ilihitaji kubadilika" -Kasisi Barnet

Ulimwengu unabadilika, watu wanabadilika,  kizazi  kipya kinafikiria tofauti kuliko wale wa  zamani,  na twahitaji  kufikiria jinsi  ya kuwafikia. Tunataka kuona vijana kwenye mikutano, lakini hatuwi  tayari  kuwapa  chochote  kinachowafurahisha.  Hatuwi tayari kukutana nao mahali waliko. Lakini kidogo kidogo mioyo yetu  ikifunguka  ili  kujaribu mambo mapya, na tunaweza kuona  matokeo makuu. Hatutawaapoteza  tena  watu na  badala  yake watu wapya watakuja,  na  wengi wao  watakuwa  vijana  wenye furaha.  Ikiwa  tuna hekima ya  kizazi cha  watu wazima  na furaha  ya  ubunifu  ya vijana, basi tuko na wote walio bora ulimwenguni.

Kasisi Barnet alinisimulia kisa hiki"siku moja Dan alitaka  kutumia rangi  fulani  katika jarida  letu la  kila mwezi ambazo  tulikuwa hatujawahi  kuzitumia. Mimi sikuzipenda kwa  hiyo nikasema hapana.  Alikuwa  mkakamavu kuhusu  kutumia  rangi mpya, na nikasisitiza nikasema, “Mimi sizipendi,  na hatutazitumia!”  akasema,  “Sikutambua  kwamba uliitwa  ili  kujihubiria.  Je,  ikiwa  watu  wengine  wanazipenda  rangi hizo?”  Kufikia  hapo  nilipata  funzo la  kunifungua macho.  Nilitambua kwamba  nina sheria za  mavazi za  ofisi  ambazo  nilipenda  na tulitumia  rangi  katika jarida,  kwa  matangazo, na katika jengo ambazo  nilizipenda. Tulikuwa na muziki  ambao  niliupenda. Niliaibika wakati nilipotambua jinsi  mawazo  yangu mengi ni kuhusu  yote ninayoyapenda na ilikuwa ni  faraja  kwangu,  sio watu wengine wanavyohitaji. Mimi  na viongozi tulianza  kutambua tunaabudu  mbinu  na kwamba  mbinu  hizo hazikumaanisha  chochote  kwa  Mungu. 

Ulikuwa na ujumbe  Wake aliotaka  kuutoa,  na njia uliotokea  ingebadilishwa. Kwa  hiyo tulianza  kubadilika na tumeendelea  kuwa wazi   kubadilika tangu  wakati huo. Tumebadilisha  mitindo  yetu ya mavazi kwa kuzingatia mitindo  ya kisasa zaidi. Tulibadilisha bendi  zetu za  kuabudu  na zile ambazo  zitawavutia  vijana  wengi zaidi. Niliamua  kukipenda kizazi  cha  sasa  ili  waimbe nyimbo wanazofurahia.  Tulipunguza  muda  wa ibada zetu kwa sababu  jamii yetu yote leo inataka  mambo yafanywe haraka.  Nilikuwa nimezoea ibada za kanisa za muda  wa saa  tatu, lakini  sio kila mmoja alipenda hivyo, kwa  hiyo tukaamua  kukutana  na watu  kati kati. Tulibadili taa  zetu kuwa  za  kuvutia zaidi.  Hata  tulipata  mashine ya  kutoa moshi wa  ukungu wanayoniambia inavutia sana watu. Mimi bado nafikiria inawazuia  watu kuona vizuri, lakini naweza  kupata ukungu ikiwa  unawafanya  watu kuwa  na uhusiano wa  kutisha na mimi  na kusikiliza ujumbe  wa  injili.  Kumbuka  Paulo alisema alikuwa hali zote kwa  watu wote;  ili  kwa  njia zote  apate kuwaokoa watu kwa kuwahubiria injili  ya Yesu  Kristo (angalia 1 KOR 9:2022). Hakuabudu mbinu na hata sisi pia."-Kasisi Barnet 

Biblia inasema  kwamba katika siku za  mwisho tutashuhudia kanisa  lenye uchoyo na ubinafsi. Watu watapoteza  maadili na watashikilia aina ya dini  lakini  watanyimwa nguvu ya injili  (angalia 2 TIM 3:1-5). Twahitaji  kuona nguvu  ya Mungu katika makanisa yetu. Twahitaji  kuona  mabadiliko  ya  maisha,  uponyaji,  kudumishwa na kukombolewa.  

Twahitaji  kuona upendo  wa  Mungu ukitiririka kwa  njia huru. Twahitaji kuona  Mageuzi,  na  nimejitolea kuwa sehemu yake! Ninaweza  kusema kuwa  mabadiliko  mengi tunayoweza kufanya  kwenye mikutano yetu si  yale ambayo tunayaweza kuyapenda. Lakini ninajifunza  zaidi kila siku  kwamba upendo unahitaji tuwache njia zetu na tutafute njia za  Mungu  kwa  msimu  wa  sasa.  

Mabadiliko yetu mengi   yamekuwa kujitolea kwangu  mimi  binafsi, lakini najua  katika moyo wangu kwamba  yamekuwa jambo la sawa  kufanya.  Kulikuwa na wakati ambapo  nilifikiri  kwamba  Mungu hangeweza  kumbariki mtu ikiwa yuko  jukwaani  akijaribu kuwaongoza  watu ilhali amevalia  nguo aina  ya  jeans. Kisha nikafikiria kuhusu  kile  ambacho Musa pengine alikuwa  amevalia  wakati alipokwenda juu mlimani  kupokea Amri Kumi  na hatimaye  nikatambua jinsi  nilivyokuwa  mjinga. 

Yohana Mbatizaji  alikuwa  akivalia mavazi  ya  aina  ya  kipekee,  alikuwa tabia  za  kipekee za  ulaji, na  makazi  yake yalikuwa  jangwani,  lakini aliongoza mageuzi. Alitayarisha njia ya Masihi. Hakuwa shabiki wa  dini yenye mpangilio na aliwaita  viongozi wakuu wa  kidini  wa nyakati zake kuwa  kundi  la nyoka  wenye sumu  kali. Alichukizwa mno na  watu  wa  kidini  waliojichukulia  kuwa  wenye haki  wa  siku hizo ambao  walikwenda hekaluni  kuomba lakini hawangeweza kuinua kidole kumsaidia mtu yeyote anayehitaji msaada. Mungu anaangalia  moyo,  na  twahitaji  kujifunza kufanya  hivyo pia.  Hakujali jinsi Musa au  Yohana  waliovyoonekana.  Alifurahi kupata  mtu asiyeogopa  kuongoza  maasi  dhidi  ya  dini  iliyokufa  na kuwaongoza watu kuwa na uhusiano na Mungu.

Imeandikwa na Jimmy J.
Mwana Mageuzi ya Upendo.
Email: mawaidhapopote@gmail.com

No comments:

Post a Comment