Wednesday, 20 March 2019

SAFARI YA MOYO

“Ni nani atakayenitunzia watoto wangu?” analia mama anayekufa, akijua kwamba watoto wake  hivi karibuni watajiunga  na mamilioni ya wengine    kote  duniani  kumtafuta  mama  mpya.  Nimewaona  marafiki wanaougua  saratani  wakilia  maombi  hayo  hayo.  Siwezi  kufikiria  juu  ya afueni kuu ya moyo, au mauguzi makuu yanayosikika nyakati za giza kuu

Nataka  kumpigia  yowe  nimwambie.  “TUTAKUTUNZIA”  Hii  kwa  kweli  ni sehemu  ambayo  twahitaji  kujikakamua,  kuvumilia,  kuomba  na  KUAMINI, na kutoka kwa imani.