Wednesday, 20 March 2019

SAFARI YA MOYO

“Ni nani atakayenitunzia watoto wangu?” analia mama anayekufa, akijua kwamba watoto wake  hivi karibuni watajiunga  na mamilioni ya wengine    kote  duniani  kumtafuta  mama  mpya.  Nimewaona  marafiki wanaougua  saratani  wakilia  maombi  hayo  hayo.  Siwezi  kufikiria  juu  ya afueni kuu ya moyo, au mauguzi makuu yanayosikika nyakati za giza kuu

Nataka  kumpigia  yowe  nimwambie.  “TUTAKUTUNZIA”  Hii  kwa  kweli  ni sehemu  ambayo  twahitaji  kujikakamua,  kuvumilia,  kuomba  na  KUAMINI, na kutoka kwa imani.

Si lazima uishi katika nchi zinazostawi  ili kuwapata mayatima wanaohitaji  familia, au watu wenye upweke wanaotafuta urafiki,  kila  mmoja  wetu  anaishi  kwenye  miji  ambako  watoto  wanateseka  kwenye mifumo ya serikali inayojaribu  iwezavyo kutimiza mahitaji ambayo sisi kama kanisa twaweza kusaidia kuyatimiza.

Ninalipenda kanisa …yeye ni mjuzi wa mambo mengi na kweli ameinuka kupitia kote duniani  akiwa na mawazo mapya ya imani na furaha. Lakini  kanisa katika mahali  pake  bora ni wakati anapompenda  Mungu  akiwa  kama alivyo… na  kisha  Kanisa  linasimama na  mikono  imenyooshwa kuhudumia  jamii inayoteseka  na ulimwengu  uliovunjika,  kuwaunganisha  watu kwa  Yesu na yote yanayomaanisha  haya. Sio kuhukumu au kulaumu maskini, bali KUWAPENDA…na  kuwapenda  kuna  gharama,  na  ni  kitendo…sio  jina.

Pamoja,  twaweza  kusimama  mahali  penye  pengo  kwa  wale  wasiokuwa na sauti…kumpenda  Bwana  Mungu  wetu kwa moyo wetu wote, roho, akili  na  nguvu…NA  kuwapenda  jirani  zetu  kama  tujipendavyo  sisi wenyewe. Kwa kweli inashangaza!

Kwahiyo  twaweza  kuishughulikia  kivipi  hali  hii  kubwa  ya kukosa matumaini?  Twawezaje  kuwafungulia  mlango  wale  waliokwama  katika gereza  hili  hatari?  HAKUNA  hata  mmoja  anayeweza  kushughulikia jambo  hili  kibinafsi. Hata watu werevu  zaidi  duniani  wanaopenda  kutoa misaada  WANAWAHITAJI    wengine  na  ujuzi  wa  makundi  mbali  mbali  ya wataalam  wanaofanyakazi  pamoja  kwa manufaa  bora kwa  watu. Lakini twahitaji  kuanza mwanzo, twaweza kumdhamini  mtoto mmoja, kuwa sauti kwa wale  waliovunjika  katika jamii  zetu, saidia  kwa njia  moja  ikiwa una uwezo  katika mfumo wa malezi  wa kupanga  (mfano, Matunzo ya dharura, matunzo ya muda mfupi au muda mrefu, mifumo ya kuwa na malezi ya mwisho wa wiki) changa pesa za msaada au mahitaji yaliyo kwenye  moyo wako, ianzishe  miradi  hii katika kanisa  lako na ufanye huduma hii ianze kuendelea, ishi maisha ya kawaida ya kujali kutoa kwa watu wengine  na wala sio kutumia…orodha  ni ndefu mno. Lakini la muhimu, tuhakikishe kwamba mioyo yetu  na   maisha yetu  yanatiwa mafuta na kuwa imara kwa fursa yoyote iliyoko kila siku, ama iwe ni ya kimataifa au ya nchi yako… ni kama vile hadithi ya Msamaria mwema, aliyetumia siku yake nzima kwenda kuleta msaada  na majibu mahali ambapo  wengine  walishuhudia  na  kupita.  Msamaria  ALIGUSWA  na upendo wa huruma…na hakuguswa tu  hisia za  moyo, bali alijibu  kwa vitendo.  Na ningependa  kusema kwamba ikiwa unapitia  msimu ambao unadhani unahitaji kuhudumiwa, kuliko wewe kwenda  kutoa huduma, basi  jipe  moyo.

Jiweke  kwenye  mazingira  ya kuabudu  na kutukuza, ijaze  nyumba  yako  na muziki  unaosisimua  moyo  wako,  jaza  gari  lako na  kanda  na  CD  za  neno  la  Mungu,  ungana  na  familia,  kanisa  na  jamii unayojua  kwamba  utaburudishwa  na kutiwa  moyo…na mruhusu  Roho wa Bwana aendelee  kukujaza  kutoka ndani hadi nje. Iwapo unahitaji uponyaji, au ushindi wa kifedha, au miujiza ya uhusiano…Mungu  wetu anaweza.  Jiruhusu  uangukie  kwenye  mikono  salama  ya Mungu  wetu  na nguvu yetu,  kwani hatakuacha wala kukukana, kumuamini Yeye ni furaha kuu na matumaini yako. Lakini ninakuachia  jambo  hili ukumbuke…

KUMPENDA  Bwana  Mungu  wako  kwa  moyo  wako  wote,  akili  yako yote,  roho  yako  yote  na  nguvu  zako  zote  NA  umpende  jirani  yako  kama ujipendavyo  wewe mwenyewe.  Umejazwa hazina na thamani kikamilifu. Usisahau!

#JitoeMwangaKwaMaishaYaWengine.
Jimmy J.

No comments:

Post a Comment