Monday, 22 October 2018

Barua

Wapendwa wangu Mama na Baba.
    Tangu Niende Chuo kikuu Najua sijachukua Muda wa kuwaandikia na Naomba msamaha kukosa kufikiria kuwaandikia paka sasa.Nitawaeleza Mambo yote katika Barua hii lakini kabla hamjasoma Tafadhali ketini chini,Tafadhali msisome paka Mketi chini.
   Naendelea Vizuri sasa,Jeraha la fuvu la kichwa baada ya kuruka kwa dirisha la Bweni langu Sasa limepona,Niliruka baada ya bweni langu kushika moto muda mfupi.baada ya kuwasili hapa sasa huwa napata maumivu ya kichwa mara moja kwa siku.