Thursday, 24 May 2018

Ni tofauti gani kati ya nafsi na roho?


Nafsi na roho ni sehemu mbili muhimu za mwili wa ndani ambazo Bibilia yaamini ni tabia kamili za mwanadamu. Inaweza kutatanisha kujaribu kutambua kabisa tofauti iliyoko kati ya hayo mambo mawili. 


Neno “roho” linaashiria mwili wa ndani pekee wa mwanadamu. Wanadamu wana roho, lakini sisi si roho. Ingawa katika maandiko ni waumini wanatambulika kuwa hai kiroho ( 1 Wakorintho 2:11; Waebrania 4:12; Yakobo 2:26), bali wasioamini wamekufa kiroho ( Waefeso 2:1-5; Wakolosai 2:13). 

Paulo katika uandishi wake, anasema kuwa roho ni kitu cha maana katika maisha ya Mkristo (1 Wakorintho 2:14; 3:1; Waefeso 1:3; 5:19; Wakolosai 1:9; 3:16). Roho ni kitu katika maisha ya mwanadamu ambacho kinampa uwezo wa kuwa na uhusiano wa karibu na Mungu. Popote neno “roho” lilikotumika, linaashiria sehemu ya ndani ya mwanadamu ambayo “inakutanika” na Mungu, ambaye Yeye mwenyewe ni Roho (Yohana 4:24).

Neno “nafsi” laweza maanisha mwili wa nje na mwili wa ndani wa mwanadamu. Mbali na mwanadamu kuwa na roho, pia mwanadamu ni nafsi. Katika maana yake ya kawaida, neno “nafsi” linamaanisha “uhai.” Ingawa zaidi ya hii maana kuu, Bibilia inazungumzia nafsi katika miktadha mbalimbali. Mojawapo ya hizi ni nia ya mwanadamu kutenda dhambi (Luka 12:26). Mwanadamu kwa maumbilie yake ni mwenye dhambi, na nafsi zetu zimeharibika kwa ajili hiyo. Nguzo kuu ya uhai imeondolewa wakati wa kifo (Mwanzo 35:18; Yeremia 15:2). Nafsi, pamoja na roho ndizo nguzo katika uzoefu wa kiroho na kihisia (Ayubu 30:25; Zaburi 43:5; Yeremia 13:17). Popote neno “nafsi” lilikotumika, linaweza kumaanisha mwili wote - uwe hai au uwe umekufa.

Nafsi na roho zimeunganika, lakina zinaweza kutenganishwa (Waebrania 4:12). Nafsi ni sehemu ya uhai wa mwanadamu; ni vile tulivyo. Roho ni sehemu ya mwanadamu ambayo inakutanika na Mungu.

No comments:

Post a Comment