Wednesday, 17 April 2019

Kuwa na Ndoto juu ya Maisha yako

Muhubiri 5:3 kwa maana ndoto huja kwasababu ya shughuli nyingi....kwasababu baadhi yetu  tunandoto na hatutaki kufanya kazi na wakati mwingine hatuna budi kupitia hali ngumu.

Naamini unapokuwa na ndoto ni kama unapokuwa na ujauzito,kuna wanawake wachache ambao huweza kujifungua bila uchungu lakini si wengi sana.Nafikiri kwamba ukitaka kuzalisha kitu lazima ufahamu kwamba ni zaidi ya kuwa na wazo nzuri,Unakuwa na ndoto,unakuwa na matumaini,unakuwa na mpango lakini lazima uwe tayari kufanya kazi na kupitia yale ambayo unapaswa kupitia ili ndoto yako iweze timia.

Wednesday, 20 March 2019

SAFARI YA MOYO

“Ni nani atakayenitunzia watoto wangu?” analia mama anayekufa, akijua kwamba watoto wake  hivi karibuni watajiunga  na mamilioni ya wengine    kote  duniani  kumtafuta  mama  mpya.  Nimewaona  marafiki wanaougua  saratani  wakilia  maombi  hayo  hayo.  Siwezi  kufikiria  juu  ya afueni kuu ya moyo, au mauguzi makuu yanayosikika nyakati za giza kuu

Nataka  kumpigia  yowe  nimwambie.  “TUTAKUTUNZIA”  Hii  kwa  kweli  ni sehemu  ambayo  twahitaji  kujikakamua,  kuvumilia,  kuomba  na  KUAMINI, na kutoka kwa imani.