Muhubiri 5:3 kwa maana ndoto huja kwasababu ya shughuli nyingi....kwasababu baadhi yetu tunandoto na hatutaki kufanya kazi na wakati mwingine hatuna budi kupitia hali ngumu.
Naamini unapokuwa na ndoto ni kama unapokuwa na ujauzito,kuna wanawake wachache ambao huweza kujifungua bila uchungu lakini si wengi sana.Nafikiri kwamba ukitaka kuzalisha kitu lazima ufahamu kwamba ni zaidi ya kuwa na wazo nzuri,Unakuwa na ndoto,unakuwa na matumaini,unakuwa na mpango lakini lazima uwe tayari kufanya kazi na kupitia yale ambayo unapaswa kupitia ili ndoto yako iweze timia.