Thursday, 9 August 2018

Je, Yesu Alikuja kwa ajiri ya Wayahudi Pekee ??

Ndugu   zetu   Waislamu   wanapenda  sana  kudai   kuwa   Yesu   alikuja kwa   ajili   ya  Wayahudi   peke   yao   na   sio   kwa   ajili   ya   ulimwengu  wote.   Na   andiko   wanalolitumia   tena  na  tena  ni   la  Mathayo   15:24  pale  Yesu  alipozungumza   na   mwanamke   Mkananayo:  Akajibu,   akasema,   Sikutumwa   ila   kwa   kondoo   waliopotea   wa  nyumba  ya  Israeli.  

Na   tazama, mwanamke   Mkananayo   wa   mipaka   ile   akatokea,  akampazia   sauti   akisema,   Unirehemu,   Bwana, Mwana  wa  Daudi;  binti   yangu   amepagawa   sana   na   pepo.   Wala   yeye   hakumjibu  neno.   Nao   wanafunzi   wake   wakamwendea,   wakamwomba,  wakisema,   Mwache   aende   zake;   kwa   maana   anapiga   kelele  nyuma   yetu.   Akajibu,   akasema,   Sikutumwa   ila   kwa   kondoo  waliopotea
Wa   nyumba   ya   Israeli.   Naye   akaja   akamsujudia,  akisema   Bwana,   unisaidie.   Akajibu,   akasema,   Si   vema   kukitwaa  chakula   cha   watoto   na   kuwatupia   mbwa.   (Mathayo  15:22-‐26)  Kwa  nini   Yesu   alisema   maneno  makali   kiasi   hiki?  Tangu   mwanzo   Mungu   (huyu   sasa   sio   Allah   tena;   huko  tumetoka   na   tumekuja   kwa   Yahwe)   aliweka   wazi   kabisa  mpango  wake  wa  ukombozi  wa  mwanadamu  utakavyokuwa.

1.  Alimwita   Ibrahimu   atoke   kwa   nyumba   ya   baba   yake   na  taifa  lake   ili   akaanzishe   uzao   mpya   na   taifa   jipya.  
Bwana   akamwambia   Abramu,   Toka   wewe   katika   nchi  yako,   na   jamaa   zako,   na   nyumba   ya   baba   yako,   uende  mpaka   nchi   nitakayokuonyesha;   nami   nitakufanya  wewe  kuwa  taifa  kubwa,  na  kukubariki.  (Mwa  12:1-‐2) 

 2. Mungu  pia  akampa  Ibrahimu  ahadi  hii:  na   katika   uzao   wako   mataifa   yote   ya   dunia  watajibarikia;   kwa   sababu   umetii   sauti   yangu.   (Mwa  22:18).  Ibrahimu   alizaa  wana  wengi.     
             -‐   Kwa  Hajiri   ni   Ishmaeli.
              -‐   Kwa  Sara  ni   Isaka.
               -‐Kwa   Ketura   Zimrani,   Yokshani,   Medani,   Midiani,  Ishbaki,  na  Sua.  

Lakini   wote   waliondolewa   nyumbani   mwa   Ibrahimu,  akaachwa  Isaka  peke   yake.     Kuhusu   Ishmaeli   tunasoma:     Ibrahimu   akaamka   asubuhi   na   mapema   akatwaa   mkate  na   kiriba   cha   maji,   akampa   Hajiri   akimtwika   begani  pake,   na   kijana,   akamruhusu;   naye   akatoka,   akapotea  katika  jangwa  la  Beer-‐sheba.   (Mwanzo   21:14).  

Na  kuhusu  wake  wengine,  tunasoma:  Lakini   wana   wa   masuria   aliokuwa   nao   Ibrahimu,  Ibrahimu   akawapa   zawadi,   naye   akawaondoa   katika  mahali   alipokaa   Isaka   mwanawe,   wakati   wa   uhai   wake,  waende  pande  za  mashariki,   mpaka   nchi   ya   Kedemu.  Kwa  nini   alifanya  hivyo?  

Mungu   aliweka   wazi   mpango   wake   kwa   Ibrahimu,   hasa  siku   ambayo   Sara   alimwambia   amfukuze   Hajiri   na  mwanawe  Ishmaeli:  Mungu   akamwambia   Ibrahimu,   Neno   hili   lisiwe   baya  machoni   pako,   kwa   ajili   ya   huyo   mwana,   na   huyo  mjakazi   wako.   Kila   akuambialo   Sara,   sikiza   sauti   yake,  kwa   maana   katika   Isaka   uzao   wako   utaitwa.  (Mwanzo  21:12)  

3.  Ndio   maana   Yesu   alipoongea   na   mwanamke   Msamaria  pale   kisimani,   alisema   hivi:     Ninyi  mnaabudu   msichokijua;   sisi   tunaabudu  tukijuacho;   kwa   kuwa   wokovu   watoka   kwa  Wayahudi.  (Yoh  4:22)  Kwa  nini   anatumia   neno   ‘watoka’?  Ni   kwa   sababu   unaanzia   pale   kuelekea   mahali   fulani.  

4.  Kwa   hiyo,   wokovu   ilibidi   uanzie   Israeli.   Baada   ya  kutimizwa   yale   ambayo   yalitabiriwa   kufanyika   Israeli,  ndipo   kipawa   kile   kingemwagikia   ulimwenguni   mwote.
  
5.  Tunajuaje  hayo?  Ni   kwa   kurudi   tena   kwenye   ahadi   ya   Mungu   ya   tangu  mwanzo   kwa   Ibrahimu:   na   katika   uzao   wako   mataifa  yote   ya  dunia   watajibarikia   (Mwa   22:18).  
Kwa   hiyo,   kile   ambacho   Yesu   alikuwa   anamwambia   mwanamke  Mkananayo   ni   kwamba,   “Muda   wako   bado.   Subiri   chakula   kiive  hapa   Uyahudi   ndipo   kitapakuliwa   na   kila   mtu   atakaribishwa  mezani.  

Yesu   ni   Mwokozi   wa   ulimwengu   wote   na   sio   wa   Waarabu  peke  yao  au  wa  Wayahudi  peke  yao.  Sikia   maneno   yake:  

  • Marko   28:18-‐19     Yesu   akaja   kwao,   akasema   nao,   akawaambia,   Nimepewa  mamlaka   yote   mbinguni   na   duniani.   Basi,   enendeni,  mkawafanye   mataifa   yote   kuwa   wanafunzi,   mkiwabatiza  kwa  jina  la   Baba,  na  Mwana,  na  Roho   Mtakatifu  

Yohana  8:12     Basi   Yesu   akawaambia   tena   akasema,   mimi   ndimi   nuru   ya  ulimwengu  Yohana  
12:47  Na   mtu  akiyasikia   maneno   yangu,   asiyashike,   mimi   simhukumu;  maana   sikuja   ili   niuhukumu   ulimwengu,   ila   niuokoe  ulimwengu.  

Yohana  3:17  Maana   Mungu   hakumtuma   Mwana   ulimwenguni   ili   auhukumu  ulimwengu,   bali   ulimwengu   uokolewe  katika   yeye.  

Isaya   49:6  naam,   asema   hivi,   Ni   neno   dogo   sana   wewe   kuwa   mtumishi  wangu   ili   kuziinua   kabila   za   Yakobo,   na   kuwarejeza   watu   wa  Israeli   waliohifadhiwa;   zaidi   ya   hayo  nitakutoa   uwe   nuru   ya  mataifa,   upate   kuwa   wokovu  wangu  hata  miisho  ya  dunia.  

CHANGAMKA   KABLA   USIKU   HAUJAINGIA   MAANA   MUDA UMEENDELEA  SANA.  

No comments:

Post a Comment