Thursday, 26 July 2018

Geuka Kulia, Geuka Kushoto..!

Mnamo mwaka 1987, jarida la  The Los  Angeles Times  lilichapisha kisa cha  mtu  mmoja  mwenye  umri  wa  miaka  53  aliyependa  kuteleza  juu ya  theluji.  Bwana  huyu  aliitwa  Ed  Kenan.  Kenan  alikuwa  mfanya biashara aliyependa mchezo wa kuteleza  na alikuwa anafanya mazoezi kisha ashindane katika mashindano  makubwa ya kuteleza wakati  wa    michezo  ya  Winter  Olympics. 

Lakini  kulikuwa  na  kitu kisicho cha kawaida juu ya Ed Kenan: Alikuwa kipofu. Miaka saba iliyokuwa imepita,  Kenan alipoteza uwezo wa kuona,  jicho moja nilipoteza uwezo kisha  lingine likafuata.  Upasuaji aliofanyiwa  mara  mbili haukuweza kuzuia  retina  zake zizipofushe macho yake. Katika  kukabiliana  na  matatizo hayo yasiyoneneka, Kenan  alikuwa  na  uamuzi  wa  kufanya:
  Alikuwa  anaweza kukaa  gizani, na kujisikitikia,  na kukasirika  kwamba maisha yamemwendea  vibaya, au angeendelea  mbele. Kenan alifanya uamuzi—miezi  sita  baada  ya  kupofuka,  alikuwa  anateleza  kwenye theluji  huko  Vail,  Colorado,  Akasema,  “Nilijilazimisha  kupona,” “Niliona  ikiwa  naweze  kuteleza  chini  ya  mlima,  ninaweza  kufanya chochote ninachoamua kufanya.” Mnamo mwaka 1983, Kenan alishinda nishani ya dhahabu katika mashindano  makubwa ya  kuteleza  ya  U.S. Association  of  Blind Athletes  Alpine  Competition  huko Alta,  Utah.  Miaka michache iliyofuata,  aliongeza  idadi ya medali,  kwa kushinda medali  kadhaa za dhahabu na fedha katika mashindano mbalimbali. 

Hata  upofu  haukuweza  kumzuia  Ed  Kenan  kuishi  maisha mazuri kabisa. Alipoulizwa jinsi  alivyoweza  kuteleza  chini ya mlima na kupitia malango  kadhaa  kwenye  eneo  hilo  la  mchezo,  Ed  alisema  kwamba kuna mtu aliyemwelekeza na mtu  huyu  alikuwa anaona. Msaidizi wake  angeteleza  mbele  yake  kuteremka  chini  ya  mlima. 

Wakati  Ed alipohitaji kuongeza kasi zaidi, yule mwelekezi wake, angeongea kwa sauti  ya  juu  na  kusema“Nenda,  nenda,  nenda”    na  walipokaribia yale  malango,  angepaza  sauti  na  kusema “Riiight  turn-Geuka kulia,”  “Leeeft  turn-Geuka  kushoto.”    Kile  Kenan  alichofanya ni kuendelea  mbele  na kuamini  maelekezo ya mwelekezi  wake. Alipofuata  maagizo, angeweza  kufuata  mkondo  wa kuteleza  vizuri sana na kuvuka mstari wa kumalizia mashindano salama.1 Ingawa matatizo unayokabiliana nayo huenda ni  tofauti  na yale  ya  Ed  Kenan,  pengine  yanafanana  na  yako  kwa  kiasi  kidogo tu.

Pengine  unajua kupoteza kitu au mtu bila kutarajia  ni nini. Pengine  unajua  uchungu wa kukabiliana na hali  ya kuvunja  moyo sana. Pengine  unakabiliana  na majibu ya  kutisha kutoka kwa daktari.  Pengine  mtu  au  kitu  ulichodhani kitakuwepo  wakati  wote kimetoweka  ghafla.  Na  pengine  unajiuliza  swali  hili  Je nikate tamaa sasa, au nitafute njia ya kuendelea mbele? Haijalishi umegubikwa na giza la aina gani, hebu nikukumbushe kwamba huko peke  yako. Mungu anaona  yale  unayopitia,  na yuko  hapo  hapo  pamoja  nawe.  Isaya  30:21  inasema,  “na  masikio yako  yatasikia  neno  nyuma  yako,  likisema,  Njia  ni  hii,  ifuateni; mgeukapo kwenda mkono wa kulia, na mgeukapo kwenda mkono wa kushoto.”  Hiyo inamaanisha  Mungu ameahidi kuwa  kiongozi wako. Unapokuwa huoni unakoelekea,  usiogope. Usijifanye kifaurongo!

Wakati  mwingine  kwenda  mbele  kunamaanisha  kuamka kitandani  na  kusafisha  nyumba  yako,  au  kwenda  kazini;  wakati mwingine  kunamaanisha kufuata maelekezo fulani kutoka  kwa Mungu. Vyovyote  vile, iwe rahisi au hali ngumu zaidi, Mungu anataka  tuwe  watendaji  ili  tusidorore  kiroho! Mungu atakuongoza na  utamsikia  akisema  “Riiight  turn-Geuka  kulia,”  “Leeeft  turnGeuka  kushoto.” Kadri  unavyotumia  imani yako zaidi, ndivyo utakavyokuwa  na  imani  zaidi!  Yesu  alisema,  “Kwa  maana  kila mwenye  kitu  atapewa,  na  kuongezewa  tele;  lakini  asiye  na  kitu, hata  kile  alicho  nacho  atanyang’anywa.”  (Mathayo  25:29).  Alikuwa anaongea  juu ya imani iliyohitajika ili mtu achukue hatua  badala  ya kujificha  kwa  woga.  Endelea  mbele—Ni  moja  ya  mambo  makubwa zaidi unayoweza kufanya.

Jimmy J.

No comments:

Post a Comment