Watu wanaopitia msiba au pigo fulani mara nyingi hupitia hatua kadhaa katika hisia zao, kama kulia na kutoweza kujizuia. Hisia hizi zinaweza kutokea na kutoweka bila ya kutarajiwa. Dakika hii mtu yule anaweza kuwa mzima hana neno. Ghafla anajikuta amekumbwa na kuwezwa na huzuni.
Hata watu ambao kwa kawaida hawaonyeshi hisia zao kwa urahisi wanaweza kujikuta wanapatwa na hisia nyingi mno wakati wa msiba au pigo. Mwanamume ambaye kwa kawaida halii anaweza kujikuta analia bila kujizuia mara kwa mara. Kwa ujumla, watu huogopa hisia zao. Na hata kuonyesha majonzi bila kujizuia huwatisha wengine.
Iwapo unapitia wakati mgumu sasa hivi, ninakuhimiza “Usiogope” kwa sababu yale unayopitia sasa yatapita. Ufahamu bora na msaada mwingi kutoka kwa Roho Mtakatifu utakupitisha hata nyakati ngumu zaidi. Watu wengine hukataa kulia au kuonyesha hisia zozote, na hili si jambo jema. Hisia ambazo zimekaliwa ndani yetu zina nguvu nyingi na zinahitaji kuachiliwa na kuondolewa. Iwapo hutoi na kuachilia hisia zako wakati wa msiba au pigo fulani, kama kifo cha mpendwa wako, unaweza kuanza kuliwa ndani yako na hisia hizo na mwishowe zinaweza kuharibu maisha yako kimwili, kiakili na hata jinsi unavyohusika na mambo kihisia.
Kwa maana Mungu ametupatia machozi pamoja na uwezo wa kulia, basi inamaanisha kuwa kutakuwa na nyakati katika maisha yetu ambapo tutahitaji kulia. Biblia inazungumza katika mahali tofauti kuhusu machozi. Kwa mfano, katika Zaburi 56:8, mtenzi anazungumzia chupa ambamo Mungu huyaweka machozi yetu. Ufunuo 21:4 inazungumzia mbingu mpya na nchi mpya itakayoandaliwa siku moja kwa ajili ya watu wa Mungu: “Mungu atayafuta machozi yao.
Hakutakuwa na kifo tena, na wala maombolezo, wala kilio, wala maumivu; maana mambo hayo yote ya awali yamekwisha toweka.” Kuna kulia kunakofaa na kulia kusikofaa. Kulia ili kuondoa hisia mbaya ya huzuni ni bora, lakini jihadhari usianze kujihurumia. Kusipoondolewa, basi kunaweza kuwa kama zimwi ambalo litakufanya uanze kujipinga mwenyewe, ambalo ni jambo lisilofaa.
Huruma ni karama ya Mungu ambayo ameweka ndani ya kila mmoja wetu ili tuweze kuwatambua na kuwageukia ili kuwasaidia wengine wanaoumia mioyoni mwao. Lakini tunapojielekezea huruma hiyo, basi inaweza kutudhuru na kuleta ulemavu maishani mwetu.
Watu pia wanaweza kupatwa na uzoefu wa kujihurumia. Unaweza kufikiri hii ni njia ya kujihudumia, lakini shetani anaitumia kukuzuia usiendelee mbele katika maisha yako. Unahitaji kuwa mwangalifu usitumie machozi yako kuwatawala wengine.
Wakati unapoumia moyoni, unawahitaji wengine wakuonyeshe upendo na ukarimu. Mara kwa mara, hata kama sisi ni watu wenye nguvu na wasiohitaji kuwategemea wengine, tutahitaji kusaidiwa na wengine kwa muda. Lakini tunafaa kukumbuka kwamba ingawa kuna nyakati ambazo tunahitaji usaidizi spesheli, watu wengine hawawezi kutatua shida zetu.
Tunapowatazamia wengine tukitarajia watuondolee shida na uchungu wetu, basi tunakosea. Kwanza, kabisa, watu hawawezi kutupatia kila kitu tunachohitaji. Pili, kuwatarajia wengine wakutane na mahitaji yetu ya kibinafsi ni kuwapatia mzigo mzito kubeba. Hii huharibu mahusiano yetu, hasa ikiwa tabia hiyo ya kuwategemea inaendelezwa kwa muda mrefu. Inaeleweka wakati mwanamke ambaye amempoteza mume wake anawageukia watoto wake ili wajaze pengo lililotokea maishani mwake.
Lakini ni vyema iwapo anafanya hivi kwa njia ya “kujitolea” kwa watoto wake zaidi kwa maana sasa ana muda na wakati wa kufanya hivyo. Lakini iwapo nia yake ni kuwalazimisha watoto hao wachukue jukumu la baba yao, wataichukia hali hiyo.
Kila mtu anafaa kuishi maisha yake, na hata kuwe na upendo kiasi gani kati ya watu wawili, hakuna mtu anayetaka kutawaliwa kwa sababu za ubinafsi au kujipenda kwa mwenziye huyo. Iwapo unapitia uchungu sasa hivi, ninakuhimiza umtegemee Mungu na umwache afanye mabadiliko anayotaka katika mahusiano yako. Anajua kuwa una mahitaji tofauti sasa. Anajua kuna utupu ambao unahitaji kujazwa.
Kila mtu anafaa kuishi maisha yake, na hata kuwe na upendo kiasi gani kati ya watu wawili, hakuna mtu anayetaka kutawaliwa kwa sababu za ubinafsi au kujipenda kwa mwenziye huyo. Iwapo unapitia uchungu sasa hivi, ninakuhimiza umtegemee Mungu na umwache afanye mabadiliko anayotaka katika mahusiano yako. Anajua kuwa una mahitaji tofauti sasa. Anajua kuna utupu ambao unahitaji kujazwa.
Wakati haya yanapotokea, Mungu atajaza pengo hilo iwapo tutamgojea na kutakataa kujaribu kutumia hisia zetu au kuwatawala wengine. Watu hawafanyi hivi kimakusudi. Yawezekana ni kwa sababu tunaumia moyoni au tunatafuta kitu chochote ambacho kinaweza kuondoa uchungu wetu. Lakini Mungu hafanyi uponyaji kwa kumwondolea mmoja mzigo na kumwekea mwingine mzigo ule. Mapigo na misiba hutuacha katika hali ya unyonge, na shetani atajaribu kutuvamia wakati tumechoka kabisa.
Shetani haoni haya kutuvamia hata wakati tumeanguka chini na kushindwa. Yeye huona nyakati hizo tunapokuwa wapweke na wenye uchungu kama nafasi bora ya kutufunga na kutuweka katika majonzi. Kutembea kwa usawa kutamfungia shetani mlango asiingie. Baada ya miaka mingi, nimegundua kuwa ni lazima tujifunze kupitia mambo mengine kwa siri. Hii haimaanishi kuwa hatuwahitaji watu wengine, kwa sababu tunawahitaji. Watu wengine hutumiwa na Mungu kutuletea faraja tunapokuwa tunaumia moyoni. Hata hivyo, iwapo “kuwahitaji” watu maishani mwetu kutapita kiasi kilicho sawa, basi huenda tukamzuia Mungu kufanya kazi katika maisha yetu.
Moja ya faida ya kukosa mtu wa kugeukia isipokuwa Mungu ni kwamba tunapata nafasi ya kuimarisha mizizi yetu “ndani yake”. Yeye ndiye mwamba, msingi ulio imara ambao hautikisiki. Haijalishi kama mengine yanatikisika. Yeye yu imara. Iwapo unaomboleza au u mpweke kutokana na pigo au mkasa fulani katika maisha yako, geuza tukio hilo liwe nafasi nzuri ya kuingia katika uhusiano wa ndani kati yako na Mungu Baba, Mungu Mwana na Roho Mtakatifu.
Kumbuka: Shetani anataka kutumia nyakati kama hizo kukuangamiza, lakini kile ambacho amepanga kikudhuru, kitaishia kuwa baraka kwako, unapoendelea kumtegemea. (Mwanzo 50: 20; Warumi 8:28)
Mtumishi Jimmy J.
No comments:
Post a Comment