Thursday, 26 July 2018

Tafuta Kilicho Kizuri Katika Kila Kitu

Kuna hadithi moja niliwah sikia ya wanaume watatu waliojikuta wanafanya kazi  mahali  pa  kipekee  kabisa.  Wanaume  hawa  walikuwa  wafanya kazi wa kawaida waliokuwa wameajiriwa  ili kusaidia kujenga kanisa  kubwa la  London ambalo  ujenzi wake ulikuwa unaendelea. Kanisa  hili  kubwa  lilikuwa  nimesanifiwa  na  msanifu  majengo maarufu  kwa  jina  Sir  Christopher  Wren  na  lilikuwa  linatarajiwa kuwa kanisa  kubwa lenye  usanifu wa kipekee. Basi mwanahabari mmoja  wa  London  alipokuwa  akiandika  makala  juu  ya  kanisa  hilo kubwa lililokuwa likijengwa aliwauliza  wale  wanaume watatu  swali hili  rahisi:  “Mnafanya  nini  hapa?”  Yule  mwanaume  wa  kwanza akasema  “Ninakata  mawe  kwa  shilingi    10  kwa  siku.”  Yule  wa  pili akajibu  akasema,  “Ninafanya  kazi  hapa  kwa  saa    10  kila  siku.” Lakini  yule  wa  tatu  alitoa  jibu  tofauti  kabisa:  “Ninamsaidia  Sir Christopher  Wren  kujenga  moja  ya  makanisa  makubwa  zaidi  mjini  London.”

Ni  ajabu  sana  jinsi  mtazamo  wako  unavyoweza  kuathiri mtazamo wako  wa maisha?  Kile  unachochagua  kuamini  ni muhimu.  Yule  mfanya  kazi  wa  kwanza  aliamini  pesa  ndiyo  kitu cha msingi. Alipoulizwa juu  ya  kazi yake, jambo la  kwanza aliloliongelea  ni  kiwango cha pesa (jinsi  kilivyokuwa  cha chini) alichokuwa  analipwa. Mfanyakazi wa pili aliamini muda wake ndio uliokuwa muhimu zaidi. Alipoulizwa aeleze  alichokuwa akifanya, bila kusita aliongea  kuhusu  saa nyingi  alizokuwa anatumia kuwa kazini. 


Lakini  mfanya  kazi  wa  tatu  aliamua  kutazama  mbele  zaidi kupita  zile  pesa  alizokuwa  akipata  na muda  aliotumia.  Hakuona mradi  huu kuwa kazi kama kazi zingine. Aliiona kuwa ni fursa ya ajabu—nafasi  ya  kujenga  kanisa  kubwa  sana.  Aliona  yale  mazuri kabisa katika  hali  yake, na hiyo ilimfanya  asisimke  na afurahie  kazi iliyokuwa mbele yake. Ninaamini  moja  ya  mambo  ya  thamani  kabisa  unayoweza kufanya ili uishi  maisha yaliyojaa  matumaini, yenye  furaha,  ya ushindi  ni kuamini yale  mazuri katika  kila hali.  Hilo si jambo  rahisi la  kufanya  wakati  wote.  Ni  jambo  la  kawaida  kupata  makosa  na kupata  wa  kulaumiwa—miili  yetu  hufanya  hivyo  moja  kwa  moja. Lakini  kuona  na  kuamini  yale  yaliyo  mazuri  ndio  uamuzi  bora zaidi. Ni  uamuzi  unaoufanya  kubadilisha  hali  ya  maisha  yako kutoka  hali mbaya hadi hali nzuri. Badala  ya  kufikiria  mabaya  zaidi  ndiyo yatakayotokea,  amini kuwa  mazuri zaidi yatatokoea. 

Muwazie  mazuri zaidi mfanya kazi  mwenzako.  Liwazie  mazuri  zaidi kanisa lako. Mwazie mazuri zaidi mkeo au  mumeo. Iwazie mazuri zaidi afya yako. Wawazie  mazuri  zaidi  watoto  wako.  Waza  mazuri  zaidi  kuhusu maisha  yako ya usoni.  Utashangaa jinsi  mtazamo wako  wote  wa maisha  utakavyobadilika kwa  kuwawazia mazuri watu wengine na hali zako katika maisha. Yesu  alitupa  amri  mpya,  nayo  ni  tupendane  sisi  kwa  sisi  kama alivyotupenda  yeye.  Neno  la  Mungu  linatufundisha  kwamba upendo  wakati  wote  hutumaini  yote  (1  Wakorintho  13:7). 

Kusema kweli,  Maandiko yanasema  kwamba upendo  “huwa tayari  wakati wote  kuamini  yote”  ya  kila  mtu.  Kila  asubuhi waza  kwamba kila kitu  kitakwenda  vizuri  siku  nzima.  Nadhani  ni  kitu  ambacho  lazima tukifanye kwa kukusudia! Unaweza  kuwa kama wale  wafanyakazi wawili wa kwanza ambao walienda kazini  kila asubuhi  na kuona  tu mshahara mdogo na  saa  nyingi  za  kazi  mbele  yao.  Walikuwa  na  mitazamo  iliyokosa hamasa na kuyaona maisha kuwa  kitu kisichopendeza. Au unaweza kuwa kama yule  mfanyakazi wa tatu  aliyeona  nafasi nzuri badala ya  kuona ni kazi tu.  Aliamini kwamba kile  alichokuwa anafanya ni  muhimu,  na  kila  siku  alisisimka  kuhusu  kazi  yake.  Ni  suala  la mtazamo  tu.  Watu  wote  watatu  walifanya  kazi  moja,  lakini  mmoja tu ndiye aliyeifurahia. 

Kila  wakati  ninapoona vigumu  kuwa na  mtazamo chanya juu ya kile ninachokifanya, hunisaidia sana kukumbuka kwamba ninamtumikia Kristo.

Lolote  mfanyalo, lifanyeni kwa  moyo, kama  kwa Bwana,  wala  si kwa wanadamu. Mkijua [kwa hakika]  ya  kuwa mtapokea kwa Bwana  [si  kwa wanadamu] ujira wa urithi. Mnamtumikia Bwana Kristo (Masihi). Wakolosai 3:23-24
Jimmy J.

No comments:

Post a Comment