Sunday, 15 July 2018

Jibu la Mungu Wakati Unapofikiri Siwezi

Mojawapo  ya  vizuizi  vibaya  zaidi  vinavyotuzuia  kuishi maisha ambayo Mungu anataka  uishi  ni ule  mtazamo wa kiakili wa  siwezi. Siwezi  ni tundu lisilokuwa na msamaha lililotengenezwa ili  likuzuie  kuinuka  na  kufikia  kilele  cha  uwezo  wako. 
Hebu  piga taswira  ya  tai  anayependeza  na  asiye  na  manyoya  mengi—ndege ambaye  aliumbwa  ili  apae  kwenye  mabawa  ya  upepo—akiwa amejibanza  kwenye  tundu,  akiwatazama  tai  wengine  wakipaa  juu. Haya  ndiyo  yanayotokea  ukiishi  na  akili  yenye  mtazamo  wa    siwezi. Badala  ya kuishi  maisha uliyoumbwa kwayo, umekwama katika kifungo cha kuwekewa  mipaka na mapungufu. 

Siwezi kuidhibiti hasira  yangu.  Siwezi  kupata  kazi. Siwezi  kusahau  mabaya  niliyotendewa. Siwezi  kuendelea.  Sielewani  na  mke/mume  wangu.  Siwezi  kuruhusu  mtu aniumize tena.  Siwezi  kutatua  tatizo  hili.  Siwezi  kulea watoto  hawa  peke yangu.  Siamini  haya yamenipata.  Siwezi...Siwezi...Siwezi. Tunaweza kuongea mpaka jioni. Hakuna mwisho  wa mambo ambayo watu hufikiria hawawezi kuyafanya. Lakini  umetambua  kipengele  muhimu  katika  orodha  ya  mawazo iliyopita?  

Si.  Siwezi...Siwezi...Siwezi...Si...   Si...Siwezi  ni mtazamo wa kiakili ambao  unajiangalia  mwenyewe. Hautegemei  kusaidiwa na watu wengine, na bila  shaka hautegemei  kusaidiwa na Mungu. Mtazamo  wa  siwezi  huangalia  sehemu  ambazo tuwadhaifu  kabisa na kufanya hitimisho la kukatisha tamaa: Siwezi kukifanya. Hakuna  jipya.
Wanawake  na  wanaume  katika  Biblia walikumbana  na  mtazamo  huu.  Sara  alifikiria,  siwezi kuzaa watoto; nimezeeka sana  (Mwanzo  18:10–12).  Musa  alifikiria,  siwezi kusimama mbele ya Farao; siwezi kuongea vizuri  (Kutoka  6:30).  Gideoni  alifikiria, siwezi  kuwaongoza Waisraeli;  mimi ndiye mdogo  katika  nyumba  ya  baba  yangu  (Waamuzi  6:15). 

Esta  alifikiria,  siwezi kuwaokoa watu wangu; sitaweza  kumwona  mfalme  (Esta  4:11).  Isaya  alifikiria,  siwezi kutoa unabii;  mimi ni mtu mwenye midomo  michafu  (Isaya  6:5–7).  Wanafunzi walifikiria,  Hatuwezi kulisha  kundi hili  lote la watu; tuna mikate mitano tu na  samaki  wawili  (Mathayo  14:  15–18).  Katika  kila  moja  ya  hali hizi,  siwezi  lilikuwa kama tundu la kujijengea,  likijaribu kuwazuia wanawake na wanaume hawa wasitimize mpango wa Mungu kwa ajili ya maisha yao. Lakini  Mungu  kamwe  hakunuia  kwamba  Sara,  Musa,  Gideoni, Esta,  Isaya,  au  wanafunzi  wake  wafanye  chochote  kwa  nguvu  zao wenyewe, kulingana na uwezo wao wenyewe. Alijua wasingeweza...  lakini hilo halikujalisha, kwa sababu yeye  aliweza. Kupitia  Kristo tunaweza  kutenda  chochote  tunachohitaji  kufanya. 

Tunaweza kukabiliana na chochote! Nayaweza mambo yote katika yeye [Kristo] anitiaye nguvu. Wafilipi 4:13 Ilikuwa  kweli:  Sara  alikuwa  amepita  umri  wa  kuzaa  watoto; Musa  hangeweza  kumshawishi  Farao  yeye  peke  yake;  Gideoni hakuwa  na  sifa  zinazofaa  kuliongoza  jeshi;  Esta  alikuwa  hajaitwa kwenda  mbele  ya  mfalme;  Isaya  alikuwa  mtu  mwenye  midomo michafu;  na  wanafunzi  hawakuwa  na  chakula  cha  kutosha  kulisha kundi  la  watu.  Lakini  lengo  la  Mungu  lilikuwa  ni  kushinda  kila siwezi  ili  aweze  kutimiza  mpango  na  lengo  lake.  Watu  hawa  wote walikuwa hawana budi kutambua na kuondoa  mitazamo yao ya “siwezi.” Badala  ya kuangazia udhaifu wao, walichagua  kuangazia nguvu za Mungu, na  matokeo  yakawa ya  ajabu sana. Mungu alitenda  mambo ya ajabu katika maisha  yao na kupitia imani  yao na utiifu wao. Hivyo  ndivyo  ilivyo  hata  kwako  wewe. 

Ninatambua  kwamba kuna mambo unayokabiliana nayo leo ambayo yanaweza kukufanya ukajisemea  hiki siwezi kukifanya.  Siwezi kukabiliana  na hali  hii  tena.  Siwezi kuvumilia hali  hii  tena.  Siwezi kusubiri  jibu. Siwezi kusamehe kamwe. Kama ungejua  yale  ninayopiitia,  ungeelewa.  Siwezi kufanya. 

Lakini  ningependa kukwambia  kwamba  Mungu anajua huwezi ... na hiyo haijalishi, kwa sababu yeye  anaweza. Yesu akawakazia  macho, akasema, Kwa wanadamu  haiwezekani, bali kwa Mungu sivyo; maana yote yawezekana kwa Mungu. Marko 10:27

No comments:

Post a Comment