Ikiwa tunataka kuwapenda watu, lazima tumwache Mungu abadilishe jinsi tunavyofikiri kuhusu watu na mambo wanayofanya. Twaweza kuamini mabaya na kushuku kila kitu watu wengine wafanyacho na kusema, lakini upendo halisi kila mara unaamini kilicho bora.Kile tunachofikiria na kuamini ni chaguo. Chanzo cha dhiki yetu nyingi katika maisha ni kuwa hatudhibiti au kunidhamisha mawazo yetu. Kwa kutochagua kunidhamisha mawazo yetu, huwa moja kwa moja twachagua kuamini mabaya ya mtu au kushuku.
Nabii Jeremiah aliwauliza watu haya, “ *Mawazo yako mabaya yatakaa ndani yako hata lini? (angalia YER 4:14).* Mawazo waliyochagua kufikiria yalikuwa mabaya kwa Mungu. Wakati tunapochagua kuamini kilicho bora, twaweza kuacha kila kitu kiondoke hasa kile ambacho chaweza kudhuru uhusiano wetu mzuri. Nimeokoa nguvu nyingi ambayo ingetumiwa na hasira kwa kusema, “Ingawa wanachosema au kufanya huniumiza, nachagua kuamini moyo wao uko sawa.”
Naendelea kujiongelesha hadi hisia za hasira yangu zianze kufifia.Ninasema mambo kama, Siamini wanaelewa jinsi vitendo vyao vinavyoniathiri. Siamini wangejaribu kuniumiza kimaksudi. Hawaelewi jinsi inavyosikika wanaposema hivyo. Pengine hawahisi vyema kimwili leo au pengine wana tatizo la kibinafsi linalowafanya kutojali jinsi walivyo.” *Ninajua kutokana na ujuzi nilio nao kwamba kuweka kumbukumbu za kimawazo za makosa hutuathiri maisha yetu na hakumbadilishi mtu mwingine.* Mara nyingi hupoteza siku tukiwa tumemkasirikia mtu fulani ambaye hata hatambui kuwa alifanya kitu kinachotuudhi.
Wanafurahia siku yao na sisi twaipoteza yetu. Ikiwa tutaweka kumbukumbu hizo, basi ni kwanini hatuweki kumbukumbu za mambo mazuri watu wanayosema na kufanya kuliko makosa wanayofanya??
Ni rahisi kuona kuwa orodha ya mambo mazuri ni ndefu kuliko ile ya mambo mabaya na nafikiri itakuwa hivyo kwa watu wengi ikiwa watachukua muda kuandika mambo mazuri. Twapaswa kuangalia na kusherehekea mambo mazuri katika ulimwengu na katika watu kwa sababu twashinda uovu kwa uzuri. Kufikiria na kuongea kuhusu mambo mazuri ya watu kutatufanya tutambue mambo ambayo wakati fulani yalituudhi..
Meditate.
Meditate.
No comments:
Post a Comment