Monday, 4 June 2018

Hakuna Kizuri Kitendekacho Kiajali


Ndipo Bwana akaniambia, Umeona vema, kwa maana ninaliangalia neno langu, ili nilitimize. Jeremiah 1:12
Hakuna mageuzi yaliyoubadilisha ulimwengu yaliyotendeka kiajali. Katika baadhi ya mageuzi, yalianza  na watu wachache  tu waliojadili kuhusu mabadiliko  yanayohitajiwa.  Iwapo  matukio haya ya kihistoria  yalizaliwa na ghasia  za  kawaida au yalipangwa, hayakufanyika tu. Yalifanywa maksudi,  kwa kunuiwa, kupendwa na kwa  mkakati maalum. Yalianza  hivi  kwamba  mtu fulani  alikataa kufanya  kitu, mtu fulani  “akaachilia  mambo yafanyike,”  mtu fulani alikataa  kusikiza na akapuuza ilhali  maovu  yalikuwa yamezidi. Mageuzi hutokea kwa sababu mtu fulani huamua kuchukua hatua. 

Biblia imejaa maagizo yanayotuhitaji sisi  kuyatekeleza.  Agizo la kutekeleza  badala  ya  kusikiza ni rahisi, lakini mamilioni  ya  watu hupuuza. Pengine wanafikiri  mambo yatakuwa bora wakijitegemea. Hayawezi. Hakuna kizuri  kitendekacho kiajali. Wakati fulani nilijifunza kwamba maisha yangu yamebadilika na kuwa bora. Kutamani kitu hakutoi matokeo tunayotarajia, bali lazima tuwe wakakamavu kufanya kile  kinachohitajiwa  kufanywa  ili  kuyapata tuyatakayo. Hatutampata  mtu aliyefaulu  ambaye katika  maisha  yake alitarajia  kufaulu na hatimaye akafaulu. Vile  vile, hatutampata  mtu asiyefanya jambo lolote na kisha  akafaulu maishani. Mfano huu pia  unahusu kuwa  sehemu ya  Mageuzi  ya  Upendo. 
Ikiwa  tunataka kuwapenda watu kama  Yesu  alivyoagiza,  ni  lazima tufanye hivyokwa lengo. Haiwezi kutendeka kiajali. Biblia inasema tulitafute lililo jema siku zote     (Wathesalonike 1 5:15). Tafuta ni  neno  lenye  nguvu linalomaanisha “matamanio  makuu, kimbilia, fuata.”  Ikiwa tutatafuta  nafasi, tuna hakika  tutapata  na hilo litatulinda kutokana  na kukaa  tu bila kufanya kitu  na kutozaa  matunda. Ni  lazima tujiulize  ikiwa tuko imara na timamu au kusikiza na kutotekeleza  jambo? Mungu yuko imara na timamu! Ninashukuru  kwamba  Yeye  yuko, lau sivyo  mambo  katika  maisha  yetu yangelizorota  haraka.  

Mungu hakuumba tu ulimwengu na kila kitu tunachokiona  na  kufurahia ndani  yake, Yeye pia anaendelea kuudumisha  kwa sababu  anajua kwamba  mambo mazuri hayatokei kiholela, yanatokea kutokana na matendo yafaayo (Waebrania  1:3). Matendo yanayoongozwa  na Mungu yanatuweka  kuwa  mbali na  hali ya  kutokuwa  na  lakufanya na  kutozaa  matunda na  hivyo  basi  kuwa  kama  kinga  kwetu. Kuwa imara  kufanya  mambo  yafaayo  kutatuzuia  kufanya  mambo  mabaya. Inaonekana  hatuhitaji kujaribu kwa  bidii  kufanya  kile  ambacho  ni makosa;  maumbile  yetu hufuata  mwelekeo huu ikiwa  hatutachagua kile ambacho ni sawa kufanya. Kwa  mfano, hatuchagui ugonjwa,  kile  tunachofaa  kufanya ni kuwa  karibu nao  na  tutaweza  kuambukizwa.  Lakini  ni lazima tuchague afya. Kuwa na afya, lazima kila mara nifanye uchaguzi bora kuhusu  mazoezi, usingizi, na lishe. Lazima  nichague kutokuwa  na mawazo  ya  kunitia wasi  wasi  au  kuwa  na  hamaki  kwa  sababu najua kufanya  hivyo  kutanifanya  nihisi  uchovu na  pengine kusababisha dalili nyingine  zinazoonekana.  Kuwa  na  afya,  lazima  niwekeze vilivyo katika afya yangu, lakini  ninaweza  kuwa mgonjwa  kwa urahisi kwa kutofanya kitu ili kujitunza.

No comments:

Post a Comment