“Roho wa Bwana yu juu yangu, kwani amenipaka mafuta niwahubirie maskini Habari Njema. Amenituma niwatangazie mateka watapata uhuru, vipofu watapata kuona tena; amenituma niwakomboe wanaoonewa. Luka 4:18
Haijalishi kilichotokea katika maisha yako kusababisha huzuni na upweke, unaweza kuwa na uhakika kwamba Mungu atakuongoza katika kupokea uponyaji wako. Naye atakuonyesha wakati ambapo utakuwa unakubalia hisia zako kwenda mrama au kupoteza usawa wako - iwapo utakubali kumsikiza Roho wake. Haiwezekani kwetu kukadiria kiasi cha wakati ambao unafaa kutumika katika kuomboleza kwa sababu hali na watu ni tofauti. Lakini, hata kama itachukua muda mrefu kiasi gani, kutakuwa na wakati ambapo Bwana atasema, “Sasa ni wakati wako wa kuamka na uendelee mbele. Ni lazima uachane na hayo ya kale nawe umalize mbio ambayo nimekuwekea katika maisha yako.
Sitakuacha, wala sitakupungukia, hivyo kuwa shujaa na hodari, na usonge mbele!” Kila Tukio ni Tofauti Kwa kawaida, miezi sita ya kwanza wakati wa kuomboleza ndio muda mgumu kabisa. Muda huu unaweza kupita au kupungua miezi sita kulingana na hali ya mambo. Kuna mambo tofauti katika kila msiba ambayo ni tofauti kwa kila moja.
Ughafla wa msiba au ajali. Mtu akiwa mgonjwa kwa muda mrefu, jamii inaweza kuwa imeanza kujitayarisha katika nia na mawazo yao kwa kifo cha mpendwa wao. Iwapo kifo ni cha ghafla na hakikutarajiwa, basi pigo linaweza kuwa kubwa zaidi na gumu kukabiliana nalo.
Uwepo au ukosefu wa jamii kukufariji. Kwa mfano, ikiwa mme au mke amekufa, inakuwa afadhali ikiwa kuna watoto walioachwa ambao wanaweza kumfariji mzazi aliyeachwa. Iwapo mtoto amekufa, basi watoto wengine wanaweza kusaidia kujaza pengo aliloacha. Hali ya uhusiano kati ya mwenye kufa na aliyeachwa. Ikiwa uhusiano ulikuwa mwema na wa karibu, basi kipindi cha kuomboleza kinaweza kuwa kirefu na kigumu kuliko kama uhusiano haukuwa wa kuridhisha sana.
Utu wa mwenye kuachwa. Hii ni kweli hasa wakati mke au mume anaachwa na mwenzi wake. Watu wengine huwategemea wengine sana na hii huwachukua muda mrefu zaidi kuchukua uongozi na kuendelea na maisha.
Kina cha uhusiano kati ya mwenye kuomboleza na Yesu Kristo. Hili ni jambo la msingi. Mara nyingi, msiba au ajali huwafanya watu waanze kutafuta uhusiano na Bwana, ambao huleta faraja. Lakini mtu ambaye tayari anamjua Bwana, “na nguvu za ufufuo wake” (Wafilipi 3:10), kwa kawaida hupata uponyaji wa haraka kuliko mtu ambaye hakuwa na uhusiano na Bwana au ambaye uhusiano wake naye ulikuwa wa juu juu tu. Kama mfano wa kukueleza ninachomaanisha kuhusu vipindi tofauti vya kuponywa kutokana na msiba.
Ningependa kushiriki nawe mifano miwili ambayo ninaijua mimi mwenyewe.
Mfano wa kwanza: Ninamjua mwanamke mmoja Mkristo ambaye alikuwa na uhusiano wa karibu na Bwana na kutembea naye kwa miaka mingi. Walikuwa wameoana na mumewe kwa muda wa miaka ishirini na tano au zaidi. Ingawa mumewe alikuwa Mkristo, hakuonyesha matunda yoyote katika uhusiano wake na Bwana. Yeye hakumtendea mke wake mema, na hii ilikuwa imeendelea kwa muda wa miaka mingi. Mtu huyu aliiweka biashara yake mbele ya kitu kingine chochote.
Alikuwa mchoyo na mwenye kujipenda kiasi cha hata kumdhulumu mke wake na kukataa kumtimizia mahitaji yake. Mwanamke huyu alipokuwa anaendelea kutembea na Bwana, Mungu alimpa ombi maaulum kwa ajili ya mume wake, alimwonya kuwa iwapo hangetubu na kumgeukia Mungu, basi angekufa baada ya miezi sita. Mwanamke yule aliendelea kuomba, naye mume akaendelea kupuuza maonyo na mwito wa Bwana. Kwa sababu ya ukaidi wake, alimfungulia shetani mlango naye akayafupisha maisha yake. Mtu huyo aliishia kufa kutokana na mshituko wa moyo. Ingawa kifo chake kilikuwa jambo gumu kwa mkewe, haingeweza kulinganishwa na mtu aliyekuwa na uhusiano mwema na mumewe. Mungu alikuwa amemuonya mwanamke huyu, na hii ilikuwa imemtayarisha. Niligundua kuwa wakati aliochukua kupokea uponyaji ulikuwa mfupi sana. Kulikuwa na mambo ambayo ilimbidi ashughulikie - mambo ya kifedha na kadhalika – lakini ilimchukua muda mfupi kuweza kuanza maisha mapya.
Mfano wa pili:
Mfano wa pili unamhusisha shangazi yangu. Yeye na mjomba wangu walikuwa wamejuana wakiwa wangali watoto na walifunga ndoa shangazi yangu alipokuwa na miaka kumi na mitano naye mjomba akiwa na miaka michache kumliko yeye. Katika siku za kukua kwake, shangazi yangu hakuwahi kuwa na mchumba mwingine au kufanya urafiki na mvulana mwingine.Walikuwa hawawezi kupata watoto, na hii iliwaleta karibu sana. Walifanya kazi pamoja katika kiwanda chao cha kuoka mikate kwa zaidi ya miaka thelathini. Walifanya kila kitu pamoja, wakimtumikia Mungu kama wenzi.
Mfano wa pili unamhusisha shangazi yangu. Yeye na mjomba wangu walikuwa wamejuana wakiwa wangali watoto na walifunga ndoa shangazi yangu alipokuwa na miaka kumi na mitano naye mjomba akiwa na miaka michache kumliko yeye. Katika siku za kukua kwake, shangazi yangu hakuwahi kuwa na mchumba mwingine au kufanya urafiki na mvulana mwingine.Walikuwa hawawezi kupata watoto, na hii iliwaleta karibu sana. Walifanya kazi pamoja katika kiwanda chao cha kuoka mikate kwa zaidi ya miaka thelathini. Walifanya kila kitu pamoja, wakimtumikia Mungu kama wenzi.
Wote walikuwa wamepitia magonjwa pamoja mara nyingi katika maisha yao na walitumia muda mwingi wakitunzana. Wakati mwingine, watu wanapokuwa pamoja na kusaidiana kwa muda mrefu, ndivyo wanavyoendelea kuwa marafiki wa karibu. Walikuwa na uhusiano wa kina kati yao. Walikuwa wanaambatana kama chanda na pete. Walikuwa na nyakati za kufurahia pamoja: wakivua samaki, kupika, kuenda kanisani pamoja, n.k. Ingawa mjomba alikuwa ameugua kwa muda mrefu, kifo chake kilikuwa ni pigo kubwa sana kwa shangazi yangu. Wakati huo shangazi alikuwa amelemazwa na ugonjwa wa kuugua mifupa katika magoti yake lakini hangeweza kufanyiwa upasuaji kwa sababu aalikuwa anugua maradhi ya moyo pia. Kwa sababu hii, ilimbidi aendelee kukaa nyumbani peke yake kwa miaka mingi baada ya kifo cha mumewe na hii iliongeze uzito kwa msiba ule. Kwa sababu ya hali hii ngumu, uponyaji wake ulichukua miaka kadhaa.
Kuomboleza ni Jambo la Kawaida, Kuishi Ukiwa na Maombolezo si Vyema Kutokana na mifano hii miwili, tunaweza kuona jinsi hali moja ya msiba inaweza kuwaathiri watu wawili kwa njia tofauti sana. Ingawa hatuwezi kusema kwa hakika muda wa kuomboleza unafaa kuwa urefu upi, ni muhimu kwa mwenye kuomboleza apige hatua kuelekea uponyaji. Mara ya kwanza, inaweza kuwa vigumu kupiga hatua hizo, lakini ni muhimu kwamba hata kama ni baada ya muda, mabadiliko thabiti yaanze kuonekana. Kama kidonda kinachopona, mtu anaweza kuhisi uchungu kwa muda mrefu, lakini uponyaji kamili huendelea kuja siku hadi siku. Wakati kidonda kinapokataa kupona, basi hii huashiria kwamba kuna kitu ambacho kinahitaji kuponywa kabisa kwanza. Ninaamini ya kuwa hivyo pia ndivyo ilivyo na vidonda katika hisia na nafsi zetu. Nia na hisia zetu zinahitaji kupona kama vile sehemu za miili yetu. Mungu alitupatia hisia kama vile alivyotupatia miili. Amekutana na mahitaji ya uponyaji wa hisia zetu na pia uponyaji wa miili yetu ndani ya Yesu Kristo. Hii ni haki yetu kama Wakristo.
Usiamini uongo wa shetani. Atajaribu kukuambia kwamba hutawahi kuushinda uchungu, hutawahi kuwa mzima tena katika hisia zako. Ingawa ni kweli kwamba pengine utaendelea kumkosa mtu au kitu ambacho umepoteza, hiyo haimaanishi kuwa utaishi chini ya huzuni na upweke milele. Baada ya muda, huzuni inafaa kuisha nawe uweze kuingia katika msimu mpya maishani mwako. Iwapo mabadiliko haya hayafanyiki katika muda ulio sawa, hii ni ishara ya kwamba pengine kuna shida mahali fulani: pengine una nia mbaya, unakataa kuukubali ukweli, au pengine una hofu kuu ambayo haistahili kuwepo. Ukitumia muda kulitafakari neno na kumtafakari Mungu, haijalishi shida yako ni ipi, Mungu atakuonyesha na kukufunulia mzizi wa shida hiyo.
Usisahau kuwa kuomboleza ni hali ya kawaida, lakini kuishi na roho ya huzuni si vyema.
No comments:
Post a Comment