Thursday, 7 June 2018

Jifunze Kusikiliza

Rafiki yangu  mmoja  alikuwa  akiongea  nami kuhusu mwanaume mmoja  kijana  katika  kanisa  lake ambaye alikuwa  na meno yaliyokaa  vibaya.  Yalikuwa  yamekaa  vibaya  hivi kwamba alikataa  kutabasamu  kwa  sababu alifedheheka wakati  mtu yeyote alipoyaona.  Kiukweli Nilimhurumia wakati niliposikia  hadithi yake na sikuweza cha kufanya.

Ni mara  ngapi  tunaposikia  kuhusu kitu kama hicho, tunaposikia huruma  na kisha tukaondoka  bila hata  kufikiria iwapo  au  la  twaweza  kufanya  kitu cha  kusaidia?  Nafikiri si mara nyingi. Twahitaji  kuelimishwa  na kufunzwa mara  kwa  mara. Twahitaji  kubuni tabia  mpya.  Badala  ya  kudhani kuwa  hakuna kitu tunachoweza  kufanya,  twapaswa  kufikiri  kuhusu  hali hiyo. Kumbuka, Waraka  wa  kwanza  wa  Yohana  3:17 inasema: “Lakini mtu akiwa  na riziki ya  dunia, kisha akamwona  ndugu yake ni mhitaji, akamzuilia  huruma zake, je! Upendo  wa  Mungu  wakaaje Ndani yake huyo?.


Kila wakati tunapofanya  jambo  la kuimarisha maisha  ya mtu mwingine  au kupinga maovu, twapeleka  tumaini  katika  kile kinachoonekana  kuwa  jamii iliyokosa  tumaini. Twaweza  kushinda uovu  kwa wema, kwa hiyo tusichoke  katika ari yetu  ya kufanya hivyo..
Mtumishi.
Jimmy J.

No comments:

Post a Comment