Tuesday, 10 October 2017

UFANYAJE UNAPOHISI HISIA ZA NGONO


Kelly anasema: “Mimi hushawishiwa sana kufanya ngono ya kujichua pale tu napohisi kufanya ngono. Nadhani hiyo ni asili yetu sote. Kila mahali unapoenda unahisi kujitosheleza Tu pale unapohisi ngono!”


Je,unahisi kama Kelly? Desturi na maadili ya kale ambayo yaliwakataza watu kufanya ngono ya kujichua yamezorota sana. (Waebrania 13:4) Uchunguzi mmoja uliofanywa katika nchi moja ya Asia ulifunua kwamba vijana wengi kati ya umri wa miaka 15 na 24 wanahisi kwamba kufanya ngono ya kujichua linalokubalika tu bali pia linatazamiwa. Haishangazi kwamba watu wengi ulimwenguni pote hujichua kabla ya kufikia umri wa miaka 19.

Pia, vijana wengine hudhani kwamba dhambi ni ya kujamiana lakini wanajihusisha katika matendo mengine yanayohusiana na ngono kama vile kupapasana viungo vya uzazi. Ripoti moja yenye kushtua katika gazeti la The New York Times ilionyesha kwamba “mara nyingi ngono ya kinywa huongoza kwenye ngono, na vijana wengi huiona kuwa salama kuliko ngono ya kawaida . . . na njia ya kuepuka kupata mimba na kudumisha ubikira wao.”

Mkristo anapaswa kuonaje kujichua? Na vipi kuangalia video za uchi? Je, Mungu anayakubali? Je, ni salama? Na je, kweli yanadumisha ubikira?karibu katika meza ya Vijana

Leo kuna magroup mengi ya kingono na vijana wengi wanazidi kuangamia na si vijana tu,Bali hata watu wazima wameingia katika mrorongo huu wa kuangalia ngono,jambo la kushangaza Shetani amewakamata wengi na kuwa na ujasiri wakutuma video zao za ngono kwenye mtandao.

Biblia inatueleza kwamba wakati mmoja Mfalme Sulemani alimwona kijana akishawishiwa kufanya ngono. Sulemani alimlinganisha kijana huyo na “ng’ombe-dume anayeenda machinjoni.” Ng’ombe-dume anayeenda kuchinjwa hajui kitakachompata.Mara nyingi vijana wanaojihusisha na ngono kabla ya ndoa hutenda vivyo hivyo, kana kwamba hawajui madhara makubwa yatakayowapata! Sulemani alisema hivi kuhusu kijana huyo: “Hajajua kwamba nafsi yake mwenyewe inahusika.” (Methali 7:22, 23) Naam, “nafsi” yako, yaani, uhai wako umo hatarini.

Kwa mfano, kila mwaka mamilioni ya vijana hupata magonjwa ya zinaa ambayo yalisababishwa na kuangalia video za ngono. Lydia anasema: “Nilipojua kwamba nina ugonjwa fulani wa zinaa ambao husababisha vidonda, nilitaka kutoroka.” Anajuta hivi: “Ni ugonjwa unaosababisha maumivu makali sana na hauwezi kuponywa.” Zaidi ya nusu ya watu wanaoambukizwa virusi vya UKIMWI ulimwenguni pote (6,000 kwa siku) wana umri wa kati ya miaka 15 na 24.

Wanawake hasa ndio wanaokumbwa zaidi na matatizo yanayosababishwa na ngono . Kwa kweli, wanawake ndio wanaokabili uwezekano mkubwa wa kupata magonjwa ya zinaa (kutia ndani virusi vya UKIMWI) kuliko wanaume. Msichana mdogo akipata mimba, yeye pamoja na mtoto wake aliye tumboni wamo hatarini. Kwa nini? Kwa kuwa mwili wa msichana huyo haujakomaa vya kutosha kuweza kujifungua bila matatizo yoyote.

Hata msichana huyo akiepuka matatizo makubwa ya afya, bado atakabili madaraka makubwa ya kuwa mzazi. Wasichana wengi huona kwamba kujiruzuku na kumtunza mtoto ni kazi ngumu sana kuliko walivyofikiri.

Kisha kuna madhara ya kiroho na kihisia. Dhambi ya uzinzi ya Mfalme Daudi ilihatarisha uhusiano wake pamoja na Mungu na alikuwa karibu kuangamia kiroho. (Zaburi 51) Ingawa Daudi alipona kiroho, alipata madhara ya dhambi yake muda wote wa maisha yake.

Vijana wanaweza kupatwa na madhara yayo hayo leo. Kwa mfano, Cherie alifanya ngono na mvulana fulani alipokuwa na umri wa miaka 17. Alifikiri kwamba mvulana huyo alimpenda. Miaka kadhaa imepita lakini bado anajutia matendo yake. Anasema hivi kwa masikitiko: “Nilipuuza kweli za Biblia na kupata madhara. Nilipoteza kibali cha Mungu, na hilo liliniumiza sana.” Kijana anayeitwa Trish anakubali hivi pia: “Kosa kubwa nililofanya maishani ni kufanya ngono kabla ya ndoa. Ninatamani sana kuwa bikira tena.” Naam, madhara ya kihisia yanaweza kudumu kwa miaka mingi na kusababisha mfadhaiko na huzuni.

Kujifunza Kujizuia
Msichana anayeitwa Shanda anazusha swali hili muhimu, “Kwa nini Mungu awape vijana tamaa ya ngono, akijua kwamba hawapaswi kuitosheleza kabla ya ndoa?” Ni kweli kwamba tamaa ya ngono inaweza kuwa yenye nguvu sana wakati wa “upeo wa ujana.” (1 Wakorintho 7:36) Kwa hakika, vijana wanaweza kupata tamaa ya ngono ghafula bila sababu yoyote. Lakini hiyo si dhambi. Hilo ni jambo la kawaida katika ukuzi wa viungo vya uzazi.*

Pia ni kweli kwamba Mungu alikusudia mahusiano ya ngono yafurahishe. Hilo linapatana na kusudi lake la awali kwamba wanadamu waijaze dunia. (Mwanzo 1:28) Hata hivyo, Mungu hakukusudia tutumie vibaya nguvu zetu za uzazi. Biblia inasema: “Kila mmoja wenu ajue jinsi ya kukiweza chombo chake mwenyewe katika utakaso na heshima.” (1 Wathesalonike 4:4) Ni upumbavu kutosheleza kila tamaa ya ngono kwani ni kama kumpiga mtu kila unapokasirika.

Mahusiano ya ngono ni zawadi kutoka kwa Mungu ambayo inapaswa kufurahiwa wakati unaofaa, yaani, baada ya mtu kufunga ndoa. Mungu anahisije tunapojaribu kufurahia ngono kabla ya ndoa? Wazia umemnunulia rafiki yako zawadi, lakini kabla ya kumpa anaiiba! Je, hungekasirika? Fikiria jinsi Mungu anavyohisi mtu anapofanya ngono kabla ya ndoa au kujichua na kutumia vibaya zawadi ambayo Mungu ametoa.

Ufanyeje kuhusu hisia zako za ngono? Jifunze kuzizuia.
Kumbuka kwamba “Mungu mwenyewe hatawanyima jambo lolote jema wale wanaotembea bila kosa.” (Zaburi 84:11) Kijana anayeitwa Gordon anasema: “Ninapoanza kufikiri kwamba si vibaya kufanya ngono kabla ya ndoa, mimi hutafakari kuhusu madhara ya kiroho na kutambua kwamba sipaswi kuruhusu dhambi yoyote iharibu uhusiano wangu na Mungu.” Huenda isiwe rahisi kujizuia. Lakini kama vile kijana anayeitwa Adrian anavyotukumbusha, “kujizuia hukuwezesha kuwa na dhamiri safi na uhusiano mzuri na Mungu, na kukazia fikira mambo ya maana zaidi bila majuto wala masikitiko yoyote.”—Zaburi 16:11.

Kuna sababu nyingi nzuri za ‘kujiepusha na uasherati’ wa aina yoyote. (1 Wathesalonike 4:3) Ni kweli kwamba si rahisi kufanya hivyo nyakati zote.
Nikauambia moyo wangu,Haya,nitakujaribu kwa njia ya furaha basi ujifurahishe kwa anasa.Na tazama,hayo nayo yakawa ubatili.Mhubiri 2;1 Hivyo ndivyo alivyosema Suleiman pamoja na anasa zote lakini mwishowe alitambua Ni Ubatili mtupu.
Tafakari
Jihoji
Chukua Hatua.
Sheikh mstaafu.

No comments:

Post a Comment