Mageuzi. Neno lenyewe linaibua tumaini, linawasha hamu na kuvutia uaminifu kama neno ambalo halijawahi kupatikana kwenye msamiati wa binadamu. Katika historia, wazo la maguezi limemimina mafuta kwenye moto na kusisimua ujasiri kwa waliovunjika moyo.
Mageuzi yamewakusanya pamoja wale wanaotafuta sababu kubwa kuliko wao wenyewe na yamewapa wanawake na wanaume waliokosa mwelekeo hapo awali, sababu ya kujitoa mhanga.
Wamewazaa viongozi mashuhuri na kuwalea wafuasi mashuhuri, wameubadili kabisa ulimwengu. Mageuzi ni jambo la ghafla, kubwa na lililo tofauti kabisa na jinsi mambo yalivyo kama kawaida.
Mageuzi huchochewa na mtu mmoja au kundi dogo sana la watu wasiokubali kuendelea kuishi kama walivyokuwa siku zilizopita.
Wanaamini kuwa lazima jambo fulani lifanyiwe mabadiliko na huendelea kuimarisha mawazo yao hadi pale msingi wao unapoanzia na hilo hatimaye huleta mabadiliko kwa njia kubwa.
Nimeishi kwa muda wa miaka ishirini na kadhaa ninapoandika kitabu hiki, na ninadhani kwamba nikiwa peke yangu nimejua mambo machache tu. Ninaweza kusema nimeishi kwa muda mrefu kiasi, kuweza kujaribu njia mbali mbali za kupata furaha na nimegundua jambo hilo kwa kufanya chaguo kuhusu kile kinachofanya kazi na kisichofanya kazi.
Uchoyo haufanyi maisha kuendelea kama yalivyonuiwa na hivyo basi haupo kwenye mpango wa Mungu kwa binadamu. Ninaamini ninaweza kuthibitisha katika kitabu hiki kwamba uchoyo kwa kweli ndilo tatizo kuu linalotukabili hivi leo ulimwenguni na kwamba juhudi kubwa za kuuangamiza uovu huu ndilo litakalokuwa jibu letu. Twahitaji kutangaza vita dhidi ya uchoyo. Twahitaji Mageuzi ya Upendo.
Upendo lazima uwe zaidi ya mtazamo au neno, lazima utekelezwe kwa vitendo. Lazima uonekane na watu wauhisi. Mungu ni Upendo! Upendo umekuweko na kila mara utakuwa wazo lake Mola. Alikuja ili kutupenda, kutufunza jinsi ya kumpenda Mola, na kutufunza jinsi ya kujipenda na kuwapenda watu wengine.
Tunapofanya hivi maisha yatakuwa mema; tusipofanya hivi hakuna kinachofanyika kwa njia nzuri. Upendo ndilo jibu la uchoyo kwa sababu upendo hutoa, ilhali uchoyo huchukua. Lazima tukombolewe kutoka kwa nafsi zetu, na Yesu alikuja kwa kusudi hili kama tunavyoona katika 2 Wakorintho 5:15 “ ?Tena alikufa kwa ajili ya wote, ili walio hai wasiwe hai tena kwa ajili ya nafsi zao wenyewe, bali kwa ajili yake Yeye aliyekufa akafufuka kwa ajili yao.”
Nimekataa kusimama kutazama bila kufanya lolote ilhali ulimwengu unazidi kudidimia. Huenda nisiweze kutatua matatizo yote ninayoyaona, lakini nitafanya lile niwezalo. Ombi langu ni kwamba uungane nami katika kuchukua msimamo dhidi ya ukiukaji wa haki na kuwa tayari kuleta mabadiliko katika njia ya maisha unayochagua. Maisha si kuhusu kile ambacho wengine wanaweza kutufanyia sisi, bali ni kuhusu kile tunachoweza kuwafanyia wengine.
Ninachagua huruma na kusalimisha misamaha yangu. Ninapinga maovu na kujitolea kufanya matendo ya Upendo wa Mungu. Ninakataa kutofanya lolote. Huu ndio uamuzi wangu. MIMI NI MAGEUZI YA UPENDO.
Ninaomba kwamba maneno haya pia yatakuwa wito wako, mtindo mpya utakaouzingatia maishani. Usisubiri kuona kile mtu mwingine anachochagua kufanya na usisubiri kuona ikiwa vuguvugu limeanza kuwa maarufu. Hili ni jambo ambalo lazima wewe mwenyewe ufanye uamuzi, kujitolea ambako wewe peke yako lazima uchague kukufanya.
Hebu jiulize, “Je, nitaendelea kuwa sehemu ya tatizo hili au nitakuwa sehemu ya jibu?” Nimeamua kuwa sehemu ya jibu. Upendo ndio utakaokuwa mwito wa maisha yangu.
Na je, wewe? Utachochea matatizo yaliyoko ulimwenguni? Utayapuuza au kujifanya kuwa huyaoni? Au utajiunga na Mageuzi ya Upendo?
Karibu ujipatie Nakala ya kitabu hiki.
No comments:
Post a Comment