Tuesday, 25 September 2018

Mimi ni Mageuzi ya Upendo.

Ninachagua huruma na kusalimisha misamaha yangu. Ninapinga maovu na kujitolea kufanya matendo ya Upendo wa Mungu. Ninakataa kutofanya lolote. Huu ndio uamuzi wangu. MIMI NI MAGEUZI YA UPENDO.- Imani yetu.

Mageuzi ni  jambo la ghafla, kubwa  na lililo  tofauti kabisa na jinsi  mambo yalivyo kama  kawaida.  Mageuzi huchochewa  na mtu mmoja au kundi  dogo sana la watu wasiokubali  kuendelea  kuishi kama  walivyokuwa  siku zilizopita.  Wanaamini  kuwa  lazima  jambo fulani lifanyiwe mabadiliko  na  huendelea  kuimarisha  mawazo yao  hadi pale msingi wao  unapoanzia  na hilo hatimaye huleta mabadiliko kwa njia kubwa.


Mageuzi yamewakusanya pamoja  wale wanaotafuta  sababu kubwa  kuliko  wao  wenyewe na  yamewapa wanawake na wanaume waliokosa  mwelekeo hapo  awali, sababu ya kujitoa mhanga. Wamewazaa  viongozi mashuhuri  na kuwalea wafuasi mashuhuri, wameubadili kabisa ulimwengu.
Thomas  Jefferson alisema “ Kila kizazi chahitaji  mageuzi  mapya ”  na ninaamini  huu  ndio  wakati wa  mageuzi yajayo  ya  Ulimwengu, mageuzi makuu sana  kwa  watu wote. Hatuhitaji mageuzi sawa na yale yaliyoharibu  nchi  ya historia ya ulimwengu katika vizazi vilivyotutangulia,  hatuhitaji mageuzi yanayozingatia  siasa,  chumi, au  teknolojia.  Twahitaji  Mageuzi  ya Upendo.

Twahitaji  kupindua hali  ya  uchoyo,  hali  ya  kuishi katika ubinafsi  maishani mwetu. Hakuna kitakachobadilika  katika ulimwengu  wetu  hadi pale kila mmoja wetu  atakapokuwa  radhi kubadilika.  Mara nyingi  huwa tunatamani ulimwengu ubadilike bila ya kukoma kutambua kwamba  hali ilivyo ulimwenguni inatokana  na  njia tunazoishi  katika  maisha  ya  ubinafsi na  chaguo tunalofanya kila siku. Ikiwa kila mmoja hapa  duniani  anafahamu  jinsi  ya kupokea na kuonyesha  upendo, dunia yetu ingelikuwa mahali tofauti  kabisa pa  kuishi. Nafikiri sote  twafahamu  kuwa  kuna jambo  lililo  kasoro katika  jamii na kwamba  lahitaji  kutatuliwa.  Lakini  hakuna  mtu anayefahamu kinachopaswa  kufanywa  au jinsi  ya  kuanza  kufanya mabadiliko.  Jibu letu kwa  ulimwengu usioweza  kuthibitika ni kulalamika na  kufikiri,  kuna  mtu  anayepaswa  kufanya jambo  fulani.

Tunafikiri  na kusema  kuwa pengine  Mungu  au serikali  au mtu mwingine  yeyote aliye  kwenye mamlaka  anahitajika  kufanya kitendo. Lakini  ukweli ni kwamba  kila mmoja wetu anahitajika kufanya  jambo  fulani. Lazima  tujifunze  kuishi maisha  yenye mwelekeo tofauti kabisa  na tulivyo sasa.  Lazima tuwe radhi kujifunza, kubadilika na kukubali kwamba  sisi ni sehemu  ya  tatizo lililoko. Hatuwezi kutatua  kile tusichoelewa,  kwa  hiyo  hitaji  letu la kwanza  ni  kutafuta  chanzo cha  tatizo lililoko.
Ni kwanini watu wengi hawana furaha? Ni kwanini ghasia zimeongezeka sana katika familia, maeneo jirani,  miji na  mataifa?  Ni kwanini watu wana hasira  nyingi? Unaweza  kufikiri  kuwa  mambo  haya  yanatendeka kwa  sababu ya dhambi. Unaweza  kusema “Watu ni wenye dhambi. Hilo ndilo tatizo.”  Nakubali usemi  huo,  lakini ningependa kulikabili tatizo  hili kwa  mtazamo  wa  vitendo tunavyokumbana  navyo kila siku. Ninaamini kikamilifu  kuwa  chanzo  cha  maswala  haya  na mengine  ni  Uchoyo.

Uchoyo kwa  kweli  ndio  chanzo  cha  dhambi. Ni mtu kusema, “Ninataka  kile  ninachokitaka  na nitafanya kile ninachohitaji  kufanya  nipate nikitakacho.”  Dhambi huweko  wakati mtu anapofanya kinyume na mapenzi ya Mungu na njia Zake. Tunaishi “nyuma”  kinyume  kabisa na tunavyopaswa kuishi. Tunaishi kwa  kujijali sisi wenyewe ilhali hatupati  kile kinachoturidhisha.  Twapaswa  kuishi  kwa  kuwajali  wengine na tujifunze  siri ya  ajabu kwamba  kile tunachotoa  huturudia kikiwa kimeongezeka zaidi ya maradufu.
Ninapenda sana  jinsi  daktari mmoja mashuhuri  kwa  jina Luka  alivyosema.  “Yatoe maisha  yako, nawe utaregeshewa  maisha  hayo,  lakini sio kuregeshewa  maisha tu,  utaregeshewa  pamoja  na  bakshishi na  baraka.  Kutoa  wala  sio kupokea  ndio  njia.  Ukarimu hulipwa  ukarimu.”  (LK 6:38  The Message).
Katika  jamii nyingi, urithi, umiliki  na  uthibiti ndilo lengo  kuu la watu wengi. Kila mmoja  anataka  kuwa  wa  kwanza  kumiliki, hii  ikionyesha moja kwa  moja kwamba  watu wengi  watakasirika kwani ni  mmoja tu atakayekuwa wa  kwanza  kila wakati katika sehemu  yoyote. Ni mtu mmoja tu anayeweza  kuwa wa  kwanza katika  mashindano ya  mbio duniani,  ni mtu mmoja  tu anayeweza kuwa  rais wa  kampuni au mchezaji  sinema bora. Ni mtu mmoja tu anayeweza kuwa mwandishi  bora wa  kitabu au mchoraji bora duniani.  Ingawa ninaamini  kuwa tunapaswa kuwa na lengo na kujitahidi, siamini  kuwa  tunapaswa  kutaka  kila kitu kiwe chetu na kutowajali watu wengine..

Nimekataa  kusimama kutazama  bila kufanya lolote ilhali ulimwengu unazidi kudidimia. Huenda nisiweze kutatua matatizo yote  ninayoyaona,  lakini nitafanya  lile  niwezalo.  Ombi langu  ni kwamba uungane nami katika kuchukua msimamo dhidi ya ukiukaji wa  haki na kuwa  tayari kuleta mabadiliko katika  njia ya  maisha unayochagua.  Maisha  si kuhusu kile ambacho  wengine wanaweza kutufanyia sisi, bali ni kuhusu kile tunachoweza  kuwafanyia wengine.
Kila  vuguvugu lahitaji maudhui  au wito wa  kuendeleza. Sisi  katika  huduma  ya  Mageuzi ya Upendo tumeweka nadhiri kupitia maombi tuliyojitolea  kuzingatia  maishani.  Je,  utaungana nasi?

Pata Nakala yako ya Mageuzi ya Upendo tujifunze pamoja.
Jimmy J.
Mwana Mageuzi

No comments:

Post a Comment