Tuesday, 4 September 2018

Vaa Miwani Yako Ya Mungu

Natuvae  kile  ninachoita  “Miwani  ya  Mungu,”  ili  tuangalie  mambo fulani  kwa  mtazamo  wa  Mungu.  Yeye  anaona  mambo  kwa  njia tofauti  sana kuliko  tunavyoona kwa sababu anaona mwisho  kutoka mwanzo. 

Je, Mungu anakuonaje? Anakupenda zaidi  ya  jinsi unavyoweza kuelewa,  na ana mpango mzuri kwa maisha yako. Huko  peke yako kwa sababu yuko  pamoja nawe  wakati  wote. 

Msamaha wa Mungu ni mkuu  kuliko  dhambi yoyote  uliyotenda. Huruma zake ni mpya kila siku.  Mungu amekupa wewe  kama muumini, nguvu, na huna haja ya kuishi  maisha ya kushindwa.
Umefanywa  kiumbe kipya kabisa katika Kristo, umepewa maisha  mapya, na unaweza kuyaacha yote  yaliyopita  na utazamie  kwa hamu mambo yaliyo mbele  yako.  Utakapojua  wewe  ni  nani  katika  Kristo—na  jinsi Mungu anavyokuona kwa sababu ya sadaka ya Mwanawe—mfumo wa maisha yako utabadilika.

 Mungu aliangalia  kila kitu alichokiumba na akasema  ni chema sana  (Mwanzo  1:31).  Wewe  ni  sehemu  ya  vitu  alivyoumba,  wewe ni  mzuri  sana.  Lakini  tunaweza  kuona  vigumu  kuamini  maneno hayo. Siongei kuhusu  mwili wako. Mtume Paulo alisema,  “Kwa maana  najua ya  kuwa ndani yangu,  yaani,  ndani ya  mwili wangu, halikai  neno  jema.”  (Warumi  7:18).  Miili  yetu  ina  kasoro,  na  sote hufanya  makosa.  Mungu  anaposema  “Wewe  ni  mzuri,”  anaongea juu ya kuumbwa upya kwako kwa kiroho! 

Maana  tu kazi  yake [mwenyewe], tuliumbwa  katika  Kristo  Yesu, [tumezaliwa  upya] ili  tutende matendo  mema, ambayo  tokea  awali Mungu aliyatengeneza ili tuenende nayo. Waefeso 2:10

Ni  muhimu  sana  tukielewa  uhalisia  wa  kuwa  kiumbe  kipya  na tuanze  kujitambulisha  nao.  

Watu  wengine  hutenda  mabaya  kwa sababu  wanafikiri  kwamba  ni  wabaya—wanaamini  ni  wabaya. Mara  kwa mara  watu  huishi  wakiwa wamekwama  katika  mtindo mbaya wa maisha kwa sababu hawaamini kwamba wamewekwa huru  kupitia  Kristo.  Wanaangalia  jinsi  walivyokuwa  wakati  wote na  hawaelewi  nguvu  halisi  za  kuzaliwa  upya

—Hata  imekuwa,  mtu akiwa  ndani  ya  Kristo  amekuwa  kiumbe  kipya;  ya  kale  yamepita, tazama! Yamekuwa mapya (2 Wakorintho 5:17).

 Hata ingawa ni vigumu kuelewa  na kuamini  kweli, Mungu  sasa anatuona kuwa watu wenye haki kupitia Yesu. 

Yeye asiyejua dhambi  alimfanya  kuwa  dhambi  kwa  ajili  yetu,  ili sisi tupate kuwa haki ya Mungu katika Yeye. 2 Wakorintho 5:21

Mimi kama  mtu  niliyehisi “nimekosea”  katika  sehemu kubwa ya maisha yangu, kujifunza  kuhusu  mafundisho  ya haki kupitia Kristo kulikuwa kunaniweka  huru  ajabu na bado  hata  sasa kunaniweka huru.  Napenda  kuwasaidia  watu  waelewe  hili  ili  waache  kujikataa wenyewe kwa sababu wanaona hawawezi kuwa wakamilifu kila siku. Uhusiano  wetu  mzuri na Mungu hautegemei  yale  tunayofanya, lakini unategemea aliyofanya Yesu. Tunapojifunza zaidi na zaidi juu ya upendo, kukubalika, na neema  ya  Mungu,  tutatambua  kwamba matumaini huwa msaidizi wetu  wa wakati wote. Siwezi kukumbuka  ni  lini mara ya mwisho nilihisi sina matumaini!  Tunaweza  kujifunza kumtumaini  Mungu na kuwa  na imani wakati  wote  kwamba tunakua  na kubadilika, Mungu anaona upendo wetu  na jinsi  tunavyojituma  kwake na bado anatuona tuko katika uhusiano mzuri naye. 

Kuna  tofauti  kubwa kati  ya  wewe  ni nani na  kile  unachofanya. Ndiyo  maana  ninawahimiza  watu  watenganishe  “nani”  na  “kufanya.”  Wewe  ni  mwana  wa  Mungu.  Umezaliwa  mara  ya  pili. Umejazwa Roho wake. Badala  ya kuangalia  mwili wako, pata mtazamo wa Mungu  na uangalie  roho  yako. Jione katika kioo  cha Neno  la  Mungu,  na  kisha  usisimke  kuhusu  wewe  ni  nani  katika Kristo Yesu. Pia  ninakuhimiza pia upate  mtazamo wa Mungu katika majaribu  yako.  Yaone  kwa  namna  ambayo  Mungu  huyaona.  Yeye anayaona kuwa ya muda mfupi tu. 

 Hakuna tatizo linalodumu milele, kwa hiyo kuwa na matumaini  kwa sababu ushindi  wako uko karibu  kuliko  unavyoweza  kufikiria.  Unapoangalia  kwa  miwani  ya Mungu, itakubidi useme “Hali hii haitadumu milele  na nitadumu zaidi ya hali hiyo!

” Unapokuwa mahali pagumu na kila kitu kinakuendea vibaya  kiasi kwamba unaona  huwezi  kuvumilia  hata kwa dakika moja  zaidi, usikate  tamaa  kamwe, kwa kuwa hapo ndipo mahali na huo ndio wakati ambao mawimbi yatabadilika. —Harriet Beecher Stowe

Mungu anatamani upitie hali hiyo ukiwa pamoja naye. Tunaweza kuchagua  kuendelea  mbele  au kukata  tamaa.  Mungu hutupa  ahadi yake, lakini ni juu yetu  kusimama  imara  na kusubiri hadi kila dhoruba maishani  mwetu  iondoke.

Bila  shaka  Mungu hutusaidia. Hutoa  neema  yake, nguvu  zake, na kututia  moyo, lakini, hatimaye, lazima  tuamue  kukaza mwendo  au  kukata  tamaa.  Moja ya  faida za majaribu ni kwamba Mungu huyatumia  kutuimarisha dhidi ya mambo magumu. Usiogope, kwa maana  mimi ni pamoja  nawe; usifadhaike, kwa  maana  mimi ni  Mungu wako;    nitakutia  nguvu, naam, nitakusaidia...

Isaya 41:10a Hili ni Andiko zuri sana linalotwambia  kwamba  hata  tunapopitia jambo fulani gumu, Mungu  atatenda  mema kutokana  na hali hiyo. Anafanya mambo mengi, lakini moja ni kwamba anatutia  nguvu zaidi. Tunaimarishwa dhidi ya mambo magumu. Kwa maneno mengine, mambo ambayo awali  yalituudhi,  au  kututisha au  kututia wasiwasi, hayatatusumbua tena kamwe. 

Mtu  anayefanya  mazoezi kwenye  ukumbi wa mazoezi  kwa kuinua  vitu  vizito  atatumuka  misuli,  lakini  wakati  atakapofikia kiwango  fulani, njia pekee  ya kupata  misuli  zaidi ni kuinuia vitu vizito zaidi ya vile vya kwanza. Tunapomwomba Mungu ili atuinue katika sehemu fulani ya maisha  yetu,  tunaweza kumtarajia  Mungu atende  kitu ndani yetu  kabla hajatufanyia kitu kwa  nje.


 Huenda tukasema kwamba lazima tuzoee  kuinua vitu vizito zaidi katika roho. Kwa mfano, tunaweza kumwomba Mungu ili upendo wetu uongezeke zaidi na zaidi, lakini huenda hiyo inamaanisha kwamba tutakuwa  karibu na watu  wengi  zaidi ambao ni vigumu kuwapenda. 

Nakumbuka  wakati  mmoja  nikimwomba  Mungu  anipe  uwezo  wa kuwapenda wale  wasiopendeka!  Baada  ya majuma machache, nilimlalamikia Mungu katika maombi juu ya watu  washindani niliokutana nao, na akanikumbusha  kwamba  siwezi kujifunza kuwapenda  wasiopendeka  ikiwa nitakuwa karibu tu  na watu  wazuri ambao hawawezi kamwe kuniudhi kwa njia yoyote. Tunapomwomba Mungu ili  atutumie  katika  njia kubwa zaidi, sharti tukumbuke kwamba  mtume Paulo alisema kwamba amefunguliwa mlango mkubwa  wa kufaa sana, na wako  wengi wampingao.    (1  Wakorintho  16:9).  

Shetani  hupinga  kitu  chochote kizuri.  Anachukia  ukuaji na maendeleo  ya aina yoyote, lakini tukiendelea  kusimama  imara,  Mungu atakukomboa na sambamba na kutukomboa  atatusaidia kukua  kiroho kupitia mambo hayo magumu. Hiyo haimaanishi kwamba  Mungu ndiye  mwanzilishi  wa matatizo yetu, lakini kwa hakika huyatumia  kutusaidia katika  njia nyingi.  

Wakati  upo  katikati  ya  hali  inayokupa  changamoto  au  ya kuumiza,  jaribu  kufikiria  yale  mazuri  yanayoweza  kutokana  na hali  hiyo,  badala  ya  kufikiria  jinsi  hali  hiyo  ilivyo  ngumu.  Wakati sababu ya kuwa na matumaini inapotoweka, endelea  kutumaini katika imani, kama alivyofanya Abrahamu. Kutokana  mtazamo  wa Mungu, mambo mazuri yanatendeka hata  wakati  unapongoja ushindi  wako au ukombozi wako. Unakuwa  kiroho, unakua katika subira, unavumilia  majaribu, na  utakapoyapita  hayo  utainuliwa.  Na  unamtukuza  Mungu kwa kumpenda  kwa njia  ile  ile  utakayompenda  wakati  hali  zako zitakapobadilika. 

Majaribu  yana  thamani.  Yanaumiza,  lakini  yana  thamani!  Sisi sote  huyapitia,  lakini si wote  wanaoyapitia  kwa mafanikio.  Mara kwa mara  napenda  kusema kwamba baada  ya majaribu (test),  watu wengine  hupata  ushuhuda  (testimony), lakini wengine husalia tu “kuomboleza (moanies).”

No comments:

Post a Comment