Tuesday, 11 September 2018

Mungu Anampenda kila mtu.


Wakristo wengi wanapenda  kuchagua  kuhusu ni yupi wanayemsaidia  na wanayemtia moyo. Wanawatafuta watu kama wao. Baadhi  ya watu hata wanaamini  kwamba  wanapaswa kuwasaidia  watu wengine  wanaoamini  kile wanachoamini  na kufikiria  kama  wanavyofikiria.  Hiyo  siyo  njia    inayopaswa  kuwa. Siyo njia  Yesu alivyofanya. 

Miaka kadhaa iliyopita nilisoma hadithi kuhusu mtu  fulani aliyeanguka  kwenye shimo na hangeweza  kutoka  na jinsi watu wengine walivyomhudumia mtu huyo. 
Mtu mbaguzi alikuja akasema, “Ninakusikitia huko chini.”
Mtu  asiye  mbaguzi  akaja  akasema,  “Aha,  ni  jambo  la  kueleweka kwamba mtu angelianguka huko chini.”



  • Mfarisayo akasema, “Ni watu wabaya wanaoanguka  kwenye mashimo.” 
  • Mtaalam wa hesabu  akafanya hesabu  jinsi  mtu huyo alivyoanguka kwenye shimo hilo. 
  • Mwandishi  wa habari  alitaka  kupata  habari   ya kipekee  kuhusu  mtu huyo katika shimo. Mwanamgambo akasema, “Unastahili shimo lako.” 
  • Mkristo mmoja akasema, Iwapo ungekuwa umeokoka hungeanguka kwenye shimo hilo.” 
  • M’Armenia  mmoja  akasema,  “Uliokolewa  na  bado  ukaanguka kwenye shimo hilo.” 
  • Mtu hodari akasema, “Tubu kwamba humo katika shimo hilo.” Mtu wa kusema yaliyo dhahiri akasema, “sasa hilo ni shimo.”
  • Mtaalamu wa Jiolojia akamwambia afurahie mwamba ulioko katika shimo hilo. 
  • Mfanyikazi wa IRS akamuuliza  ikiwa alikuwa  akilipa ushuru kwa shimo hilo. 
  • Mkaguzi wa baraza akamuuliza  ikiwa ana kibali cha kuchimba shimo hilo. 
  • Mtu wa kujihurumia  akasema, “Hukuona  kitu chochote  mpaka ukaona shimo hilo langu.” 
  • Mdowezi akasema, “Mambo yanaweza kuwa hata mabaya zaidi.” Mtarajia mabaya akasema, “Mambo yatakuwa mabaya zaidi.”


Yesu alipomuona  mtu huyo, akaenda  hadi chini na akamshika mkono na kumuinua hadi nje ya shimo hilo. Yesu  alikuja  ili  kufa  kwa  ajili  ya  watu.    Alikuwa  na  yuko  katika kujishughulisha  na watu. Na  mimi na wewe  twahitaji  kuwa  katika kujishughulisha  na watu pia. Kila mara lazima tukumbuke kwamba  Mungu anampenda kila mmoja, na twahitaji kuwahudumia wengine kwa njia ambayo  Yesu angeliwahudumia.  Twahitaji  kuwatia moyo ili wawe vile  Mungu  alivyowaumba  kuwa. Ninaamini  kwamba  kila  mmoja  anataka kuwa mfariji, na kila mmoja anayemjua  Yesu anataka  kuwa kama  Yesu, hata yule mtu mbaya. 

Kwa nini  nasema  hivyo?  Kwa sababu  ninaamini kwamba sote twataka kuwa washawishi  wema kwa maisha ya wengine. Twataka kuongeza thamani kwa wengine, sio kuchukua kutoka kwao. Kwa hiyo tafadhali niruhusu niwe mfariji wako. Unaweza kuleta tofauti. Unaweza  kuongeza  thamani kwa wengine.  Unaweza  kumwakilisha Yesu vyema  na  siku  moja  ukasikia  maneno,  “Vyema  sana,  vizuri  na  mtumishi mwaminifu.”  Kila mmoja anaweza  kuwa mfariji. Si lazima uwe tajiri. Si lazima  uwe  mwerevu.  Si lazima  uwe  na  uhodari  wa hali  ya juu. Na  si lazima uwe navyo vyote. Unahitaji  tu kuwajali  watu wengine  na kuwa tayari kuanza  kufanya hivyo. Si lazima ufanye kitu chochote kikubwa au cha kutambulika. Mambo madogo unayoweza kufanya  kila siku yana uwezo wa kupata mambo makuu kuliko unavyodhani. 

Shika mtu akifanya kitu fulani kwa njia sawa. 
•Mpe mtu fulani sifa ya kweli. 
•Msaidie mtu fulani anayehitaji msaada. 
•Mpe mtu fulani bega la kuegemea alilie.
*Sherehekea na mtu fulani anayefaulu. 
•Mpe mtu fulani tumaini. 

Unaweza kufanya hivi. Anza  sasa  kwa vitendo.  Na  kumbuka msemo huu ambao ninaupenda  sana. “Ninataraji  kupitia katika ulimwengu  huu lakini mara moja. Jambo zuri lolote ninaloweza  kufanya au ukarimu wowote ninaoweza kuonyesha kwa kiumbe chochote,  wacha nifanye sasa. Wacha nisitofautiane wala kupuuza, kwani sitapitia haya tena.”

Jimmy J.
#MwanaMageuzi

No comments:

Post a Comment