The mission Of Mawaidha Popote is to Prepare the Nations of the world for the coming of Jesus Christ and establishment of the kingdom of God on Earth.our ultimate goal is to achieve a time in history when "the knowledge of the Lord will cover the earth as the waters cover the sea".
Wednesday, 20 March 2019
SAFARI YA MOYO
Nataka kumpigia yowe nimwambie. “TUTAKUTUNZIA” Hii kwa kweli ni sehemu ambayo twahitaji kujikakamua, kuvumilia, kuomba na KUAMINI, na kutoka kwa imani.
Monday, 17 December 2018
Mungu Anakupenda
Monday, 22 October 2018
Barua
Tangu Niende Chuo kikuu Najua sijachukua Muda wa kuwaandikia na Naomba msamaha kukosa kufikiria kuwaandikia paka sasa.Nitawaeleza Mambo yote katika Barua hii lakini kabla hamjasoma Tafadhali ketini chini,Tafadhali msisome paka Mketi chini.
Naendelea Vizuri sasa,Jeraha la fuvu la kichwa baada ya kuruka kwa dirisha la Bweni langu Sasa limepona,Niliruka baada ya bweni langu kushika moto muda mfupi.baada ya kuwasili hapa sasa huwa napata maumivu ya kichwa mara moja kwa siku.
Tuesday, 25 September 2018
Mimi ni Mageuzi ya Upendo.
Wednesday, 12 September 2018
Wewe Ni Nani: Tai au Ndege Mvumaji?
Badala yake, hutafuta maua yenye rangi za kupendeza ya mimea ya jangwani. Tai huishi kwa kutegemea kitu kilichokuwako zamani. Wanaishi kwa kutegemea yaliyopita. Wanajishibisha kwa kula wanyama waliokufa na wasiokuwako tena. Lakini ndege wavumaji huishi kwa kutegemea kilichoko. Wanatafuta maisha mapya. Wanajishibisha kwa vitu vipya na kwa maisha.
Tuesday, 11 September 2018
Mungu Anampenda kila mtu.
Wakristo wengi wanapenda kuchagua kuhusu ni yupi wanayemsaidia na wanayemtia moyo. Wanawatafuta watu kama wao. Baadhi ya watu hata wanaamini kwamba wanapaswa kuwasaidia watu wengine wanaoamini kile wanachoamini na kufikiria kama wanavyofikiria. Hiyo siyo njia inayopaswa kuwa. Siyo njia Yesu alivyofanya.
Miaka kadhaa iliyopita nilisoma hadithi kuhusu mtu fulani aliyeanguka kwenye shimo na hangeweza kutoka na jinsi watu wengine walivyomhudumia mtu huyo.
Mtu mbaguzi alikuja akasema, “Ninakusikitia huko chini.”
Mtu asiye mbaguzi akaja akasema, “Aha, ni jambo la kueleweka kwamba mtu angelianguka huko chini.”
Monday, 10 September 2018
Mpango wa Pili.
Tatizo lako si tatizo lako bali mtazamo wako ndio tatizo lako...chanzo cha tatizo ni mtazamo wala si tatizo!!Haijilishi umefanyiwa nini kwenye maisha yako, haijalishi umefanya nini kwenye maisha yako, Ujachelewa kuingia Mwanzo mpya, Ujachelewa kuingia mwanzo mpya tena.Lakini mustakabali wako huna nafasi kwa maisha yako ya kale. "Nimeharibu maisha yangu nami Nitakaa hapa paka Yesu aje anichukue"hapana hatuwezi kufanya hivyo.
Sunday, 9 September 2018
Je, Twahitaji Ufufuo au Mageuzi?
Wakati kitu fulani kinapofufuliwa, mambo ya zamani yanaletwa tena kuwa hai, mawazo mapya yanaletwa yanaletwa kuwa kitu. Wakati jamii inaposhuhudia maslahi mapya ya kidini, huo huitwa ufufuo. Kamusi ya MerrianWebster Collegiate inaelezea ufufuo kama “mkutano wa hisia za juu sana wa kiinjilisti au msururu wa mikutano.” Katika maisha yangu ya utu uzima kama Mkristo, nimewasikia watu wakiongea kuuhusu na kuombea ufufuo. Lakini sina hakika kwamba ufufuo ndio tunaohitaji.
Tuesday, 4 September 2018
Vaa Miwani Yako Ya Mungu
Je, Mungu anakuonaje? Anakupenda zaidi ya jinsi unavyoweza kuelewa, na ana mpango mzuri kwa maisha yako. Huko peke yako kwa sababu yuko pamoja nawe wakati wote.
Msamaha wa Mungu ni mkuu kuliko dhambi yoyote uliyotenda. Huruma zake ni mpya kila siku. Mungu amekupa wewe kama muumini, nguvu, na huna haja ya kuishi maisha ya kushindwa.
Monday, 3 September 2018
Usingoje Kesho
Jana ni historia, kesho ni siri, leo ni zawadi kutoka kwa Mungu, ndiposa tunaiita present-zawadi.” —Bil Keane
Siku moja mwandishi aliyeitwa Leo Buscaglia alisimulia hadithi kuhusu mama yake na kile alichoita “chakula cha jioni cha familia na cha mateso.” Ulikuwa usiku ule wa kwanza baada ya baba yake kurudi nyumbani na akasema kwamba inaonekana kana kwamba itabidi afilisike kwa sababu mwenzi wake kibiashara alikuwa ametoroka na pesa za kampuni. Mama yake Buscaglia alienda kuuza vito ili anunue chakula kwa ajili ya karamu ya kukata na shoka.
Sunday, 2 September 2018
MAGEUZI YA UPENDO
Wednesday, 29 August 2018
Nguvu za Kuendelea Mbele
Thursday, 9 August 2018
Je, Yesu Alikuja kwa ajiri ya Wayahudi Pekee ??
Sunday, 5 August 2018
Je, Yesu Alikufa...??
Wednesday, 1 August 2018
Amini Kilicho Bora
Nimeokoa nguvu nyingi ambayo ingetumiwa na hasira kwa kusema, “ Ingawa wanachosema au kunifanyia huniumiza, nachagua kuamini moyo wao uko sawa.” Naendelea kujiongelesha hadi hisia za hasira yangu zianze kufifia. Ninasema mambo kama, Siamini wanaelewa jinsi vitendo vyao vinavyoniathiri. Siamini wangejaribu kuniumiza kimakusudi. Hawaelewi jinsi ninavyojisikia wanaposema hivyo. Pengine hawahisi vyema kimwili leo au pengine wana tatizo la kibinafsi linalowafanya kutojali jinsi walivyo.”
Ninajua kutokana na ujuzi nilio nao kwamba kuweka kumbukumbu za kimawazo za makosa hutuathiri maisha yetu na hakumbadilishi mtu mwingine. Mara nyingi hupoteza siku tukiwa tumemkasirikia mtu fulani ambaye hata hatambui kuwa alifanya kitu kinachotuudhi.Wanafurahia siku yao na sisi twaipoteza yetu. Ikiwa tutaweka kumbukumbu hizo, basi ni kwanini hatuweki kumbukumbu za mambo mazuri watu wanayosema na kufanya kuliko makosa wanayofanya?
Ikiwa tunataka kuwapenda watu, lazima tumwache Mungu abadilishe jinsi tunavyofikiri kuhusu watu na mambo wanayofanya. Twaweza kuamini mabaya na kushuku kila kitu watu wengine wafanyacho na kusema, lakini upendo halisi kila mara unaamini kilicho bora. Kile tunachofikiria na kuamini ni chaguo. Chanzo cha dhiki yetu nyingi katika maisha ni kuwa hatudhibiti au kunidhamisha mawazo yetu. Kwa kutochagua kunidhamisha mawazo yetu, huwa moja kwa moja twachagua kuamini mabaya ya mtu au kushuku. Nabii Jeremiah aliwauliza watu haya, “Mawazo yako mabaya yatakaa ndani yako hata lini? (angalia YER 4:14). Mawazo waliyochagua kufikiria yalikuwa mabaya kwa Mungu.
Wakati tunapochagua kuamini kilicho bora, twaweza kuacha kila kitu kiondoke hasa kile ambacho chaweza kudhuru uhusiano wetu mzuri.
```Amini Kilicho Bora.```
Mtumishi













