Muhubiri 5:3 kwa maana ndoto huja kwasababu ya shughuli nyingi....kwasababu baadhi yetu tunandoto na hatutaki kufanya kazi na wakati mwingine hatuna budi kupitia hali ngumu.
Naamini unapokuwa na ndoto ni kama unapokuwa na ujauzito,kuna wanawake wachache ambao huweza kujifungua bila uchungu lakini si wengi sana.Nafikiri kwamba ukitaka kuzalisha kitu lazima ufahamu kwamba ni zaidi ya kuwa na wazo nzuri,Unakuwa na ndoto,unakuwa na matumaini,unakuwa na mpango lakini lazima uwe tayari kufanya kazi na kupitia yale ambayo unapaswa kupitia ili ndoto yako iweze timia.
Mawaidha Popote
The mission Of Mawaidha Popote is to Prepare the Nations of the world for the coming of Jesus Christ and establishment of the kingdom of God on Earth.our ultimate goal is to achieve a time in history when "the knowledge of the Lord will cover the earth as the waters cover the sea".
Wednesday, 17 April 2019
Wednesday, 20 March 2019
SAFARI YA MOYO
“Ni nani atakayenitunzia watoto wangu?” analia mama anayekufa, akijua kwamba watoto wake hivi karibuni watajiunga na mamilioni ya wengine kote duniani kumtafuta mama mpya. Nimewaona marafiki wanaougua saratani wakilia maombi hayo hayo. Siwezi kufikiria juu ya afueni kuu ya moyo, au mauguzi makuu yanayosikika nyakati za giza kuu
Nataka kumpigia yowe nimwambie. “TUTAKUTUNZIA” Hii kwa kweli ni sehemu ambayo twahitaji kujikakamua, kuvumilia, kuomba na KUAMINI, na kutoka kwa imani.
Nataka kumpigia yowe nimwambie. “TUTAKUTUNZIA” Hii kwa kweli ni sehemu ambayo twahitaji kujikakamua, kuvumilia, kuomba na KUAMINI, na kutoka kwa imani.
Monday, 17 December 2018
Mungu Anakupenda
Usifike mwishoni mwa maisha yako ukiwa umejawa na majuto ya hasara ya maisha yako kwa sababu uliyatumia kwa. vitu visivyo na maaana kamwe.......
Wakati ni karama ya ajabu kutoka kwa Mungu, na ni muhimu tuwe waangalifu sana tunatumia wakati wetu kufanya nini. Wajua, mradi tu tumeshautumia mda, hatuwezi kuupata tena. Kuwa na wakati na Mungu huleta thawabu ya ajabu, lakini vitu vingine vingi huleta sisimko lisilo na thamani kwa bei ghali.
Monday, 22 October 2018
Barua
Wapendwa wangu Mama na Baba.
Tangu Niende Chuo kikuu Najua sijachukua Muda wa kuwaandikia na Naomba msamaha kukosa kufikiria kuwaandikia paka sasa.Nitawaeleza Mambo yote katika Barua hii lakini kabla hamjasoma Tafadhali ketini chini,Tafadhali msisome paka Mketi chini.
Naendelea Vizuri sasa,Jeraha la fuvu la kichwa baada ya kuruka kwa dirisha la Bweni langu Sasa limepona,Niliruka baada ya bweni langu kushika moto muda mfupi.baada ya kuwasili hapa sasa huwa napata maumivu ya kichwa mara moja kwa siku.
Tangu Niende Chuo kikuu Najua sijachukua Muda wa kuwaandikia na Naomba msamaha kukosa kufikiria kuwaandikia paka sasa.Nitawaeleza Mambo yote katika Barua hii lakini kabla hamjasoma Tafadhali ketini chini,Tafadhali msisome paka Mketi chini.
Naendelea Vizuri sasa,Jeraha la fuvu la kichwa baada ya kuruka kwa dirisha la Bweni langu Sasa limepona,Niliruka baada ya bweni langu kushika moto muda mfupi.baada ya kuwasili hapa sasa huwa napata maumivu ya kichwa mara moja kwa siku.
Tuesday, 25 September 2018
Mimi ni Mageuzi ya Upendo.
Ninachagua huruma na kusalimisha misamaha yangu. Ninapinga maovu na kujitolea kufanya matendo ya Upendo wa Mungu. Ninakataa kutofanya lolote. Huu ndio uamuzi wangu. MIMI NI MAGEUZI YA UPENDO.- Imani yetu.
Mageuzi ni jambo la ghafla, kubwa na lililo tofauti kabisa na jinsi mambo yalivyo kama kawaida. Mageuzi huchochewa na mtu mmoja au kundi dogo sana la watu wasiokubali kuendelea kuishi kama walivyokuwa siku zilizopita. Wanaamini kuwa lazima jambo fulani lifanyiwe mabadiliko na huendelea kuimarisha mawazo yao hadi pale msingi wao unapoanzia na hilo hatimaye huleta mabadiliko kwa njia kubwa.
Wednesday, 12 September 2018
Wewe Ni Nani: Tai au Ndege Mvumaji?
Makala moja katika jarida la Reader’s Digest ilisema: Ndege mvumaji na tai hupaa juu ya majangwa ya mataifa. Kile ambacho tai wote huona ni nyama iliyooza, kwa sababu hicho ndicho wanachotafuta. Wananawiri kwa lishe hiyo. Lakini ndege wavumaji hupuuza nyama ya mizoga inayonuka.
Badala yake, hutafuta maua yenye rangi za kupendeza ya mimea ya jangwani. Tai huishi kwa kutegemea kitu kilichokuwako zamani. Wanaishi kwa kutegemea yaliyopita. Wanajishibisha kwa kula wanyama waliokufa na wasiokuwako tena. Lakini ndege wavumaji huishi kwa kutegemea kilichoko. Wanatafuta maisha mapya. Wanajishibisha kwa vitu vipya na kwa maisha.
Badala yake, hutafuta maua yenye rangi za kupendeza ya mimea ya jangwani. Tai huishi kwa kutegemea kitu kilichokuwako zamani. Wanaishi kwa kutegemea yaliyopita. Wanajishibisha kwa kula wanyama waliokufa na wasiokuwako tena. Lakini ndege wavumaji huishi kwa kutegemea kilichoko. Wanatafuta maisha mapya. Wanajishibisha kwa vitu vipya na kwa maisha.
Tuesday, 11 September 2018
Mungu Anampenda kila mtu.
Wakristo wengi wanapenda kuchagua kuhusu ni yupi wanayemsaidia na wanayemtia moyo. Wanawatafuta watu kama wao. Baadhi ya watu hata wanaamini kwamba wanapaswa kuwasaidia watu wengine wanaoamini kile wanachoamini na kufikiria kama wanavyofikiria. Hiyo siyo njia inayopaswa kuwa. Siyo njia Yesu alivyofanya.
Miaka kadhaa iliyopita nilisoma hadithi kuhusu mtu fulani aliyeanguka kwenye shimo na hangeweza kutoka na jinsi watu wengine walivyomhudumia mtu huyo.
Mtu mbaguzi alikuja akasema, “Ninakusikitia huko chini.”
Mtu asiye mbaguzi akaja akasema, “Aha, ni jambo la kueleweka kwamba mtu angelianguka huko chini.”
Monday, 10 September 2018
Mpango wa Pili.
"Penzi la kweli halikosi mkwarunzo"......utahuzunika Kwa muda gani? Utaishi kwa majuto kwa Muda gani??Mwenzangu Majuto humaliza nguvu." Laiti ninge.....Laiti nisinge.......kamaa inge...."Looh
Tatizo lako si tatizo lako bali mtazamo wako ndio tatizo lako...chanzo cha tatizo ni mtazamo wala si tatizo!!Haijilishi umefanyiwa nini kwenye maisha yako, haijalishi umefanya nini kwenye maisha yako, Ujachelewa kuingia Mwanzo mpya, Ujachelewa kuingia mwanzo mpya tena.Lakini mustakabali wako huna nafasi kwa maisha yako ya kale. "Nimeharibu maisha yangu nami Nitakaa hapa paka Yesu aje anichukue"hapana hatuwezi kufanya hivyo.
Tatizo lako si tatizo lako bali mtazamo wako ndio tatizo lako...chanzo cha tatizo ni mtazamo wala si tatizo!!Haijilishi umefanyiwa nini kwenye maisha yako, haijalishi umefanya nini kwenye maisha yako, Ujachelewa kuingia Mwanzo mpya, Ujachelewa kuingia mwanzo mpya tena.Lakini mustakabali wako huna nafasi kwa maisha yako ya kale. "Nimeharibu maisha yangu nami Nitakaa hapa paka Yesu aje anichukue"hapana hatuwezi kufanya hivyo.
Sunday, 9 September 2018
Je, Twahitaji Ufufuo au Mageuzi?
Kila mmoja anafikiria juu ya kuubadili ulimwengu, lakini hakuna anayefikiria kujibadili yeye mwenyewe. Jimmy J
Wakati kitu fulani kinapofufuliwa, mambo ya zamani yanaletwa tena kuwa hai, mawazo mapya yanaletwa yanaletwa kuwa kitu. Wakati jamii inaposhuhudia maslahi mapya ya kidini, huo huitwa ufufuo. Kamusi ya MerrianWebster Collegiate inaelezea ufufuo kama “mkutano wa hisia za juu sana wa kiinjilisti au msururu wa mikutano.” Katika maisha yangu ya utu uzima kama Mkristo, nimewasikia watu wakiongea kuuhusu na kuombea ufufuo. Lakini sina hakika kwamba ufufuo ndio tunaohitaji.
Wakati kitu fulani kinapofufuliwa, mambo ya zamani yanaletwa tena kuwa hai, mawazo mapya yanaletwa yanaletwa kuwa kitu. Wakati jamii inaposhuhudia maslahi mapya ya kidini, huo huitwa ufufuo. Kamusi ya MerrianWebster Collegiate inaelezea ufufuo kama “mkutano wa hisia za juu sana wa kiinjilisti au msururu wa mikutano.” Katika maisha yangu ya utu uzima kama Mkristo, nimewasikia watu wakiongea kuuhusu na kuombea ufufuo. Lakini sina hakika kwamba ufufuo ndio tunaohitaji.
Tuesday, 4 September 2018
Vaa Miwani Yako Ya Mungu
Natuvae kile ninachoita “Miwani ya Mungu,” ili tuangalie mambo fulani kwa mtazamo wa Mungu. Yeye anaona mambo kwa njia tofauti sana kuliko tunavyoona kwa sababu anaona mwisho kutoka mwanzo.
Je, Mungu anakuonaje? Anakupenda zaidi ya jinsi unavyoweza kuelewa, na ana mpango mzuri kwa maisha yako. Huko peke yako kwa sababu yuko pamoja nawe wakati wote.
Msamaha wa Mungu ni mkuu kuliko dhambi yoyote uliyotenda. Huruma zake ni mpya kila siku. Mungu amekupa wewe kama muumini, nguvu, na huna haja ya kuishi maisha ya kushindwa.
Umefanywa kiumbe kipya kabisa katika Kristo, umepewa maisha mapya, na unaweza kuyaacha yote yaliyopita na utazamie kwa hamu mambo yaliyo mbele yako.
Je, Mungu anakuonaje? Anakupenda zaidi ya jinsi unavyoweza kuelewa, na ana mpango mzuri kwa maisha yako. Huko peke yako kwa sababu yuko pamoja nawe wakati wote.
Msamaha wa Mungu ni mkuu kuliko dhambi yoyote uliyotenda. Huruma zake ni mpya kila siku. Mungu amekupa wewe kama muumini, nguvu, na huna haja ya kuishi maisha ya kushindwa.
Monday, 3 September 2018
Usingoje Kesho
"....tazama, wakati uliokubalika ndio sasa; tazama, siku ya wokovu ndiyo sasa.) 2 Wakorintho 6:2 “
Jana ni historia, kesho ni siri, leo ni zawadi kutoka kwa Mungu, ndiposa tunaiita present-zawadi.” —Bil Keane
Siku moja mwandishi aliyeitwa Leo Buscaglia alisimulia hadithi kuhusu mama yake na kile alichoita “chakula cha jioni cha familia na cha mateso.” Ulikuwa usiku ule wa kwanza baada ya baba yake kurudi nyumbani na akasema kwamba inaonekana kana kwamba itabidi afilisike kwa sababu mwenzi wake kibiashara alikuwa ametoroka na pesa za kampuni. Mama yake Buscaglia alienda kuuza vito ili anunue chakula kwa ajili ya karamu ya kukata na shoka.
Jana ni historia, kesho ni siri, leo ni zawadi kutoka kwa Mungu, ndiposa tunaiita present-zawadi.” —Bil Keane
Siku moja mwandishi aliyeitwa Leo Buscaglia alisimulia hadithi kuhusu mama yake na kile alichoita “chakula cha jioni cha familia na cha mateso.” Ulikuwa usiku ule wa kwanza baada ya baba yake kurudi nyumbani na akasema kwamba inaonekana kana kwamba itabidi afilisike kwa sababu mwenzi wake kibiashara alikuwa ametoroka na pesa za kampuni. Mama yake Buscaglia alienda kuuza vito ili anunue chakula kwa ajili ya karamu ya kukata na shoka.
Sunday, 2 September 2018
MAGEUZI YA UPENDO
Mageuzi. Neno lenyewe linaibua tumaini, linawasha hamu na kuvutia uaminifu kama neno ambalo halijawahi kupatikana kwenye msamiati wa binadamu. Katika historia, wazo la maguezi limemimina mafuta kwenye moto na kusisimua ujasiri kwa waliovunjika moyo.
Mageuzi yamewakusanya pamoja wale wanaotafuta sababu kubwa kuliko wao wenyewe na yamewapa wanawake na wanaume waliokosa mwelekeo hapo awali, sababu ya kujitoa mhanga.
Wamewazaa viongozi mashuhuri na kuwalea wafuasi mashuhuri, wameubadili kabisa ulimwengu. Mageuzi ni jambo la ghafla, kubwa na lililo tofauti kabisa na jinsi mambo yalivyo kama kawaida. Wednesday, 29 August 2018
Nguvu za Kuendelea Mbele
Nakumbuka siku moja nilipokea habari mbaya sana muda mfupi kabla kuaanza kongamano la siku tatu. Ilikuwa vigumu kuendelea, lakini nilijua sina budi kuendelea. Nilihisi Roho Mtakatifu akisema, “Nyanyua mguu wako na upige hatua kwenda mbele. Endelea kwenda Mbele!”
Kuendelea kwenda mbele hakukuondoa uchungu wote na hali ya kuvunjika moyo niliyohisi, lakini kulinizuia nisiweze kuzama katika kilindi cha kukata tamaa, na baada ya majuma machache, hali iliweza kutatuliwa. Moja ya dalili za ukomavu wa kiroho ni kuwa na nidhamu ya kutimiza ahadi zako, hata ikiwa unapitia wakati mgumu. Nilikuwa naumia, lakini nilihitaji kuendelea kuwahudumia wengine waliokuwa wanaumia, na nilifanya hivyo, Mungu aliniponya na kusuluhisha tatizo langu.
Thursday, 9 August 2018
Je, Yesu Alikuja kwa ajiri ya Wayahudi Pekee ??
Ndugu zetu Waislamu wanapenda sana kudai kuwa Yesu alikuja kwa ajili ya Wayahudi peke yao na sio kwa ajili ya ulimwengu wote. Na andiko wanalolitumia tena na tena ni la Mathayo 15:24 pale Yesu alipozungumza na mwanamke Mkananayo: Akajibu, akasema, Sikutumwa ila kwa kondoo waliopotea wa nyumba ya Israeli.
Na tazama, mwanamke Mkananayo wa mipaka ile akatokea, akampazia sauti akisema, Unirehemu, Bwana, Mwana wa Daudi; binti yangu amepagawa sana na pepo. Wala yeye hakumjibu neno. Nao wanafunzi wake wakamwendea, wakamwomba, wakisema, Mwache aende zake; kwa maana anapiga kelele nyuma yetu. Akajibu, akasema, Sikutumwa ila kwa kondoo waliopotea
Sunday, 5 August 2018
Je, Yesu Alikufa...??
Na KWA AJILI YA KUSEMA KWAO MV BUKOBA Ilizama; na kwa hakika MV BUKOBA haikuzama Bali ulizama tu mtumbwi uliofanana na MV BUKOBA na wale wanaosema ilizama wamo katika shaka na jambo hilo la kusema MV BUKOBA alizama mwaka 1996; hawana uhakika isipokuwa wanafuata Dhaka tu. Na wala Meli hii haikuzama Bali mtumbwi unaofanana na MV BUKOBA ndio uliozama. Na kwa yakini MV BUKOBA haikuzama”-Maalim Chaka
Qurani 4:157-158 Suratul An-Nisaa (Wanawake) Na kwa (ajili ya )kusema kwao sisi tumemuua masihi Isa mwana wa Maryamu, mtume wa Mungu. Hali hawakumuua wala hawakumsulubu bali walibabaishiwa (mtu mwingine wakamdhani nabii Isa.) Na kwa hakika wale waliokhitalifiana katika (hakika)hiyo (ya kumuua nabii Isa) wamo katika shaka nalo (jambo hilo kusema kauwawa]. Wao (kabisa) hawana yakini juu ya (jambo)hili (la kuwa kweli wamemuua nabii isa) isipokuwa wanafuata dhana tu.Na kwa yakini hawakumuua. Bali mwenyenzi Mungu alimnyanyua kwake. Na mwenyenzi Mungu ni mwenye nguvu (na)mwenye hikima.
Subscribe to:
Posts (Atom)