Sunday, 17 June 2018

UAMUZI MUHIMU ZAIDI UTAWAHI KUFANYA

Ningependa kuzungumza nawe kuhusu uamuzi muhimu zaidi. Kusema kweli, huu ndio uamuzi muhimu kabisa ambao utawahi kukabiliana nao. Uamuzi huu ni muhimu zaidi kuliko chaguo la shule utakayoenda, chaguo la kazi, ni nani utakayeoa, au ni wapi utakapoishi. 

Uamuzi huu unahusu mahali utakapokuwa milele.  Hebu lifi kirie jambo hili.  Milele ni muda mrefu, mrefu sana. Watu wengi wanajishughulisha tu na mambo ya leo, au ya miezi michache. 
Wengi wanashughulikia swala la watakapostaafu.Ningependa kuzungumza zaidi ya hayo.  Ningependa kuzungumza kuhusu “maisha baada ya kufa.” Je unashughulikia swala hilo? Je, wajua kwamba wewe sio nyama na mifupa tu, damu na misuli?  Wewe ni roho, una nafsi na unaishi katika mwili. Utakapokufa, ambalo ni jambo litamkumba kila mmoja wetu, mwili wako utalazwa kaburini.  Utaharibika na kuwa majivu na mavumbi.  Lakini je ni vipi kuhusu “yule wewe wa kweli” – wewe uliye ndani, utu wako, akili, hiari na hisia? Sehemu yako ya kiroho ni sehemu ile ya utu wako ambayo haionekani kwa macho ya miili yetu.  Sehemu yako hii ndiyo itakayoishi milele.

Thursday, 14 June 2018

Amini kilicho Bora

Ikiwa  tunataka  kuwapenda watu, lazima  tumwache  Mungu abadilishe jinsi tunavyofikiri kuhusu watu  na  mambo  wanayofanya. Twaweza  kuamini  mabaya na kushuku  kila kitu watu wengine wafanyacho  na kusema, lakini  upendo  halisi  kila mara unaamini kilicho bora.Kile  tunachofikiria  na kuamini  ni  chaguo. Chanzo cha dhiki yetu nyingi katika maisha ni kuwa hatudhibiti au kunidhamisha mawazo  yetu.  Kwa  kutochagua  kunidhamisha  mawazo  yetu, huwa moja kwa moja twachagua kuamini mabaya ya mtu au kushuku.

Nabii Jeremiah aliwauliza watu haya, “ *Mawazo yako mabaya yatakaa ndani  yako hata lini?  (angalia YER  4:14).* Mawazo  waliyochagua kufikiria yalikuwa mabaya kwa Mungu. Wakati tunapochagua kuamini  kilicho bora,  twaweza  kuacha kila kitu  kiondoke  hasa  kile  ambacho  chaweza kudhuru  uhusiano wetu mzuri. Nimeokoa  nguvu nyingi  ambayo ingetumiwa na hasira kwa  kusema, “Ingawa  wanachosema  au kufanya huniumiza, nachagua  kuamini  moyo wao  uko sawa.”

Thursday, 7 June 2018

Jifunze Kusikiliza

Rafiki yangu  mmoja  alikuwa  akiongea  nami kuhusu mwanaume mmoja  kijana  katika  kanisa  lake ambaye alikuwa  na meno yaliyokaa  vibaya.  Yalikuwa  yamekaa  vibaya  hivi kwamba alikataa  kutabasamu  kwa  sababu alifedheheka wakati  mtu yeyote alipoyaona.  Kiukweli Nilimhurumia wakati niliposikia  hadithi yake na sikuweza cha kufanya.

Ni mara  ngapi  tunaposikia  kuhusu kitu kama hicho, tunaposikia huruma  na kisha tukaondoka  bila hata  kufikiria iwapo  au  la  twaweza  kufanya  kitu cha  kusaidia?  Nafikiri si mara nyingi. Twahitaji  kuelimishwa  na kufunzwa mara  kwa  mara. Twahitaji  kubuni tabia  mpya.  Badala  ya  kudhani kuwa  hakuna kitu tunachoweza  kufanya,  twapaswa  kufikiri  kuhusu  hali hiyo. Kumbuka, Waraka  wa  kwanza  wa  Yohana  3:17 inasema: “Lakini mtu akiwa  na riziki ya  dunia, kisha akamwona  ndugu yake ni mhitaji, akamzuilia  huruma zake, je! Upendo  wa  Mungu  wakaaje Ndani yake huyo?.

Tuesday, 5 June 2018

Mungu, Huu sio wakati Mnzuri

Biblia  inaelezea  hadithi kuhusu mwanaume  mmoja  ambaye hakumfuata  Mungu  kwa  sababu kufanya hivyo lilikuwa  ni  jambo la usumbufu  kwake. Mwanaume huyu  aitwaye Feliki,  alimtaka  Paulo aje  na  amhubirie injili.  Lakini wakati Paulo  alipoanza  kuzungumza naye kuhusu  maisha  yaliyonyooka,  usafi wa  maisha,  na  kudhibiti hamu alizo nazo, Feliki alishangaa  na kuogopa.  Alimwambia Paulo aende  zake  na kwamba  atamwita  wakati ufaao zaidi (angalia      MDO  24:25). “Na Paulo alipokuwa akitoa  hoja zake  katika habari ya  haki,  na  kuwa  na  kiasi na  hukumu itakayokuja,  Feliki  akawa na  hofu akajibu,  Sasa  enenda  zako,  nami nikipata  nafasi  nitakuita.” 

Ninashangazwa  mno na  jambo  hili, sio kwa  sababu linafurahisha, bali kwa  sababu laonyesha  wazi  jinsi  tulivyo. Hatujali kusikia kuhusu jinsi Mungu alivyo  na  upendo mwingi kwetu na  kuhusu mipango mizuri  aliyo nayo katika  maisha  yetu,  lakini wakati anapoanza  kutulaumu   kwa  makosa  tunayofanya au kuturekebisha.
kwa  njia yoyote,  tunajaribu kumwambia  kwamba  “sasa”  sio wakati mzuri. Nina shaka  kuwa  Yeye huchagua  wakati tunaodhani,  “ni mzuri,”  na nafikiri hufanya hivyo kwa kusudi lake! Wakati wana  wa  Israeli walipokuwa  wakisafiri kupitia jangwani,  waliongozwa  na  Mungu ndani ya  wingu mfano wa nguzo wakati wa  mchana  na ndani  ya moto  mfano wa  nguzo wakati wa  usiku. Wakati wingu lilipoenda,  pia nao walienda  na wakati liliposimama, walikaa  mahali  walipofika.  Jambo  la kufurahisha  ni kwamba  hakukuwa na mtindo au mpango  waliofahamu  kuhusu  ni wakati gani wingu hilo litaenda. Walilazimika kuondoka wakati wingu linaenda (angalia  HES 9:15-23). 

Monday, 4 June 2018

Kukaa Bila kufanya kitu humwalika Adui


Kulala kwenye kochi au kuegemea kwenye kiti maalum kumuuliza Mungu  alinde  kila kitu kinachohitaji  kufanywa  ni  rahisi, lakini inatuwacha  tusiwe na  la  kufanya  na  kutozaa  matunda na  kutuweka wazi  kushambuliwa na muovu. Ikiwa  akili zetu hazina  mawazo mazuri, shetani anaweza kuzijaza  mambo mabaya kwa  urahisi. Ikiwa  tu walegevu na  hatufanyi lolote,  anaweza  kutujaribu kufanya  makosa  na  hata  mambo  machafu.  Biblia inatuambia  kila mara tuisome kujikumbusha  na itatuepusha kuwa  walegevu na watu wa  kutozaa  matunda.  Tukifikiria  kwa  bidii  kile  tunachoweza kuwafanyia  watu wengine hakutakuwa  na  nafasi katika  akili zetu ya kuwa na mawazo mabaya.

Watu  wasiokuwa  na  lakufanya  huvunjika moyo  kwa  urahisi, hulemewa  kimawazo,  na  kujisikitikia wenyewe.  Wanaweza kuanguka  katika  aina  zote  za  dhambi. Mtume Paulo  hata alisema ikiwa mwanamke aliye  bado kijana amekuwa mjane, anapaswa  kuolewa  tena. Lau  sivyo huenda asiwe na lakufanya na  kuanza  masengenyo  na  kuwa  mdakuzi  wa  mambo  (angalia Timotheo  1 5:11-15).  Paulo aliendelea  kusema kwamba  baadhi  ya wajane  ambao  bado  wangali vijana  kwa  kutokuwa  na lakufanya tayari walikuwa wameanza kumgeukia shetani. Ina umuhimu gani kuendelea kuwa  imara?  Ninaamini maandiko  ya  Paulo yanathibitisha  kwamba  ni muhimu.

Kwanini Mwili ni Mlegevu...?


Mtume Paulo  anafundisha  wazi  kwamba  mwili ni mlegevu, wenye tamaa,  na  matamanio  mengi ya  dhambi (angalia  RUM 13:14). Namshukuru  Mungu  kwa vile  tuko zaidi ya mwili.  Pia tuko na roho na sehemu  ya roho ya Mkristo ni  pale ambapo  maumbile ya  Mungu hukaa.  Mungu ni mwema na kwa  kuwa  Anakaa ndani  yetu inamaanisha  tuna wema ndani  yetu.

Kwa  roho zetu twaweza  kuunidhamisha  na kuutawala  mwili, lakini haihitaji juhudi.  Inahitaji ushirikiano na Roho Mtakatifu  Anayetupa nguvu sisi na kutuwezesha  kufanya  mambo mazuri. Paulo anasema hatuhitaji  kuuwekea  mahitaji  mwili na  ninaamini njia  moja  ambayo tumeuwekea mwili mahitaji ni kukaa bila kufanya kitu! Kukaa  bila kufanya chochote  ni  mazoea  mabaya. 
Kadiri tunavyokaa  bila kufanya  lolote,  ndivyo  tunavyotaka  kutofanya lolote. Nina hakika umewahi kukaa nyumbani siku  nzima na kupata  kuwa  kadiri unavyolala  hapo  kitandanii, ndivyo unavyohisi ugumu  kuinuka.  Unapoinuka kwanza,  kila kitu huwa kigumu  na kuhisi  uchovu, lakini unapoendelea  kujilazimisha kuondoka,  nguvu inakurudia. Leo niliamka nikiwa sina furaha.  Nilifanya  kazi juma zima kufanya  mkutano  na  bado  nahisi uchovu kiasi.

Hakuna Kizuri Kitendekacho Kiajali


Ndipo Bwana akaniambia, Umeona vema, kwa maana ninaliangalia neno langu, ili nilitimize. Jeremiah 1:12
Hakuna mageuzi yaliyoubadilisha ulimwengu yaliyotendeka kiajali. Katika baadhi ya mageuzi, yalianza  na watu wachache  tu waliojadili kuhusu mabadiliko  yanayohitajiwa.  Iwapo  matukio haya ya kihistoria  yalizaliwa na ghasia  za  kawaida au yalipangwa, hayakufanyika tu. Yalifanywa maksudi,  kwa kunuiwa, kupendwa na kwa  mkakati maalum. Yalianza  hivi  kwamba  mtu fulani  alikataa kufanya  kitu, mtu fulani  “akaachilia  mambo yafanyike,”  mtu fulani alikataa  kusikiza na akapuuza ilhali  maovu  yalikuwa yamezidi. Mageuzi hutokea kwa sababu mtu fulani huamua kuchukua hatua. 

Biblia imejaa maagizo yanayotuhitaji sisi  kuyatekeleza.  Agizo la kutekeleza  badala  ya  kusikiza ni rahisi, lakini mamilioni  ya  watu hupuuza. Pengine wanafikiri  mambo yatakuwa bora wakijitegemea. Hayawezi. Hakuna kizuri  kitendekacho kiajali. Wakati fulani nilijifunza kwamba maisha yangu yamebadilika na kuwa bora. Kutamani kitu hakutoi matokeo tunayotarajia, bali lazima tuwe wakakamavu kufanya kile  kinachohitajiwa  kufanywa  ili  kuyapata tuyatakayo. Hatutampata  mtu aliyefaulu  ambaye katika  maisha  yake alitarajia  kufaulu na hatimaye akafaulu. Vile  vile, hatutampata  mtu asiyefanya jambo lolote na kisha  akafaulu maishani. Mfano huu pia  unahusu kuwa  sehemu ya  Mageuzi  ya  Upendo. 

Wajibu wa mkristo kwa muislam.

Baadhi ya Wakristo wanaona kwamba Huduma ya Injili kwa muislam ni jambo la ziada tu lakini si lalazima lakini Huduma ya Mkristo yeyote Yule ni kumfanya Yesu Kristo kujulikana kwa wao wasio mjua,wawe wanaishi mbali au karibu kwake. Kuhama kwa watu toka nchi za Kiislamu hadi nchi zenye Wakristo wengi imefungua fursa mpya kwa huduma ya Kikristo katika maisha yetu ya kila siku. 

Kama mwaamini na kushiriki Injili, utapata uwepo unao endelea wa Bwana Yesu Kristo: Kwa sababu hii, enendeni ulimwenguni mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi, mkiwabatiza kwa Jina la Baba na la Mwana na la Roho Mtakatifu, nanyi wafundisheni kuyashika mambo yote niliyowaamuru ninyi. Hakika Mimi niko pamoja nanyi sikuzote, hadi mwisho wa nyakati Kuhusu Kristo na cha kuzingatia ni hapa sasa, huduma ya Kikristo kushikilia katika tarajio ni Muhimu sana kwa maisha yote, matarajio, na utu wa upeo wa Kiislam.Walakini, watu wengi hawajui jinsi ya kushiriki Injili kwa Waislam au wameogopa kufanya hivyo. Kwa ukurasa huu kuna baadhi ya miongozo jinsi ya kushiriki nao.

KUPATA UPONYAJI  KUTOKA KWA PIGO AU MSIBA

 
“Roho wa Bwana yu juu yangu,  kwani amenipaka mafuta niwahubirie maskini  Habari  Njema.  Amenituma niwatangazie mateka watapata uhuru,  vipofu watapata kuona tena; amenituma niwakomboe wanaoonewa. Luka 4:18 

Haijalishi kilichotokea katika maisha  yako kusababisha huzuni na upweke, unaweza kuwa na uhakika kwamba Mungu atakuongoza  katika  kupokea uponyaji wako. Naye atakuonyesha wakati ambapo utakuwa  unakubalia hisia zako kwenda mrama au kupoteza usawa wako - iwapo utakubali kumsikiza Roho wake. Haiwezekani kwetu kukadiria kiasi cha wakati ambao unafaa kutumika katika kuomboleza kwa sababu hali na watu ni tofauti. Lakini, hata kama itachukua muda mrefu kiasi gani, kutakuwa na wakati ambapo Bwana atasema,  “Sasa ni wakati  wako  wa kuamka na uendelee mbele. Ni lazima  uachane na hayo ya kale nawe  umalize mbio  ambayo  nimekuwekea katika  maisha  yako. 

Je Quran Imetoka wapi?

Niseme mapema kwamba nimechoka na kelele ambazo waislam wamekuwa wakitupigia masikioni mwetu na kututaka kutuaminisha kuwa Quran ni kitabu cha Mwenyenzi Mungu,jambo ambalo siwezi kulikubali bila kulifanyia utafiti,maana waislam wamekuwa wakiongea kama waimba taarabu, yaani kuongea bila kuleta udhibitisho wa kile wanachokisema jambo ambalo mkristo yeyote makini hawezi kukubali jambo bila kupata udhibitisho hakinifu.

Lakini jambo moja la kushangaza waislam wenyewe wamekuwa wakwanza kutojua hata kitabu chao wanachokiamini, kama woote tunavyofahamu kuwa dunia ziko dini nyingi sana na zote zina vitabu vyake vitakatifu vinavyodaiwa kuwa ni Neno la Mungu na kuwa ndio mamlaka ya Mwisho ya Dini hizo wahindu wanakitabu chao kiitwacho

Kwanini Yesu aitwe Mungu?

                         Kupitia Qur’an Na Biblia.

Kelele nyingi zimesikika miongoni mwetu, Waislam wakijaribu kutuaminisha juu ya kile wanachoamini, Wanaendelea kushikilia mitazamo yao kuhusu Uungu wa Yesu,Chanzo cha maswali yote wanayouliza juu ya Bwana Yesu kinaanzia mara tu Yesu alipovaa mwili wa kibinadamu tendo hilo kwa fikra za haraka tu linaweza kudhaniwa kuwa ndilo linaloshusha mamlaka yake ya asili kama Mungu. Pamoja na hayo mimi binafsi nichoelewa ni kuwa tendo hilo kamwe halishushi mamlaka bali linafunika mamlaka aliyokuwa nayo kwa kadri ya sababu Ifuatayo:-

Mungu aliwahi kujifunua wazi katika nyakati za nyuma na wanadamu wakaangamia
Fuatilia:- kutoka 19:20-21 Bwana akaushukia mlima, juu ya kilele cha mlima; Bwana akamwita Musa aende hata kilele cha mlima; Musa akapanda juu. Ndipo Bwana akamwambia Musa, Shuka chini, uwaonye watu wasije wakapasua njia waje kwa Bwana kutazama, kisha wengi miongoni mwao wakaangamia.

Sunday, 3 June 2018

SUBIRA,TAFADHALI!!

Biblia inasema katika  Waebrania  6:12 kwamba tunarithi ahadi zake kwa imani  na uvumilivu.  Kupokea urithi hakuhitaji bidii yoyote kutoka kwetu. Tunahitaji kungoja  tu, mpaka wakati ulioteuliwa.

Kwa  mfano  unaweza  kuamini, au  kuwa na  imani  kwamba jamaa yako fulani amekuwosia urithi fulani, lakini ni lazima uwe na uvumilivu  na  kusubiri  wakati  ufaao  kufika  ili  upokee  urithi  ule. Imani na subira ni hushirikiana katika  kutimiza jambo lolote. Zinafanya kazi pamoja kutimiza lengo linalotarajiwa. Yakobo 1:2,  3  (Tafsiri  ya  AMP)  inasema  kuwa yafaa tufurahi “tunapoangukia majaribu ya kila aina”, tukijua kwamba “kuthibitishwa kwa imani yetu” huleta saburi. Na saburi ikishafanya kazi yake kikamilifu, tutakuwa watu ambao “wamekomaa kikamilifu … wasiopungukiwa  na neno.”
Jamani! Andiko la ajabu hili!

WAKATI UFAAO KUAMINI

“Nilikuamini, na kukutegemea, na kuwa na uhakika ndani  Yako, Ee Bwana. Nilisema, Wewe ndiwe Mungu wangu. “Nyakati  zangu zimo mikononi mwako; nikomboe kutoka kwa mikono ya adui zangu na wale wanaonifuatia na kuniletea dhiki.” Zaburi 31: 14,15 AMP Katika sura  hii, mwandishi  wa Zaburi ansema kwamba alimtumainia Mungu kumkomboa, na alimtegemea kufanya hivyo kwa wakati uliofaa. Kumtumainia Mungu kunahitaji tuseme, “Nyakati zangu  zimo mikononi Mwako.”

Nimejifunza kwamba tegemeo linatuhitaji kukubali  kwamba kuna maswali mengine ambayo yatabaki  yakiwa  hayana majibu na  hivyo  basi kuweka nyakati zetu mikononi  mwake  Mungu  – tukiamini kwamba japo hatuyajui majibu yote,  Yeye ayajua. Anao wakati  unaofaa kikamilifu kwa kila jambo maishani mwetu.

MSIMU MWAFAKA

Mambo  Ya  Walawi  26:4  inasema,  “Nitazinyezesha mvua  zenu kwa nyakati zake.” Wagalatia 6:9 kwa tafsiri ya  AMP  inasema ni lazima  “…tusife moyo  na kuwa wachovu  na kuzimia katika kutenda kiungwana  na kutenda yaliyo ya haki, maana kwa wakati wake na kwa msimu ulioteuliwa tutavuna,  kama tusipouachilia na kupunguza ujasiri wetu na hapo kuzimia.”

Friday, 1 June 2018

VIWANGO SABA VYA KUOMBOLEZA

Mtumaini Mungu kwa moyo wako wote, wala usitegemee akili  zako mwenyewe.Umtambue Mungu katika  kila ufanyalo, naye atazinyosha njia zako. Mithali 3:5-6 Baada  ya mtu kupatwa na msiba au pigo fulani, karibu kila mmoja  wetu hupitia hali ya kuomboleza. Kwa kawaida, kuna viwango saba katika  kuomboleza. Hebu  tuvichunguze  viwango hivi kwa makini na tujaribu kupata ufahamu ni nini kinachokuwa kikitendeka katika nafsi zetu na kile tunachoweza kufanya ili kupitia kiwangi hicho kitufaidi kikamilifu.

Kiwango Cha 1: Kushtuka na Kukataa Mara nyingi, mambo haya mawili huwa ndiyo ya mwanzo kutokea tunapopatwa  na pigo au msiba. Mungu huyatumia kutulinda  ili tusivunjike kabisa. Kushituka:   Mshituko ni hali ambayo inagutusha nia na hisia zetu kwa pigo kubwa mno ambalo halikutarajiwa. Kuweza kushtuka ni hali tunayozaliwa nayo ndani yetu.  Hutupatia muda wa kuweza  kukubaliana  na mabadiliko yaliyotukia. Hutuzuia kukumbana na ukweli mara moja.