Ningependa kuzungumza nawe kuhusu uamuzi muhimu zaidi. Kusema kweli, huu ndio uamuzi muhimu kabisa ambao utawahi kukabiliana nao. Uamuzi huu ni muhimu zaidi kuliko chaguo la shule utakayoenda, chaguo la kazi, ni nani utakayeoa, au ni wapi utakapoishi.
Uamuzi huu unahusu mahali utakapokuwa milele. Hebu lifi kirie jambo hili. Milele ni muda mrefu, mrefu sana. Watu wengi wanajishughulisha tu na mambo ya leo, au ya miezi michache.
Wengi wanashughulikia swala la watakapostaafu.Ningependa kuzungumza zaidi ya hayo. Ningependa kuzungumza kuhusu “maisha baada ya kufa.” Je unashughulikia swala hilo? Je, wajua kwamba wewe sio nyama na mifupa tu, damu na misuli? Wewe ni roho, una nafsi na unaishi katika mwili. Utakapokufa, ambalo ni jambo litamkumba kila mmoja wetu, mwili wako utalazwa kaburini. Utaharibika na kuwa majivu na mavumbi. Lakini je ni vipi kuhusu “yule wewe wa kweli” – wewe uliye ndani, utu wako, akili, hiari na hisia? Sehemu yako ya kiroho ni sehemu ile ya utu wako ambayo haionekani kwa macho ya miili yetu. Sehemu yako hii ndiyo itakayoishi milele.













