Sunday, 3 June 2018

WAKATI UFAAO KUAMINI

“Nilikuamini, na kukutegemea, na kuwa na uhakika ndani  Yako, Ee Bwana. Nilisema, Wewe ndiwe Mungu wangu. “Nyakati  zangu zimo mikononi mwako; nikomboe kutoka kwa mikono ya adui zangu na wale wanaonifuatia na kuniletea dhiki.” Zaburi 31: 14,15 AMP Katika sura  hii, mwandishi  wa Zaburi ansema kwamba alimtumainia Mungu kumkomboa, na alimtegemea kufanya hivyo kwa wakati uliofaa. Kumtumainia Mungu kunahitaji tuseme, “Nyakati zangu  zimo mikononi Mwako.”

Nimejifunza kwamba tegemeo linatuhitaji kukubali  kwamba kuna maswali mengine ambayo yatabaki  yakiwa  hayana majibu na  hivyo  basi kuweka nyakati zetu mikononi  mwake  Mungu  – tukiamini kwamba japo hatuyajui majibu yote,  Yeye ayajua. Anao wakati  unaofaa kikamilifu kwa kila jambo maishani mwetu.

Sote huwa tunatamani na kuamini kwamba mambo mazuri yatendeke maishani mwetu, SASA – si baadaye! Tunavyoendelea kukomaa katika maisha yetu ya Kikristo, tunajifunza kuaminia vitu sio  SASA,  lakini  katika  wakati  mwafaka wa Mungu. Waiberania 11:1 inasema, “Basi imani ni kuwa na hakika ya mambo yatarajiwayo, ni bayana ya mambo  yasiyoonekana. Wakati wowote tunaweza kuwa na imani  ‘sasa’,  lakini sio  kila wakati tutaweza kuona udhihirisho wa yale tunayoyaaminia  sasa. Kumtumainia Mungu mara nyingi  kunahitaji  kutofahamu  jinsi Mungu atakavyo timiza yale yanayohitaji kutimizwa na pia kutofahamu ni  lini  atakavyofanya hivyo. 

Sisi  husema,  “Mungu hachelewi,” lakini mara nyingi yeye haji mapema  pia. Kwa nini? Kwa maana Yeye hutumia nyakati hizo kuimudu imani  yetu ndani yake, na kutufanya tukakua wakati wa kungoja. Mojawapo wa wale watumishi wa huduma ya kifedha kila mwezi hivi maajuzi alijipata na haja ya kifedha ili aweze kulipa kodi  zilizotokea  ghafla,  hakuzitarajia. Kodi  zenyewe  ilipasa zilipwe kufikia taerehe 15  Aprili. Mume na mke huyo walitoa sadaka maalum kwa huduma ya Ujenzi kanisani kwetu wakiamini Mungu awape muujiza waliohitaji. Tarehe 14  Aprili walipata pesa  za kulipa kodi ile. Mbona muujiza haukuwafikia tarehe  1  au  5  Aprili?  Ni  kwa  nini  mara  nyingine Mungu hungoja mpaka siku au dakika ya mwisho kabisa? Sababu ni kwamba yeye anatufundisha masomo  kuhusu kumtumainia na kumtegemea.


Kutumainia hakupokelewi kama urithi, huja  kwa kujifunza. Tunajifunza kumtumainia Mungu kwa kupitia mabo yanayohitaji kumtegemea.Tunapouona uaminifu Wake mara moja hadi nyingine,  tunawacha kujitegemea na taratibu tunaingia kwenye pumziko la Mungu na kuweka imani yetu  ndani Yake.

Tukiitazama hivi, ni rahisi kuona ni vipi wakati  mwafaka unavyotimiza jukumu muhimu  katika kujifunza kumtumainia Mungu. Kama Mungu angefanya kila kitu tunachomuomba mara  moja, hatungeweza kukua na kukomaa. Wakati unaofaa na kutumainia ni mapacha. Wanafanya kazi bega kwa bega.
GetYourHopesUp

No comments:

Post a Comment