Friday, 1 June 2018

VIWANGO SABA VYA KUOMBOLEZA

Mtumaini Mungu kwa moyo wako wote, wala usitegemee akili  zako mwenyewe.Umtambue Mungu katika  kila ufanyalo, naye atazinyosha njia zako. Mithali 3:5-6 Baada  ya mtu kupatwa na msiba au pigo fulani, karibu kila mmoja  wetu hupitia hali ya kuomboleza. Kwa kawaida, kuna viwango saba katika  kuomboleza. Hebu  tuvichunguze  viwango hivi kwa makini na tujaribu kupata ufahamu ni nini kinachokuwa kikitendeka katika nafsi zetu na kile tunachoweza kufanya ili kupitia kiwangi hicho kitufaidi kikamilifu.

Kiwango Cha 1: Kushtuka na Kukataa Mara nyingi, mambo haya mawili huwa ndiyo ya mwanzo kutokea tunapopatwa  na pigo au msiba. Mungu huyatumia kutulinda  ili tusivunjike kabisa. Kushituka:   Mshituko ni hali ambayo inagutusha nia na hisia zetu kwa pigo kubwa mno ambalo halikutarajiwa. Kuweza kushtuka ni hali tunayozaliwa nayo ndani yetu.  Hutupatia muda wa kuweza  kukubaliana  na mabadiliko yaliyotukia. Hutuzuia kukumbana na ukweli mara moja.



Kabla  yetu kusonga mbele, ni lazima tuwe tumepata nia mpya. Kushituka hutupatia muda wa  kujenga upya nia zetu kuhusu maisha yetu ya sasa na ya baadaye. Kwa mfano.
Fikiria  Shock Absorbers*  za motokaa.Zimetengenezwa ili  kuituliza gari wakati inapopitia barabara yenye mashimo.  Bila yake, basi gari linaweza kuvunjika vipande  kutokana na mapigo inayopata inapoenda huku na kule. Mara  nyingi, sisi  huwa  hivi  pia.  Tunasafiri  katika  barabara  ya maisha,  na wengi wetu hawatarajii mashimo  na barabara mbovu. Hivyo tunakuwa hatujajitayarisha wakati mashimo  yanapotokea. Shock absorbers  zetu  ambazo zimewekwa na Roho Mtakatifu hutuliza  pigo  lile hadi tunapokuwa  na uwezo wa kubadilisha nia na mawazo yetu  kuweza kukubali  na kukabili  mabadiliko ya ghafla yaliyoingia katika maisha yetu. Kipindi cha mshutuko kinaweza kudumu kutoka dakika chache hadi wiki kadhaa. Lakini kikipita muda huo, basi kuna shida fulani. Mshutuko ni kama dawa za kuzuia uchungu wakati wa kufanyiwa upasuaji. Lakini hatuwezi kuendelea kuzitumia dawa hizo daima. Ni lazima tuendelee na maisha. Kushituka  ni kuepuka  ukweli kwa muda, lakini  iwapo si kwa  muda mfupi, basi huenda kukaleta madhara mengi zaidi. Ninakumbuka nilikuwa na shangazi yangu wakati mjomba alipoaga dunia.

Alikuwa ameugua kwa muda, na ingawa ilikuwa wazi kwamba  hangeishi sana, shangazi yangu  aliendelea kusema tena na tena, “Siwezi kuamini. Siwezi kuamini ameenda.” Alikuwa katika kiwango cha kwanza cha kushtuka ambacho kwa kawaida huja baada ya msiba. Wakati ambapo unapopitia kipindi cha kushituka, ni vyema usikae bila ya kufanya chochote  kwa muda  mrefu sana.

Wakati  unapopitia kushituka  kwa sababu  ya msiba fulani, wewe kama mkristo, unahitaji kutofautisha kati ya nafsi  yako, na roho yako.  Hata  wakati  wa msiba, unahitaji kupambanua  tofauti  kati  ya hisia zako na mwongozo wa kweli wa Roho Mtakatifu.

Kukana:   Kukana ni kuukataa ukweli wa mambo  na kunaweza kutuletea magonjwa ya hisia na nia katika vipimo mbali mbali. Mungu ametupatia Roho wake ili tuweze kuupokea ukweli kwa ujasiri, tumshike mkono, na kutembea kati kati ya mabonde yote ya giza na kushinda vizuizi vyote tunavyopitia maishani. Huku tukiwa na Roho wa Mungu ndani yetu kutulinda, tunaweza kusema pamoja na mfalme Daudi, “Ndio, hata nijapopita kwenye bonde  la  uvuli  wa  mauti, sitaogopa  lolote.  Maana  wewe  Mwenyezi Mungu  u  pamoja  nami.  Gongo lako  na  fimbo  yako  vyanilinda.

Hata wakati mauti yanapoleta uvuli wake juu yetu, tunaweza kuishi na tumaini.Tunapozungumza  juu  ya  tumaini,  fikiria  tena  kuhusu  Shedraki,
Meshaki na  Abednego katika  tanuru ya moto. (Danieli 3:8-27). Hata ingawa walitupwa ndani  ya  tanuru  iliyotiwa moto  mara  saba zaidi, Bwana alikuwa pamoja nao katika moto huo.

Tunaweza  kusoma hadithi za Biblia kama  hii ambayo tumetaja hapo juu wakati tunapojikuta katika hali ngumu. Kama vile Mungu alivyokuwa  pamoja na watoto wale wayahudi katika  tanuru ya moto, hata wakatoka wakiwa wazima bila ya kuumizwa, hivyo ndivyo  atakavyokuwa nasi  katika kila hali tutakayopitia maishani. Ni  mapenzi yake  Mungu  kwetu sisi  kuukubali ukweli wa  mambo, tuyapitie  na tupate kushinda katika kila njia. Kukumbana na ukweli kunaweza kuwa kugumu,  lakini kuukimbia huleta hali ngumu zaidi.

Kiwango Cha 2: Hasira Kiwango cha pili huashiriwa na hasira: hasira dhidi ya Mungu, dhidi ya shetani, dhidi  yetu wenyewe, na hasira dhidi  ya mtu aliyesababisha uchungu au msiba ule, hata kama mtu huyo, katika kuisababisha hali hiyo alikufa. Hasira dhidi ya Mungu: Kila mtu huamini kuwa Mungu ni mwema,  na kwamba anatawala maisha  yetu. Hivyo, wakati msiba  au pigo fulani linapotokea katika  maisha yetu,  hatuelewi ni kwa nini Mungu hakuzuia mambo mabaya kama hayo yasitokee na kutuumiza. Kila tunapokutana na pigo baya au msiba,  mara  nyingi, sisi hukasirika na kuuliza,  “Iwapo Mungu ni mwema, na mwenye nguvu zote, kwa nini anakubalia  mambo mabaya yawatokee  watu wema?”  Swali hili hututatiza zaidi  hasa  iwapo ni sisi,  watoto wa Mungu, ambao tunaumia na kuteseka.

Katika nyakati kama hizi, nia zetu na mawazo yetu hutaka kupiga mayowe na kusema,  “Sielewi hata kidogo!”  Tena na tena  swali hili, “Kwa nini Mungu, kwa nini?” linawasumbua wale wanaoomboleza katika  maisha yao, na wale wapweke na waliokataliwa pia.

Katika 1  Wakorintho 13:12,  Mtume  Paulo  anaeleza kwamba kutakuwa na mambo tusiyoelewa katika maisha haya: Tunachoona  sasa  ni  kama  tu  sura hafifu  katika  kioo,  lakini hapo baadaye tutaona uso  kwa uso.  Sasa  ninajua kiasi fulani tu, lakini hapo baadaye nitajua yote kikamilifu, kama vile Mungu anavyonijua mimi. Kufikiri  kwingi  na  kujaribu  kutatua  mambo  ambayo hatutaweza kuyaelewa  huleta  mateso na kuchanganyikiwa  lakini katika Mithali 3:5,6 Biblia inatuambia kwamba kumtegemea Bwana kunaleta uhakika na mwelekeo: Mtumaini mwenyezi Mungu kwa moyo wako wote, wala usitegemee akili zako mwenyewe. Umtambue Mungu katika kila ufanyalo, naye atazinyosha njia zako. Wakati tumo  matatani maishani  mwetu, tunahitaji mwelekeo. Maandiko haya yanatueleza kuwa kumtegemea Mungu ndio njia ya kupata mwelekeo huo.

Kumtegemea Mungu huhitaji uwe na maswali ambayo hayana majibu katika maisha yako! Ukweli huu ni mgumu kwa wengi wetu kuukubali kwa sababu utu wa mwanadamu hutaka kuelewa kila kitu.  Katika  Warumi 8:6, tunaambiwa kuwa  “…nia ya mwili … ni akili  na mawazo bila Roho Mtakatifu…”  (AMP) Sisi hutaka mambo yapate  kueleweka, lakini  Roho Mtakatifu anaweza kutusababisha tuwe na amani hata ingawa tunapitia mambo yasiyoeleweka kabisa. Haijalishi una uchungu wa aina gani kutokana na msiba wako.

Roho Mtakatifu anaweza kukupatia amani, nawe upate kujua kuwa kila kitu kitaenda vyema. Kumkasiria Mungu hakunaa  maana kwa sababu  yeye  pekee ndiye anayeweza kutusaidia.  Yeye tu ndiye anayeweza kuleta faraja ya milele na uponyaji ambao unahitajika. Ninakuhimiza uendelee kuamini kuwa Mungu ni mwema na ujue kwamba chochote  kilichotendeka hakibadilishi ukweli huu; Mungu ni mwema. Hata kama huelewi kwa nini mambo yanakwenda kama yanavyokwenda, endela kuamini na kukiri kwamba Mungu ni mwema - kwa maana ni kweli! Katika  Zaburi  34:8, mtenzi anatuhimiza, “Jaribuni  muone Mwenyezi -Mungu alivyo mwema.  Heri Mtu anayemkimbilia usalama kwake.” Kisha katika Zaburi 86:5 anasema, “Wewe ee Bwana, U mwema, na mwenye kusamehe; mwingi wa fadhili kwa wote wakuombao.” Mwishowe katika  Zaburi  136:1, tunaambiwa,  “Mshukuruni mwenyezi Mungu kwa kuwa ni mwema; kwa maana fadhili zake zadumu milele.

Mungu ni mwema, lakini shetani anataka tuamini kwamba hatuwezi kumtegemea Mungu na kwamba  Yeye hatujali wala kutupenda.  Ikiwa una mashaka  kuhusu upendo wa Mugu kwakona  uaminifu wa ulinzi wake,  tafadhali tafakari  maneno haya ya Paulo kuhusu swala  hili yanayopatikana katika Warumi 8:35-39: Ni nani awezaye kututenga  na mapendo  ya Kristo? Je, ni taabu, au dhiki, au mateso,  au njaa, au ukosefu wa nguo, au hatari, au kuuawa?  Kama Maandiko Matakatifu  yasemavyo: “Kwa ajili yako, twakikabili kifo kutwa kucha: tunatendewa kama kondoo wa kuchinjwa.”  Lakini, katika mambo  haya yote, tumepata ushindi mkubwa kwa msaada  wake yeye aliyetupenda.

Maana ninajua hakika kwamba hakuna kitu kiwezacho  kututenganisha na upendo wake: wala kifo, wala uhai; wala malaika, au nguvu nyingine za mbinguni; wala yanayotokea sasa, wala yatakayotokea baadaye;  wala mamlaka;  Wala ulimwengu wa juu, wala wa chini kabisa. Hakuna kiumbe chochote kitakachoweza kututenga  na upendo wa Mungu kwetu kwa njia ya Kristo  Yesu Bwana wetu.

Usimkasirikie Mungu. Pokea huduma ya Roho Mtakatifu. Yasikize maneno ya Yesu katika maandiko haya: Yesu  aliwaambia, “Msifadhaike  mioyoni  mwenu. Mwaminini Mungu, niaminini na mimi pia. Nami nitamwomba Baba naye atawapeni Msaidizi mwingine, atakayekaa  nanyi milele. “Sitawaacha ninyi yatima; nitakuja tena kwenu. (John 14:1, 16,18) Farijiwa na maneno  haya na umpinge shetani ambaye atakuwa anajaribu kukufanya  umwelekezee Mungu hasira yako na usumbufu wako.

Kumkasirikia shetani:
Biblia inasema  tunafaa kuchukia uovu  (Amosi  5:15), na kwa kuwa shetani ndiye chanzo cha uovu wote, basi kuwa na hasira juu yake ni sawa - iwapo tunaidhihirisha hasira hiyo kwa njia ya kibiblia. Katika  waefeso 6:12, tunaelezwa kuwa, “Maana vita vyenu si  vita kati yetu na binadamu,  bali ni vita dhidi  ya jeshi  ovu  la ulimwengu wa roho; tunapigana na watawala, wakuu na wenye nguvu wanaomiliki ulimwengu  huu wa  giza.” Tafsiri  moja  ya kiingereza inasema,  “Tunapigana  dhidi  ya watawala wa  giza, dhidi ya majeshi ya roho za uovu…”

Ni wazi kwamba vita vyetu si dhidi ya Mungu au watu, bali ni dhidi  ya adui Shetani.Je tunaweza kuweka hasira zetu kwa njia ifaayo?

No comments:

Post a Comment