Kwa roho zetu twaweza kuunidhamisha na kuutawala mwili, lakini haihitaji juhudi. Inahitaji ushirikiano na Roho Mtakatifu Anayetupa nguvu sisi na kutuwezesha kufanya mambo mazuri. Paulo anasema hatuhitaji kuuwekea mahitaji mwili na ninaamini njia moja ambayo tumeuwekea mwili mahitaji ni kukaa bila kufanya kitu! Kukaa bila kufanya chochote ni mazoea mabaya.
Kadiri tunavyokaa bila kufanya lolote, ndivyo tunavyotaka kutofanya lolote. Nina hakika umewahi kukaa nyumbani siku nzima na kupata kuwa kadiri unavyolala hapo kitandanii, ndivyo unavyohisi ugumu kuinuka. Unapoinuka kwanza, kila kitu huwa kigumu na kuhisi uchovu, lakini unapoendelea kujilazimisha kuondoka, nguvu inakurudia. Leo niliamka nikiwa sina furaha. Nilifanya kazi juma zima kufanya mkutano na bado nahisi uchovu kiasi.
Vile vile, nilipata kukasirika kuhusu jambo fulani ambalo nilitarajia. Nilihisi nilale kwenye kochi na kujisikitikia siku nzima, lakini kwa vile kwa miaka mingi nimefanya hivyo na sijawahi kufaulu, nimeamua kufanya chaguo lingine. Niliamua kuendelea na kuandika mlango huu kuhusu matendo ninayofanya. Ilikuwa njia yangu ya kupambana dhidi ya njia ambayo mwili wangu ulihisi! Kadiri ninavyoendelea kuandika, ndivyo ninavyohisi kuwa bora zaidi. Katika hali ambayo miili yetu inatujaribu tuwe walegevu, twaweza kuanza kushinda kwa kumuuliza Mungu atusaidie na kwa kufanya maamuzi muhimu ya kuwa imara badala ya kuwa mlegevu.
Kisha tunapoendelea mbele na kufanya kulingana na maamuzi yetu, tutaona kuwa hisia zetu zinaanza kuzoea. Mungu amenipa roho ya nidhamu na kujizuia kwa siku kama ya leo, lakini ni juu yangu kuchagua iwapo nitumie kile ambacho Yeye amenipa au nifuate njia za mwili.
Paulo pia anaandika kuhusu “Wakristo mwili” ambao ni watu waliomkubali Yesu Kristo kuwa mwokozi wao, lakini hawafanyikazi na Roho Mtakatifu kuendeleza ukomavu wao wa kiroho. Katika 1 Wakorintho 1 3:1-3, Paulo anawaambia Wakristo “Lakini, ndugu zangu, mimi sikuweza kusema nanyi kama na watu wenye tabia ya rohoni, bali kama na watu wenye tabia ya mwilini, kama na watoto wachanga katika Kristo. Naliwanywesha maziwa sikuwalisha chakula; kwa kuwa mlikuwa hamjakiweza. Naam, hata sasa hamkiwezi, kwa maana hata sasa ninyi ni watu wa tabia ya mwilini. Maana ikiwa kwenu kuna husuda na fitina, je? Si watu wa tabia ya mwilini ninyi; tena mnaenda kwa jinsi ya kibinadamu?”
Paulo aliwaambia Wakristo alihitaji kuongea nao kama watu wasio wa kiroho bali wa kimwili ambao maumbile yao ya kimwili yametawala. Hangeweza hata kuwafunza mambo ya nguvu bali alizingatia kile alichokiita “jumbe za maziwa.” Aliwaambia si watu wa kiroho kwa sababu waliruhusu mahitaji ya kimwili yawathibiti. Je, unaruhusu mahitaji ya kimwili yakudhibiti? Leo nilijaribiwa kuwacha mahitaji ya kimwili yanidhibiti na kusema kweli, pengine nitahitaji kuzuia jaribu hilo kwa siku nzima kwa kufanya jambo ninaloamini kuwa litazaa matunda mema. Siwezi kufuata mahitaji ya kimwili kwa sababu sina siku ya kupoteza. Hakuna Zawadi ya Kutofanya lolote Hakuna kati yetu anayeweza kupoteza wakati wetu akikaa bila kufanya lolote. Mungu hawezi kuzawadia hali ya kutofanya lolote. Watu wasiofanya kitu hawatumii nafasi yao kufanya lile wanalojua linafaa
Badala yake, wanasubiri kuhisi kana kwamba wanafanya kitu au kutiwa motisha na nguvu za kiajabu kutoka nje. Wanatumai kitu kizuri kitatendeka, hasa kwao, na wamejitolea kutofanya lolote ilhali wanasubiri kuona ikiwa kitu kitafanyika. Mungu hafurahii tabia kama hii, kwanza ni hatari sana. Uamuzi wa kutofanya lolote bado ni uamuzi, na ni uamuzi ambao hutufanya sisi tuwe wanyonge na wanyonge sana. Unampa shetani nafasi ya kutudhibiti zaidi na zaidi. Mahali patupu bado ni mahali, na Neno la Mungu latufunza kwamba ikiwa shetani atakuja na apate utupu, yeye huujaza mara moja utupu huo (angalia Mathayo 12:43-44). Kutokuwa na lakufanya kwaonyesha kwamba tumekubaliana na kuidhinisha chochote kinachoendelea. Kwanza, ikiwa hatufanyi lolote kuibadili hali hiyo basi lazima tufikirie kwamba chochote kinachotendeka ni sawa.
Badala yake, wanasubiri kuhisi kana kwamba wanafanya kitu au kutiwa motisha na nguvu za kiajabu kutoka nje. Wanatumai kitu kizuri kitatendeka, hasa kwao, na wamejitolea kutofanya lolote ilhali wanasubiri kuona ikiwa kitu kitafanyika. Mungu hafurahii tabia kama hii, kwanza ni hatari sana. Uamuzi wa kutofanya lolote bado ni uamuzi, na ni uamuzi ambao hutufanya sisi tuwe wanyonge na wanyonge sana. Unampa shetani nafasi ya kutudhibiti zaidi na zaidi. Mahali patupu bado ni mahali, na Neno la Mungu latufunza kwamba ikiwa shetani atakuja na apate utupu, yeye huujaza mara moja utupu huo (angalia Mathayo 12:43-44). Kutokuwa na lakufanya kwaonyesha kwamba tumekubaliana na kuidhinisha chochote kinachoendelea. Kwanza, ikiwa hatufanyi lolote kuibadili hali hiyo basi lazima tufikirie kwamba chochote kinachotendeka ni sawa.
No comments:
Post a Comment