Tuesday, 5 June 2018

Mungu, Huu sio wakati Mnzuri

Biblia  inaelezea  hadithi kuhusu mwanaume  mmoja  ambaye hakumfuata  Mungu  kwa  sababu kufanya hivyo lilikuwa  ni  jambo la usumbufu  kwake. Mwanaume huyu  aitwaye Feliki,  alimtaka  Paulo aje  na  amhubirie injili.  Lakini wakati Paulo  alipoanza  kuzungumza naye kuhusu  maisha  yaliyonyooka,  usafi wa  maisha,  na  kudhibiti hamu alizo nazo, Feliki alishangaa  na kuogopa.  Alimwambia Paulo aende  zake  na kwamba  atamwita  wakati ufaao zaidi (angalia      MDO  24:25). “Na Paulo alipokuwa akitoa  hoja zake  katika habari ya  haki,  na  kuwa  na  kiasi na  hukumu itakayokuja,  Feliki  akawa na  hofu akajibu,  Sasa  enenda  zako,  nami nikipata  nafasi  nitakuita.” 

Ninashangazwa  mno na  jambo  hili, sio kwa  sababu linafurahisha, bali kwa  sababu laonyesha  wazi  jinsi  tulivyo. Hatujali kusikia kuhusu jinsi Mungu alivyo  na  upendo mwingi kwetu na  kuhusu mipango mizuri  aliyo nayo katika  maisha  yetu,  lakini wakati anapoanza  kutulaumu   kwa  makosa  tunayofanya au kuturekebisha.
kwa  njia yoyote,  tunajaribu kumwambia  kwamba  “sasa”  sio wakati mzuri. Nina shaka  kuwa  Yeye huchagua  wakati tunaodhani,  “ni mzuri,”  na nafikiri hufanya hivyo kwa kusudi lake! Wakati wana  wa  Israeli walipokuwa  wakisafiri kupitia jangwani,  waliongozwa  na  Mungu ndani ya  wingu mfano wa nguzo wakati wa  mchana  na ndani  ya moto  mfano wa  nguzo wakati wa  usiku. Wakati wingu lilipoenda,  pia nao walienda  na wakati liliposimama, walikaa  mahali  walipofika.  Jambo  la kufurahisha  ni kwamba  hakukuwa na mtindo au mpango  waliofahamu  kuhusu  ni wakati gani wingu hilo litaenda. Walilazimika kuondoka wakati wingu linaenda (angalia  HES 9:15-23). 


Biblia inasema kwamba wakati mwingine  lilienda wakati wa mchana  na wakati mwingine lilienda  wakati wa  usiku.  Wakati mwingine lilipumzika kwa  siku chache  na  wakati mwingine lilipumzika  kwa  siku moja.    Nina shaka  kuu kwamba  wakati wa  usiku waliweka ishara  isemayo “Usisumbue”  kwenye milango ya  mahema yao  ili  Mungu afahamu kuwa  hawakutaka  kukatiziwa  wapendavyo. Wakati Alipoamua ni wakati wa  kupata  ufanisi walikusanya  virago  na  kumfuata,  na wakati Anapoamua   ni wakati wetu kwenda kwenye kiwango cha pili cha  safari ndani Yake,  hatupaswi kusema, “Huu sio wakati mzuri!” Je,  halingekuwa  jambo  zuri iwapo  Mungu angelitoa  kalenda ya kila mwezi inayoonyesha siku  zote  zinazoenda ili  wajiandae kimawazo, kihisia na kimwili?  

Ninashangaa  ni kwa  nini  Hakufanya hivyo. Je, ni  kwa  sababu hutukatiza  kwa  kusudi  lake ili  aone jinsi tutakavyojibu? Mungu anajua  vyema  na  wakati  wake kila  mara  ni sawa  kabisa. Kwa  vile sijihisi kuwa  tayari  kushughulikia jambo  fulani maishani mwangu haimaanishi kuwa siko tayari. Mungu  ndiye  kiongozi wa “njia na namna”  ya mipango yetu. Njia zake  sio njia zetu, lakini  ni za juu na bora kuliko njia zetu (angalia Isaiah 55:9).

No comments:

Post a Comment