Sunday, 3 June 2018

SUBIRA,TAFADHALI!!

Biblia inasema katika  Waebrania  6:12 kwamba tunarithi ahadi zake kwa imani  na uvumilivu.  Kupokea urithi hakuhitaji bidii yoyote kutoka kwetu. Tunahitaji kungoja  tu, mpaka wakati ulioteuliwa.

Kwa  mfano  unaweza  kuamini, au  kuwa na  imani  kwamba jamaa yako fulani amekuwosia urithi fulani, lakini ni lazima uwe na uvumilivu  na  kusubiri  wakati  ufaao  kufika  ili  upokee  urithi  ule. Imani na subira ni hushirikiana katika  kutimiza jambo lolote. Zinafanya kazi pamoja kutimiza lengo linalotarajiwa. Yakobo 1:2,  3  (Tafsiri  ya  AMP)  inasema  kuwa yafaa tufurahi “tunapoangukia majaribu ya kila aina”, tukijua kwamba “kuthibitishwa kwa imani yetu” huleta saburi. Na saburi ikishafanya kazi yake kikamilifu, tutakuwa watu ambao “wamekomaa kikamilifu … wasiopungukiwa  na neno.”
Jamani! Andiko la ajabu hili!


Neno la kiyunani  “saburi” katika mstari huu ni neno,  hupomone, nalo humaanisha aina ya “subira ikuayo kupitia kwa majaribu peke  yake.”  Yaani, tunawezaje kukua  katika  uvumilivu na saburi ikiwa hatutahitajika  kungojea kile tunachokitarajia au kustahimili yale tusiyoyafurahia tukiwa katika hali ya kungojea? Tunapojaribiwa, tunakua  au angalau tunaweza kukua,  iwapo tutaruhusu “saburi ifanye kazi yake kikamilifu” (Yakobo 1:4).
```GetYourHopesUp``` .

No comments:

Post a Comment