Biblia inasema katika Waebrania 6:12 kwamba tunarithi ahadi zake kwa imani na uvumilivu. Kupokea urithi hakuhitaji bidii yoyote kutoka kwetu. Tunahitaji kungoja tu, mpaka wakati ulioteuliwa.
Kwa mfano unaweza kuamini, au kuwa na imani kwamba jamaa yako fulani amekuwosia urithi fulani, lakini ni lazima uwe na uvumilivu na kusubiri wakati ufaao kufika ili upokee urithi ule. Imani na subira ni hushirikiana katika kutimiza jambo lolote. Zinafanya kazi pamoja kutimiza lengo linalotarajiwa. Yakobo 1:2, 3 (Tafsiri ya AMP) inasema kuwa yafaa tufurahi “tunapoangukia majaribu ya kila aina”, tukijua kwamba “kuthibitishwa kwa imani yetu” huleta saburi. Na saburi ikishafanya kazi yake kikamilifu, tutakuwa watu ambao “wamekomaa kikamilifu … wasiopungukiwa na neno.”
Jamani! Andiko la ajabu hili!
Jamani! Andiko la ajabu hili!
Neno la kiyunani “saburi” katika mstari huu ni neno, hupomone, nalo humaanisha aina ya “subira ikuayo kupitia kwa majaribu peke yake.” Yaani, tunawezaje kukua katika uvumilivu na saburi ikiwa hatutahitajika kungojea kile tunachokitarajia au kustahimili yale tusiyoyafurahia tukiwa katika hali ya kungojea? Tunapojaribiwa, tunakua au angalau tunaweza kukua, iwapo tutaruhusu “saburi ifanye kazi yake kikamilifu” (Yakobo 1:4).
```GetYourHopesUp``` .
No comments:
Post a Comment