Monday, 4 June 2018

Wajibu wa mkristo kwa muislam.

Baadhi ya Wakristo wanaona kwamba Huduma ya Injili kwa muislam ni jambo la ziada tu lakini si lalazima lakini Huduma ya Mkristo yeyote Yule ni kumfanya Yesu Kristo kujulikana kwa wao wasio mjua,wawe wanaishi mbali au karibu kwake. Kuhama kwa watu toka nchi za Kiislamu hadi nchi zenye Wakristo wengi imefungua fursa mpya kwa huduma ya Kikristo katika maisha yetu ya kila siku. 

Kama mwaamini na kushiriki Injili, utapata uwepo unao endelea wa Bwana Yesu Kristo: Kwa sababu hii, enendeni ulimwenguni mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi, mkiwabatiza kwa Jina la Baba na la Mwana na la Roho Mtakatifu, nanyi wafundisheni kuyashika mambo yote niliyowaamuru ninyi. Hakika Mimi niko pamoja nanyi sikuzote, hadi mwisho wa nyakati Kuhusu Kristo na cha kuzingatia ni hapa sasa, huduma ya Kikristo kushikilia katika tarajio ni Muhimu sana kwa maisha yote, matarajio, na utu wa upeo wa Kiislam.Walakini, watu wengi hawajui jinsi ya kushiriki Injili kwa Waislam au wameogopa kufanya hivyo. Kwa ukurasa huu kuna baadhi ya miongozo jinsi ya kushiriki nao.

Ushirikiano wako na Yesu
Kuchanganya na dini nyingine inaweza kuwa uzoefu mgumu, Mungu aliwaumba wanadamu wawe na uhuru wa kuchagua. Watu wanaweza tu kuguswa na Mungu kupata ukweli. Kwa hivyo utajiuliza mwenyewe: jinsi gani ulivyo uhusiano wako na Yesu Kristo? Utahitaji moyo ulio wazi kwa Roho wa Mungu Atakapokuja huyo Roho wa kweli atawaongoza awatie katika kweli yote. Yeye hatanena kwa ajili Yake mwenyewe, bali atanena yale yote atakayosikia, naye atawaonyesha mambo yajayo. Atanitukuza Mimi, kwa maana atayachukua yaliyo Yangu na kuwajulisha ninyi (Yohana 16:13-14). Pia mtindo wa maisha yako ni wa muhimu.

Tukiwa na maisha yaliyo kweli ya Kikristo, Waislam wata ona mabadiliko Mungu amefanya katika maisha yako. Zaidi, hauhitaji kujiombea wewe mwenyewe, ila pia tuwaombee Waislam, ambao Mungu anawaleta katika umakini wetu. Inaweza kuwa watu wanaojulikana au pia wasiojulikana. Ombea hekima ndani yako jinsi unavyoweza kuwafikia wao kwa njia bora.Kama mtu ye yote miongoni mwenu amepungukiwa na hekima na amwombe Mungu, Yeye awapaye watu wote kwa ukarimu wala hana kinyongo, naye atapewa (Yakobo 1:5).

Tabia yako inayo tenda kazi
Mojawapo ya matatizo siku za leo katika kushiriki Injili kwa Waislam ni kwamba hatuna bidii sana kutembelea rafiki zetu Waislam kushiriki Injili. Wakati hatujatulia sana ulimwenguni ndipo tunaweza kutangaza ufalme wa Bwana wetu. Wakati Wakristo wameandaliwa kufanya vitu vya Injili ya Yesu, aliye tuitia kutangaza, Waislam wengi wangefikiwa leo hii.[15] Nayo miguu yenu ifungiwe utayari tuupatao kwa Injili ya amani (Waefeso 6:15). Ni vema kufanya mapatano kwako mwenyewe au na wengine kuwa pale ambako Waislam wapo na kuanza mazungumzo na wao.
Waambie Waislam Kuhusu Yesu
Hapa katika hutua ya kuanza mazungumzo na Muislam kushiriki Injili. Kila mtu ni tofauti na pia kuna tofauti katika mazingira. Kwa kila mazungumzo ni ya ajabu. Kukupa wewe tukio jinsi mazungumzo yanavyoweza kuendelea, hapa kuna maswali yafuatayo na majibu:
1. Je huna ufahamu wa Injili ya Yesu Kristo? Waislam wengi watasema: Mimi Muislam. Kwa sentensi hii wanataka kuonyesha kwamba jamii zao zina toka nchi ya Kiislam na kwamba Injili ya watu kutoka Magharibi, na si wao.Baada ya wazo hili, utaweza kuangalia swala muhimu la kila mwanadamu:
2. Je una uhakika unaenda Mbinguni ukifa? Waislam wengi watasema hawana uhakika kwamba wanaenda Mbinguni kama mtume muhammad. Wataongeza ya kwamba hakuna anayejua awe mke au mume hana uhakika kama wanaenda Mbinguni. Kwa hivyo utaweza kuuliza swali lifuatalo:
3. Je umewahi kusema kitu kisicho kuwa kweli au kuchukua kitu kisicho kuwa chako?
Marafiki zetu Waislam wengi wao watakubali wamewahi kufanya makosa, iwapo hawawezi, unaweza kuwaliza iwapo wamewahi kufanya makosa katika kutotii mojawapo ya amri. Mwishowe watakubali wamewahi kufanya hata kosa mojawapo.
4. Je una taka kumkubali Yesu Kristo kama Mwokozi wako kibinafsi?
Katika nchi ambako imani ya Kikristo haifanyi kazi, utaweza kusema hadithi yako jinsi ulipata kufanya uhusiano na Yesu Kristo kama mwokozi wa maisha yako. Utaweza kumalizia swali: Je unafikiri nini kuhusu haya? Ni uhuru wa kila mmoja aseme, awe waume au kike anataka kumkubali Yesu Kristo kama Mwokozi wa maisha yake. Waislam watasema ‘hapana’. Wengine ni wapole kwa kusema watafikiri kuhusu mambo hayo. Hata hivyo kuna Waislam wanao mkubali Yesu Kristo na wanaziidi kuongezeka kila mwaka.
5. Omba maombi ya mwenye dhambi
Hapa sasa tuna fika hatua ya mwisho ambako Roho Mtakatifu atamwongoza rafiki yetu Muislamu kumpokea Yesu Kristo. Utamwuliza rafiki yako kuomba maombi ya mwenye dhambi.
6. Waalike wao waje Kanisani
Baada ya kuokoka, rafiki zetu wanahitaji kuja kanisani kufanywa wafuasi: kulingana na miongozo ya Bibilia. Mpe Mungu utukufu: Basi msifurahi kwa kuwa pepo wachafu wanawatii, bali furahini kwa kuwa majina yenu yameandikwa mbinguni (Luka 10:20).

No comments:

Post a Comment