Monday, 4 June 2018

Kukaa Bila kufanya kitu humwalika Adui


Kulala kwenye kochi au kuegemea kwenye kiti maalum kumuuliza Mungu  alinde  kila kitu kinachohitaji  kufanywa  ni  rahisi, lakini inatuwacha  tusiwe na  la  kufanya  na  kutozaa  matunda na  kutuweka wazi  kushambuliwa na muovu. Ikiwa  akili zetu hazina  mawazo mazuri, shetani anaweza kuzijaza  mambo mabaya kwa  urahisi. Ikiwa  tu walegevu na  hatufanyi lolote,  anaweza  kutujaribu kufanya  makosa  na  hata  mambo  machafu.  Biblia inatuambia  kila mara tuisome kujikumbusha  na itatuepusha kuwa  walegevu na watu wa  kutozaa  matunda.  Tukifikiria  kwa  bidii  kile  tunachoweza kuwafanyia  watu wengine hakutakuwa  na  nafasi katika  akili zetu ya kuwa na mawazo mabaya.

Watu  wasiokuwa  na  lakufanya  huvunjika moyo  kwa  urahisi, hulemewa  kimawazo,  na  kujisikitikia wenyewe.  Wanaweza kuanguka  katika  aina  zote  za  dhambi. Mtume Paulo  hata alisema ikiwa mwanamke aliye  bado kijana amekuwa mjane, anapaswa  kuolewa  tena. Lau  sivyo huenda asiwe na lakufanya na  kuanza  masengenyo  na  kuwa  mdakuzi  wa  mambo  (angalia Timotheo  1 5:11-15).  Paulo aliendelea  kusema kwamba  baadhi  ya wajane  ambao  bado  wangali vijana  kwa  kutokuwa  na lakufanya tayari walikuwa wameanza kumgeukia shetani. Ina umuhimu gani kuendelea kuwa  imara?  Ninaamini maandiko  ya  Paulo yanathibitisha  kwamba  ni muhimu.
Kwanza,  katika  maandiko Mungu anatuhimiza sisi tusiwe watu wa  kutokuwa  na lakufanya. Nyakati za  Agano  la Kale, wakati mtu alipofariki wana  wa  Israeli waliruhusiwa kuomboleza  mpendwa  wao  kwa  siku  thelathini (angalia  KUM  34:8). Kwanza,  huenda ikaonekana  kuwa  si muhimu, lakini Mungu alifanya  sheria hiyo kwa  sababu alijua kwamba muda  mrefu  wa kuomboleza na kutokuwa na lakufanya unaweza kusababisha matatizo mabaya. Lazima  tukae imara  tusijihusishe  kupita kiasi bali tujihusishe vyakutosha  ili  tuweze kuendelea  katika mwelekeo ufaao.
Kujipanga katika  mambo tunayoyafanya  ni muhimu.  Hatuwezi kutumia muda wetu  wote kusaidia watu wengine, lakini  kwa  upande  mwingine, kutotumia  muda  huo  kulingana  na  mpango  huenda kukasababisha matatizo. Ikiwa  unaweza  kumkumbuka mtu unayemjua asiyekuwa na lakufanya, na ambaye hajishughulishi na jambo lolote pengine pia utatambua kwamba  hawana  furaha  kwa  sababu kutojishughulisha na jambo lolote na kukosa  furaha  mambo haya mawili  huwa pamoja. 

Miaka  kadhaa  iliyopita  shangazi  yangu  alihitaji kuhamia katika makazi ya kupewa  usaidizi. Kwa  miaka mitatu au minne  ya kwanza  alitaka  kukaa  tu bila kufanya  lolote.  Alihuzunika kwa  vile aliondoka nyumbani  na hakuwa  na nia ya kushiriki  katika maisha mapya  yaliyokuweko.  Ingawa  kulikuwa na  shughuli nyingi   na  hata nafasi za  kusaidia wengine,  hakutaka  kufanya  lolote. Siku baada  ya siku alikaa  tu nyumbani  kwake na alivunjika moyo. Alihisi vibaya mwilini  na  mara  nyingine alikuwa  na  wakati mgumu kukabiliana na hali hii. Hatimaye alifanya uamuzi kwamba  hangeendelea  kukaa tu  bila kufanya  lolote na  akajihusisha  na  mafunzo  ya  Biblia  na kutembelea  wagonjwa  katika hospitali iliyo karibu na makazi  yake. Alicheza  michezo,  akahudhuria  karamu,  kukutana  na  marafiki wengi. Muda si muda  alikuwa akinieleza  kuwa ana  furaha  zaidi kuliko alivyokuwa  maishani mwake na anahisi vizuri zaidi mwilini. 

Hali ya  mtu mlegevu huanza  kuwa  mbaya  hadi mbaya  zaidi hadi ulegevu wake unapoanza  kuathiri kila sehemu  ya  maisha  yake. Yeye huruhusu kuyumbushwa  huku na  huko  na  mazingira yake na  hali ilivyo.  Huwacha  hisia zake zimuongoze,  na  kwavile hajihisi kufanya  lolote,  yeye hutazama  tu na  kulalamika  huku maisha yake yakisambaratika. Anataka  kufanya  mambo mengi, ilhali amezongwa  na  hisia  asizoweza  kuzieleza.  Anahisi  ulegevu na  hana  mawazo  ya  ubunifu. Anaweza  hata  kuanza  kufikiria kuwa kuna kitu  kilicho kasoro  mwilini  mwake  na hiyo ndiyo sababu  hana nguvu. Kwake yeye, maisha yamekuwa urithi wa matatizo mengi. Kujiruhusu  kukaa  tu bila kufanya lolote mara nyingi  hutokea baada  ya  kupata  pigo  au  msururu wa  mambo  ya  kughadhabisha, au wakati mikasa  inapotokea,  ambayo nitazungumzia  mwisho wa  mlango huu. Wakati mambo kama  haya yanapotokea, huenda tukataka  kukata  tamaa,  lakini  tunapofanya hivyo, shetani anasubiri kuingia na kuchukua fursa ya hali ilivyo. Hatuwezi kwa  sababu yoyote  kuruhusu ulegevu kumpa nafasi  adui aingie katika  maisha yetu.

No comments:

Post a Comment