Mambo Ya Walawi 26:4 inasema, “Nitazinyezesha mvua zenu kwa nyakati zake.” Wagalatia 6:9 kwa tafsiri ya AMP inasema ni lazima “…tusife moyo na kuwa wachovu na kuzimia katika kutenda kiungwana na kutenda yaliyo ya haki, maana kwa wakati wake na kwa msimu ulioteuliwa tutavuna, kama tusipouachilia na kupunguza ujasiri wetu na hapo kuzimia.”
Na katika 1 Petro 5:6 tunatiwa moyo “kujinyenyekeza chini ya mkono wa Mungu wenye nguvu, ili wakati wake ufaao utakapotimia” atatuinua. Msimu mwafaka au wakati ufaao ni lini? Naamini ni wakati Mungu anajua kuwa tuko tayari, wakati ambapo kila mtu anayehusika ako tayari na wakati jambo hilo linaingia vizuri katika mpango mkuu wa Mungu unaojumlisha mabo yote. Mungu anao mpango wa kipekee kwa maisha yetu binafsi, lakini pia anao mpango wa jumla kwa ajili ya ulimwengu wote.
Waaaoh safi sana mtumishi wa bwana mungu akutie nguvu nyingi
ReplyDelete