Monday, 28 May 2018

CHANZO CHA TATIZO


  • "Nilidhulumiwa  kingono  na  baba  yangu  mzazi  kwa  miaka  mingi. Nilijaribu mara  mbili  tofauti  kumwambia mtu fulani  kilichokuwa kikitendeka  kwangu  na kwa  vile  hawakunisaidia,  niliendelea kuteseka peke yangu  hadi nikawa  mtu mzima na  hatimaye nikaanza kuzungumza  hadithi yangu  na  watu wengine na  nikapokea. uponyaji kutoka  kwa  Mungu."






Ufunguo wa furaha si kupendwa, bali ni kuwa na mtu wa kupenda.

Chanzo  cha  jambo  ndio  mwanzo  wake,  na  msaada  wake.  Mizizi kawaida  huwa  chini ardhini. Na  kwa  sababu hiyo  mara  nyingi twapuuza  na  kuzingatia  tu  kile tunachokiona  juu ardhini. Mtu anayeumwa na jino mara  nyingi anahitaji  kujua chanzo  cha  jino linavyouma. Mzizi wa  jino hilo umeoza na lazima uchunguzwe bila hivyo jino lote halitakoma kuwa na uchungu. Mzizi wa  jino hauwezi  kuonekana,  lakini unajua  uko  hapo  kwa  sababu uchungu ni mwingi.
Ulimwengu una  uchungu,  na  uchungu huo hautakoma hadi pale tutakapojua  chanzo  cha  matatizo  yanayowakumba  watu binafsi na jamii. Ninaamini kwamba  chanzo  ni uchoyo.   Nimejaribu kufikiria  juu ya tatizo ambalo  halianzii na uchoyo, na sijapata hata moja.
Watu hawajali  juu  ya kuharibu maisha ya wengine  ili  kupata kile wanachohitaji au kile wanachoonelea ni bora kwao. Nimejaribu kufikiria juu ya tatizo ambalo halianzii na uchoyo, na sijapata hata moja. Kwa  neno kamili, uchoyo ndio chanzo  cha  matatizo  yote ulimwenguni.


Uchoyo Una Maelfu ya Sura

Uchoyo  una Maelfu ya  Sura,  na  pengine hiyo  ndiyo  sababu hatuutambui ni nini.  Tunauona  kwa  watoto  ambao  hulia wakati wasipopata  kile  watakacho  na kwa  watoto  ambao  huchukua vikaragosi vya  kuchezea  vya  watoto  wengine.
Hii  ni dhahiri katika mawazo  yetu kuonekana tuko hali bora  kuliko wengine  au kufanya vyema kuliko wanavyofanya.  Uchoyo ni  kuhusu  kuwa wa  kwanza katika kila jambo, na ingawa hakuna makosa ya kutaka  kufanya vyema  zaidi,  ni makosa  kufurahia  kuwaona  wengine wakikosa kufaulu ili sisi tufaulu.

Ninaamini  kwamba  uchoyo wa aina yote ni  mbaya na kwamba unasababisha matatizo. Katika  sehemu  hii, nataka  niyalete mawazo yako kwa  aina tatu maalum za  uchoyo ambao  kwa  kawaida unapatikana  katika  ulimwengu wa  leo na  matokeo  mabaya yanayotokana na uchoyo huo.

Dhuluma  za  kingono: 
Ann  ana  umri  wa  miaka kumi  na mitatu. Baba  yake humwambia yeye ni mwanamke sasa  na kwamba wakati umefika kwake kufanya  yale ambayo  wanawake hufanya. Anapomaliza  kumuonyesha  kile anachomaanisha  kuwa  yeye ni mwanamke, yeye huona haya,  huwa  na hofu na kujiona mchafu. Ingawa  baba  yake humhakikishia kwamba  kile  anachofanya  ni jambo zuri, yeye hushangaa  ni  kwa  nini  humtaka aliweke jambo hilo kuwa siri na ni kwa nini linamfanya ahisi vibaya. Huku  miaka  ikiyoyoma  na  baba  yake akiendelea kumdhulumu na  kumbaka,  Ann hufunga  hisia zake kwa  hiyo  hahitaji  kuhisi uchungu tena.  Baba yake Ann ameuiba utoto  wake, ubikira  wake, uhalali wake, na bila ya  mwingilio kutoka  kwa  Mungu, ataiba maisha yake ili kupata kile alichokitaka. Twachukizwa  mno  na visa vya kina-baba kuwabaka  watoto wao  na  visa  vya  watu  wa  familia kujamiiana  tunavyosikia,  lakini ukweli  ni  kwamba  asilimia 90-95 ya visa hivyo haviripotiwi.

Nilidhulumiwa  kingono  na  baba  yangu  mzazi  kwa  miaka  mingi. Nilijaribu mara  mbili  tofauti  kumwambia mtu fulani  kilichokuwa kikitendeka  kwangu  na kwa  vile  hawakunisaidia,  niliendelea kuteseka peke yangu  hadi nikawa  mtu mzima na  hatimaye nikaanza kuzungumza  hadithi yangu  na  watu wengine na  nikapokea. uponyaji kutoka  kwa  Mungu.
"Baba yangu  alifariki akiwa  na umri  wa  miaka  themanini  na sita  bila ya  kuadhibiwa  kwa  uhalifu alionitendea. Watu aliofanyakazi  nao  na  aliohudhuria nao  karamu na  dhifa mbali mbali hawakujua  alikuwa  akimbaka  bintiye tangu alipokuwa msichana mdogo."Jesca..
Twaona yale watu wanayofanya na kuwa haraka kuwahukumu, lakini  tunajua chanzo  cha  tabia zao?  Wanawake wengi tunaowahukumu kuwa “matatizo  katika  jamii”  ni wahasiriwa  wa kubakwa na baba zao au watu wa familia zao.
Kwa mfano,  
          •Asilimia 66 ya makahaba wote ni  wahasiriwa  wa  dhuluma za kingono walipokuwa watoto.
          •Asilimia 36.7 ya wanawake walio gerezani nchini  Tanzania walidhulumiwa walipokuwa watoto.
           •Thuluthi  moja ya watoto  walio dhulumiwa  na kutelekezwa baadaye huwadhulumu  na kuwatelekeza  watoto  wao wenyewe.
          •Asilimia 94 ya  wahasiriwa  wa  dhuluma za  kingono  huwa chini ya umri wa miaka kumi na miwili wanapodhulumiwa. Uchungu unaosababishwa  na visa vya  kina baba  kuwabaka watoto  wao  na watu wa  familia kujamiiana na dhuluma za  kingono ulimwenguni ni mkubwa  mno na  yote  yalianza  kwa  sababu watu  ni wachoyo na hawakujali ni  nani  atakayeumia  ilimradi  wamepata kile wakitakacho.

Ndio,  pengine hutaua,  hutaiba,  hutadanganya,  wala  kutenda vitendo vya  dhuluma  dhidi  ya  watoto, lakini kuna uwezekano kwamba  u mchoyo  katika  njia fulani. Ikiwa  tutakuwa  na  msamaha wa  uchoyo  wetu kwa  kuwaelekezea  kidole cha  lawama  wale ambao  uhalifu  wao  ni  mbaya kuliko wetu, hatutafaulu kukabiliana na matatizo haya katika jamii hivi  leo. Kila mmoja wetu  lazima achukue jukumu  la kukabiliana na tabia yetu ya uchoyo, haijalishi ni wa kiwango gani  au kwa njia ipi tunayoueleza. Ulafi:  Uchoyo  mara  nyingi huchukua  njia ya  ulafi. Ulafi ni roho ambayo hairidhiki  na kila mara inataka  zaidi. Jamii  yetu  hivi
leo imezoea  kutumia mambo  yaliyoko.  Nilishangaa  nilipokuwa nikiendesha  gari  na  kuona  majumba  ya  ukahaba  yaliyoko  na  yale yanayojengwa.  Uchafu, uchafu, na uchafu mbaya  zaidi na yote si mambo ya  kweli. Yanaahidi  maisha  rahisi na furaha  zaidi,  lakini kwa watu wengi yote yanayobuniwa ni deni la unyanyasaji. Shinikizo na  majaribu ya  kununua zaidi na  zaidi ili kutufanya tuingie  katika uchoyo.

Lakini habari njema ni  kwamba  twaweza kubadilika ikiwa  kweli  twataka  kufanya  hivyo. Hebu tujifunze kununua  kile  tunachohitaji  na baadhi ya yale tunayotaka  na kisha tujifunze  kutoa  sehemu  ya mali yetu, hasa  yale ambayo hatuyatumii tena  kwa  mtu ambaye anahitaji.  Hebu tujizoeshe  kutoa  hadi pale litakapokuwa  jambo  la  kwanza  na  la  kawaida  tufanyalo  kila siku za  maisha yetu. Kwa  watu wengi  hii  kweli  itakuwa  njia ya kugeuza maisha yao. Biblia inasema kwamba kupenda  fedha  ndicho chanzo  cha maovu  (angalia 1 TIM 6:10). Sababu  ya pekee  ya watu kupenda pesa  na  watafanya  chochote  kupata  ni kwamba  wanafikiri pesa zitawafanya  wapate  kila  watakacho.

Wanaamini  zinaweza  kununua furaha.  Watu kila mara  huua, kuiba na kudanganya  ili  wapate pesa na haya  yote chanzo  chake ni ugonjwa  huu wa  uchoyo. Hivi majuzi nilisoma  taarifa  fulani ya  mcheza  sinema mmoja  mashuhuri aliyesema watu wanaamini  kwamba  ikiwa wana  vitu vyote wanavyohitaji  basi  watakuwa  na  furaha,  lakini ni ahadi  ya  uongo. Aliendelea  kusema kwamba alikuwa na kila kitu  mwanaume alichopaswa  kuwa  nacho  na  aligundua kuwa  bado  hakupata  furaha kwa  sababu wakati mtu anapotimiza  lengo  lake la  kumiliki  kila kitu kipatikanacho duniani bado amesalia yeye mwenyewe.

Ndoa  Kuvunjika:
   Uchoyo pia ni  chanzo  cha  Ndoa kuvunjika. Watu mara  nyingi huoana  wakiwa  na mawazo  tofauti  ya  vile ndoa  inavyopaswa  kuwa.  Wengi wetu huamua kwamba  mume au mke wetu ni mtu anayepaswa  kutufanya  kuwa na furaha,  na wakati jambo  hili  lisipotendeka,  vita huanza.  Ni  toafuti ipi  ambayo ingelitokea iwapo  tungeoa  au kuolewa  na kuweka akili zetu kufanya tutakalofanya  ili kuwawafanya  waume au wake zetu kuwa  na furaha!  Kwa  sasa  hivi huenda unafikiria,  sitafanya hivyo  kwa  sababu najua  mtu atachukua fursa ya mambo  yalivyo.  Katika  miaka  yangu  ya mwanzo  ningelikubali. Lakini baada  ya maisha marefu ninaamini Biblia ni  ya ukweli.  Inafundisha  kuwa upendo  haushindwi (angalia 1 KOR 13:8). Pia inasema kwamba  kile  mtu  apandacho  ndicho atakachovuna (GAL  6:7).  Ikiwa  ninaamini Biblia na  ndivyo ninavyoamini, basi ninaamini kwamba  ninasimamia mavuno ninayopokea katika maisha yangu,  kwa  sababu yanategemea mbegu ninazopanda.  Ikiwa tunapanda  huruma tutavuna huruma, ikiwa tunapanda ukarimu tutavuna ukarimu.

Yesu alikuja ili  kufungua milango ya  gereza  na kuwafanya walio kifungoni kuwa huru (angalia ISA 61:1). Ameniweka huru kutokana  na mambo mengi, lililo  kuu  zaidi ni  mimi  mwenyewe. Nimewekwa huru  kutokana na mimi!  Ninaendelea kukua kila siku katika  uhuru huu, lakini nina shukuru kutambua kwamba  furaha halisi haipatikani kwa mambo yangu kwenda vizuri kila wakati. Pengine  kama  vile  mimi, wewe pia ulikuwa na  mifano mibaya maishani na unahitaji kuondoa mambo ambayo ulikuwa umejifunza katika  miaka  yako ya  mwanzo. Kuwa  mwaminifu. Je, utafanya nini  usipopata  kile ukitakacho?  Utakasirika?  Utanung’unika na kulalamika? Unaweza  kumwamini  Mungu  akulinde  au unaishi katika  hofu ambayo  ikiwa  hutajilinda mwenyewe,  hakuna atakayekulinda? Kuamini  kuwa ni lazima ujilinde  wewe mwenye kusababisha uchoyo, unaosababisha maisha yasiyokuwa na furaha.

Ninakuhimiza ujiepushe na uchoyo hivi leo na uanze kuthamini,  kulinda  na kuwapenda kwa ukweli watu wengine. Uchoyo ni Chaguo Wengi wetu hutumia muda  mwingi kufikiria, kuongea  na  kufanya mipango yetu wenyewe. Ingawa  ninafunza kwamba  twapaswa kujipenda  sisi  wenyewe katika njia ya uwiano, siamini  kuwa tunapaswa  kujipenda sana  hivi kwamba  tuwe katika  ulimwengu wetu na  kujali tu kile  tunachotaka  tupate. Kwa  njia zote  lazima tujitunze   kwa  sababu sisi  ni  wa  thamani kuu  kwa  mpango wa Mungu hapa  duniani.  Alitupa uhai kwa  hivyo  lazima  tuufurahie (angalia  Yohana  10:10). Kwa  hivyo tunahitaji  kuutafuta,  lakini lazima  tusikose kutambua  kwamba  njia ya  kweli ya  kupata  furaha ni kuyatoa  maisha  yetu kuliko  kujaribu kujiwekea  maisha  hayo  sisi wenyewe. Yesu anasema  kwamba ikiwa  tunataka  kuwa  Wanafunzi wake,  lazima  tujisahau,  tukose kujionea sisi wenyewe na  maslahi yetu yote  na  tumfuate Yeye (angalia  Marko  8:34).

 Sasa  nakubali kuwa hili  ni  wazo  la kutisha, lakini  nina  nafasi maana  nimeishi  kwa muda mrefu  wa  kuweza  kulijaribu na  nimegundua  kuwa  linafanya kazi.  Yesu kadhalika  anasema  kwamba  ikiwa  tutayatoa  maisha  ya chini”  (maisha  ya  uchoyo) tutapata  maisha  ya  “juu”  (maisha  yasiyo ya  uchoyo), lakini tukiyaweka maisha  ya  chini tutapoteza  maisha ya juu  (angalia Marko 8:35).
Anatupatia chaguo kuhusu  jinsi tutakavyoishi. Anatuambia kile  kitakachotufaa  na kisha kutuacha tuamue iwapo  tutafanya  au  lah.  Ninaweza  kuendelea kuwa  mchoyo na pia wewe  waweza kufanya hivyo, lakini  habari njema  ni  kwamba si lazima  tufanye hivyo. Tuna nguvu ya  Mungu ya  kutusaidia kuyapita  mambo yetu na kuishi  maisha ya kuwafanya watu wengine waishi maisha bora. Safari Uchoyo  si tabia  ya  kujifunza, tunazaliwa  nayo.  Ni sehemu ya maumbile yetu.  Biblia inautaja  uchoyo  kuwa  “maumbile ya  dhambi.”
Adamu na Hawa  walifanya  dhambi kwa  Mungu kwa  kufanya  kile alichowaamuru wasifanye na  dhambi kuu waliyoifanya  ilipitishwa kwa  kila mtu ambaye  alizaliwa.
 
Mungu  alimtuma Mwanawe  Yesu afe kwa ajili  ya dhambi, na kutukomboa kutokana  na dhambi  hiyo. Alikuja kutangua  kile  ambacho  Adamu alikifanya.  Tunapomkubali Yesu kuwa Mwokozi wa maisha yetu, Yeye huingia na kukaa pamoja nasi katika  roho  zetu na ikiwa tutaruhusu  sehemu hii iliyofanywa upya katika  nafsi zetu ili  kuyatawala  mawazo  yetu, twaweza kuishinda  dhambi ambayo imo milini  mwetu. Dhambi huwa haiendi mbali, lakini Yule mkuu anayeishi ndani yetu hutusaidia kuishinda kila siku (angalia  Wagalatia  5:16). 

Hii haimaanishi kwamba  hatufanyi dhambi, lakini tunaweza  kuimarika na  kupata ufanisi katika maisha yetu. Siwezi kusema kabisa  kabisa  kwamba  nimeushinda uchoyo,  na sidhani kama  kuna mtu yeyote  ambaye ameushinda  kabisa  uchoyo. Kusema hivi ni  kama  kusema kwamba  hatufanyi dhambi, kwa sababu dhambi yote inaanzia na aina  fulani  ya uchoyo. Sijashinda uchoyo  kabisa  kabisa,  lakini nina matumaini ya  kuimarika kila  siku. Niko safarini na ingawa  huenda  sitawasili, nimejitolea kwamba wakati  Yesu atakapokuja  kunichukua kurudi nyumbani,  atanipata ninaendelea kusukuma lengo hili (angalia Wafilipi 3:12-13).

Mtume  Paulo alisema maneno  yafuatayo: “Nimesulubiwa pamoja  na Kristo; lakini ni  hai; wala  si  mimi  tena, bali Kristo yu hai  ndani yangu;  na  uhai nilio nao  sasa  katika  mwili, ninao katika imani ya  Mwana  wa  Mungu,  ambaye alinipenda akajitoa  nafsi yake kwa  ajili yangu  (Wagalatia  2:20).
Paulo  alimaanisha  kwamba  haishi tena kwa  ajili  yake mwenyewe na mapenzi yake, bali kwa  Mungu na  mapenzi ya  Mungu. Nilitiwa moyo  sana  siku moja  wakati nilipogundua kupitia mafunzo ambayo Paulo alisema maneno haya  miaka  ishirini  baada  ya  kuokoka  kwake.  Kujifunza kuishi bila uchoyo ndiyo iliyokuwa  safari  yake, kama  ilivyo kwa  kila mmoja wetu. Paulo pia alisema “Nina kufa kila siku  (ninakabiliwa na kifo kila siku na kufa ndani yangu).”  (1 Wakorintho  15:31). Kwa  maneno mengine kuwatanguliza  wengine kwanza vilikuwa vita  vya  kila siku na kulihitaji uamuzi wa  kila siku. Kila mmoja  wetu lazima  aamue  jinsi tutakavyoishi na  kitakachotufanya tuishi kwacho,  na  hakuna  wakati bora  wa  kufanya  hivyo  kuliko sasa. 
Wewe na  mimi tuna  wakati  mmoja  wa  kuishi na  uhai  mmoja wa  kutoa,  kwa   hivyo swali ni: “Je, tutaishi vipi?”  Ninaamini kabisa kwamba ikiwa kila mmoja wetu atafanya sehemu yake kuyatanguliza maslahi  ya  watu wengine kwanza  basi  twaweza  kuona  na  kuwa sehemu ya mageuzi yenye uwezo wa kubadili ulimwengu.

No comments:

Post a Comment