Thursday, 31 May 2018

Nisaidie!Niko mpweke.

Shangazi yangu aliniambia kuwa baada ya mjomba wangu kufa, wakati  mwingine alilia usiku huku  akipiga  mto wake na kusema, “Kwa nini uliniacha?” Alijua katika nia yake kwamba hakumwacha kimakusudi, lakini hiyo ilikuwa ni sauti ya hisia zake.
Tunahitaji kujua kuwa hisia  zetu zina sauti, na wakati zinapokuwa zimeumia, basi zinaweza kuitikia hali tunayoipitia  kama mnyama aliyeumia. Wanyama walioumia wanaweza kuwa  hatari,  na hisia zilizoumia zinazweza kuwa hivyo pia tukizifuata na kuzitii. Wakati mtu  ana  msiba,  ni  muhimu  asiache  hisia  zilizoumia zimfanye kuwa mwenye chuki na uchungu moyoni.

Wakati pigo linakuwa ni talaka, ni rahisi kumchukia yule aliyesababisha utengano au hata kujaribu kulipiza kisasi. Usiharibu maisha yako kwa kuendelea kuwa na uchungu moyoni. Badala  yake, mwamini Mungu kuwa anaweza kuchukua yale ambayo yametukia na kukufanya uwe mtu bora zaidi. Jambo hilo  hilo  linalokuumiza  linawafinya  wengi  pia.  Mwombe  Mungu achukue “majivu” yako na akupe “uzuri” badala yake.


Mwombe akuwezeshe kuwasaidia wengine wanaopitia maombolezo na upweke kama wewe. Hata wakati mpendwa anapokufa unaweza kuwa na wakati ambapo una hasira   kwake kwa sababu amekuacha  peke yako.
Unaweza kuwa unasema katika  mawazo yako, “Kama ungejaribu sana, hungelikufa,”  au, “Unawezaje kuniacha niwalee watoto pekee na nibebe majukumu haya peke yangu,Kwanini Umeniacha katika Hali hii?” Hata ingawa mawazo kama haya yanaweza kuonekana kama mzaha  kwa mtu ambaye haupitii msiba  nyakati za kawaida, msiba unapoingia  ghafula na huzuni  kutuzingira,  kuna  uwezekano wa “kuwalaumu” wengine  kwa sababu  ya  uchungu tunaouhisi. Mawazo na hisia zinaweza kubadilika -badilika. 

Wakati  mmoja unaweza kuwa na hasira  dhidi  ya Mungu, wakati mwingine hasira juu yako mwenyewe, na wakati mwingine juu ya shetani na  juu  ya mtu  aliyesababisha pigo  au  msiba  huo.  Mwenendo  huu unaweza kurudiwa tena na tena hata uanze kumchanganyisha mwenye msiba. Wakati tunapoumia moyoni, njia ya kawaida ya kibinadamu ni kukasirika na kujaribu kujiondoa mbali na uchungu tunaoupitia. Hii ndio maana ni muhimu kuelewa kipindi cha kuomboleza na kufahamu kuwa kuna hisia ambazo huambatana na kipindi hiki. Katika nyakati zilizopita wengi wetu tulifundishwa kutothamini hisia zetu - kuzichukua kama jambo lisilo la maana. Baada  yako kupatwa na pigo au msiba  katika maisha  yako, huo si  wakati wa kukataa hisia zako au kujiingiza katika mambo mengine ambayo  yatakutia dhiki au uchungu zaidi.  Badala  yake, unafaa kukabiliana na hisia zako na uzitulize.

Hakuna suluhisho katika  kujaribu kuzizuia hisia zako, bali jambo la busara ni kuzitambua na kuzikabili kama ipasavyo.

GetYourHopesUp .
Jimmy J.

No comments:

Post a Comment