Sunday, 27 May 2018

KUWA NA MATUMAINI YA KWENDA MBELE ZAIDI

 

...bali  wao  wamngojeao BWANA watapata  nguvu  mpya.   Watapanda juu kwa mbawa kama tai...   Isaya 40:31 (SUV) 

 
Mara  kwa mara  watu  huhisi  kuwa mtu  akitarajia  zaidi ya  alivyo navyo basi ni mlafi  au anafanya makosa. Ijapokuwa ni kweli kwamba wakati  wote  tunapaswa kuridhika na kutosheka na yale  tuliyo nayo, haimaanishi  kuwa  kutamani kuwa  na vitu vizuri  ni makosa  alimradi tuna sababu nzuri ya kuvitamani.  Tunawezaje  kutosheka na huku bado tunataka  kuwa  na vingi?  Mimi  sasa  hivi  ninatosheka sana na kila kitu katika maisha  yangu kwa  sababu ninaamini  wakati wa Mungu  maishani  mwangu  ndio  mzuri  zaidi.  Ninaweza  kufurahi hata  kama sina kitu chochote  cha ziada kwa sababu furaha  yangu na kutosheka kwangu viko  katika Kristo. Hata  hivyo, wakati  huo huo ninataka  niwe  na vitu vingi zaidi kwa sababu ninataka  niendelee katika maisha kadri Mungu atakavyoniruhusu  na nimfanyie mengi na pia  niwafanyie wengine  mengi  iwezekanavyo. Sitaki  kitu kingine zaidi isipokuwa  maisha mazuri zaidi ambayo Mungu anataka kunipa! Ninamtaka  Mungu  zaidi  maishani  mwangu,  ninataka  kuwa karibu  naye,  niishi  ndani  yake  (Wafi lipi  3:10).  Ninataka  hekima zaidi,  uthabiti  zaidi,  na  marafiki  wengine  zaidi  walio  wazuri. 

Ninataka  wanangu  wawe  na  kila  kitu,  na  ninataka  watu  wengine zaidi  wampokee  Yesu  kuwa  Mwokozi  wao.  Ninataka  kuona  miujiza mingi zaidi, watu wakiponywa zaidi, ushindi, na nguvu. 

Ninaamini  kabisa  kwamba  tunaweza  kutosheka  kufikia  kiwango cha kutosumbuka  au kutokuwa  na wasiwasi  na yale  tuliyo nayo, na wakati  huo huo tukitamani  mengi  zaidi kwa sababu fulani nzuri na kwa wakati ufaao (Wafilipi 4:11. 19). Kusema kweli ninaamini kwamba wale wanaotosheka na kiwango cha  chini cha  yote  ambayo  Mungu anaweza  kuwatendea  wanazuia ukuu wa Mungu. Anataka ajidhihirishe kuwa ana nguvu katika maisha ya  kila  mmoja wetu.  Basi atukuzwe  yeye  awezaye  kufanya mambo ya ajabu mno kuliko  yote  tuyaombayo au tuyawazayo, kwa kadiri ya nguvu itendayo kazi ndani yetu (Waefeso 3:20).
Pandisha Kiwango Chako cha Matarajio
Umtumainie BWANA,  uwe imara,  Upige moyo  konde,    naam, umngoje BWANA.   Zaburi 27:14 “Matarajio makubwa ndio ufunguo wa kila kitu.” —Sam Walton
Hebu niwasimulie  kisa  cha mwanamke mmoja aitwaye  Betty. Betty ni  mwamini.  Yeye  husoma  Biblia  mara  kwa  mara.  Mara  moja  kwa mwezi yeye hujitolea  kwa kuwagawia blanketi  watu wasiokuwa  na makazi. Betty anaonekana mtu mzuri, sivyo? Mm,  kuna  kitu  fulani  kuhusu  Betty  ambacho  sharti  ukijue: Anapokuwa  hayupo  marafiki  zake  humwita  “Betty-Yule  Mbaya” Wanahisi  vibaya  juu  ya  jina  hilo  alilobandikwa,  lakini  pasipo kumwonea,  Betty  alijitafutia  jina  hilo;  ana  namna  ya  kutarajia, kutabiri,  na  kutafuta  yale  mabaya  zaidi  katika  kila  hali.  Nitawapa mfano. Majira ya kiangazi yaliyopita,  Betty  na mumewe (Phil  Ambaye Hufanikiwa)  walienda  likizoni  pamoja  na  watoto  wao  wawili  (Will Ambaye  Hatafaulu  Vile  na Pack Megan Aliye  Katikati).  Sasa, lazima niwaambie kwamba Phil  ni mume mzuri anayempenda mkewe  na  Will  na  Megan  ni  watoto  wazuri  sana,  lakini  Betty  hana matumaini  makubwa juu yao. Hatarajii  mambo mengi  kutoka kwao pia.  Kusema  kweli, kwa kiasi fulani  anatazamia  mabaya, sawa na majina waliyobandikwa..
Miezi  kadhaa  iliyotangulia,  Phil  na  Betty  walipanga  kusafiri na  kwenda  likizo ya  wiki  nzima mahali  mashuhuri  kwa ajili  ya mapumziko,  lakini  safari  ilipokaribia,  Betty  alifahamu  fika  kwamba mambo hayatakwenda  vizuri.  Walipokuwa  njiani  wakiendesha  gari umbali  wa  maili  300  kuelekea  mahali  pa  likizo,  Betty  muda  wote alikuwa  akilalamika  na  kusema,  “Wazo  la  kwenda  likizo  halikuwa zuri.”  Sehemu za kufanyia chochote  katika bustani zitakuwa na foleni ndefu ya maili moja. Siamini ikiwa  hoteli  tutakayolala  itakuwa nzuri kama ilivyotangazwa. Mvua itanyesha wiki  nzima.”  Phil  na watoto walijaribu kumhakikishia Betty kwamba kila kitu kitakwenda vizuri—wanaweza  kutumia  vizuri  hali  yoyote  itakayotokea—lakini hali  ya Betty  ya  kuona kila kitu kuwa giza  haikuweza  kuondoka. Maskini  Phil,  Will,  na  Megan  ...waliuona  mwendo  huo  wa  maili 300- kwa gari ukiwa kama maili  1,000 za kuchosha sana. Kwa kweli  mambo yalikwenda  sawa na matarajio ya   Betty.

Foleni  za  bustani  ya  maji  zilikuwa  ndefu  kuliko  kawaida.  Phil,  Will, na  Megan  hawakujali—hali  hii  iliwapa  muda  zaidi  wa  kucheka pamoja  na  kupanga  watakuwa  kwenye  msafara  wa  ngapi—lakini  Betty  alikuwa  amekasirika  sana.
Alinong’ona  na  kusema,  “Nilijua tu haya yangetokea.” Ule  mkahawa waliochagua kwenda kula chakula cha jioni usiku  ule wa kwanza  vile vile haukuwa  mzuri.  Mhudumu wa kike alimweleza  Phil  na Betty  kwamba vinywaji laini walivyokuwa wameagiza  vilikuwa  vimeisha.  Phil  aliagiza  kinywaji  kingine;  Betty yeye akachagua kununa tu. Akaguna na kusema, “Ajabu hii!” Lakini  kitu  kilichowaudhi  zaidi  ni  kile  walichokiona  walipoingia katika  chumba  chao  cha  hoteli.  Walipoingia  chumbani  mwao  ili walale, waligundua kwamba TV ilikuwa haifanyi  kazi  vizuri.  Betty alilalamika  tena  na  kusema,  “Nilijua  tu!”  Nilijua!  Nilijua!  “Nilijua hii hoteli  si nzuri kamwe.” Phil  aliwaita  wahudumu wa sehemu ya  mapokezi, na mafundi wakaja mara  moja na televisheni  mpya, lakini tayari mambo yalikuwa yameharibika. Betty  Mbaya alikuwa na likizo mbaya...hivyo ndivyo alivyotarajia haswa.

Swala la Moyo Kisa  cha Betty ni cha kubuni tu na kinahusu  mtu ambaye kwa  kiasi fulani  anafanana  na  mimi na  wewe  wakati  mwingine. Tumejikuta tukipambana na hali ya kutoona mafanikio na kutokuwa na matarajio  makubwa—tukiiona  hali  ya  hewa  kuwa    “ya  mawingu kiasi”  badala  ya kuiona  kuwa yenye “jua kiasi,”  tukiiona  glasi ikiwa “tupu nusu” badala ya kuiona  “imejaa nusu.” Kwa Betty, matarajio  yake  madogo  yalimzuia  kufurahia likizo yake  ya  wakati  wa  kiangazi, lakini kwa watu  wengi,  matarajio madogo  huwazuia  kufurahia  maisha  yao.  Wanaishi  kila  siku  huku wakiwa na mitazamo hasi, ya kutafuta  makosa,  kukosoa  kila kitu, na ni  nadra sana kwao  kutarajia  mema kwa  sababu wanajishughulisha sana  kutarajia  mabaya  zaidi.  Wakati  mambo  hayaendi  vizuri wanajisemea  Nilihisi  leo itakuwa  siku  mbaya,  mambo yanapokwenda vizuri  wanasema  Yamkini hii  haitadumu  kwa muda mrefu.  Siku iwe njema  au  mbaya,  wawe  juu mlimani au  bondeni,  hawafurahii maisha yao...  kwa sababu hawakutarajia  watayafurahia.  Huenda mimi  na wewe si  wabaya kama Betty, lakini kusema  kweli,  kiwango chochote  cha  kukosa  matumaini  kina athari  kubwa maishani mwetu.  Kwa nini wasiamini mema na wafungue  mlango waone mambo ambayo Mungu anaweza kuwafanyia? Matarajio  madogo ni zaidi ya malalamiko kidogo ya siku  ndefu ya Jumatatu  au  kuhisi  pengine  umeamka vibaya.  Matarajio  madogo ni dalili ya tatizo kubwa zaidi, tatizo la  kiroho.  Mtu anaweza  kuwa na historia  ya  kuvunjwa moyo iliyomfanya  awe  na mazoea  ya  kutarajia mambo  kama  hayo  zaidi  kila  wakati.  Watu  wengine  wana  kiwango cha chini cha kujistahi kiasi kwamba wanajiona  kuwa hawafai kuwa  na  kitu  chochote  kizuri,  hivyo  hawatarajii  chochote. 

Na  kisha kuna wale  watu  wengine  ambao  hawajui Mungu ni mwema  na anataka  kuwatendea  mema wanawe. Hatari  zinazotokana na dalili hizi kubwa. Kama  tungeeleza  yale  yanayoendelea  katika  nafsi zetu kama ambavyo tunaeleza  ugonjwa wa mwili, basi ingekuwa kama hivi:

Daktari:  Kwa hiyo, unasema husikii  vizuri  kiroho na kimwili. Tafadhali niambie dalili za ugonjwa wako.

Mgonjwa:  Mmm,  Daktari, ninahisi  vibaya kuhusu  siku  za usoni.  Nimevunjwa  moyo  mara  nyingi  maishani  mwangu, na sitarajii ikiwa  mambo  yataniendea  vizuri  au hata familia yangu.

Daktari: Dalili  zako zinaniambia kila kitu ninachopaswa kujua. Una tatizo kubwa la ukosefu wa matumaini.

Dalili  za Betty  zilikuwa kuona kila kitu ni kibaya, wasiwasi, na  kulalamika.  Dalili  hizi  zilisababishwa  na  tatizo  la  moyo  wake: ukosefu wa matumaini.  Badala  ya  kutarajia  likizo nzuri ya  familia, Betty  alitarajia mambo  mabaya sana. Foleni zitakuwa ndefu.
Hatutapata mkahawa  mzuri. Hoteli  itakuwa  mbaya  sana.  Hakuna matumaini yoyote  katika  mawazo  kama  hayo.  Hata  hivyo,  Phil,  Will,  na Megan  walionyesha  dalili  tofauti.  Walikuwa  na  mtazamo  chanya, walisisimka,  wakafurahi, na walikuwa tayari  kukabiliana  vizuri na hali  yoyote.  Walijaa  matumaini,  na  matarajio  yao  yalikuwa  ya  juu sana. Ni  muhimu kutambua kwamba mazingira yalikuwa yale yale kwa Betty  na familia yake, lakini  jinsi  walivyoyapokea  mazingira hayo ni  tofauti.  Wote  walisimama  kwenye  foleni  ndefu;  wote  walikula kwenye  mkahawa  mmoja;  wote  walikaa  chini  mbele  ya  televisheni iliyoharibika. Mambo haya yalipotokea,  matarajio  madogo ya Betty  yalithibitishwa,  hali  iliyomfanya  atake  kukata  tamaa.

Kwa wengine  katika familia  hiyo, matarajio  yao makubwa yalikumbwa na changamoto, lakini wakachagua  kuendelea  kuwa  na matumaini na furaha,  jambo lililowawezesha kupata  njia za kukabiliana na mazingira hayo na kusonga mbele, huku  wakifurahia kila hatua  ya mwendo wao. Basi  ukiwa  na  taswira  hiyo,  ningependa  nikuulize  swali  muhimu: Dalili zako  ni zipi? Kama ungeuchunguza vizuri moyo wako, je, ungeona nini ndani yako? Je,  wewe  ni    kama  Phil,  Will,  na  Megan?  Waliosisimshwa  na mambo  yaliyokuwa  mbele yao, wakitarajia  leo iwe siku  nzuri  zaidi kushinda  jana  na  kesho  iwe  siku nzuri zaidi kuliko leo?
 Je, huwa  unaamka kila asubuhi ukiwa  na  furaha  na  matarajio kwamba Mungu anaenda kutenda  kitu cha ajabu mashani mwako? Au wewe ni  kama  Betty  Mbaya? Je, huwa unajikuta  unajiandaa  kukabiliana na mambo mabaya? Je, huwa  una wasiwasi  wa mambo mabaya kutokea hata  kabla  hayajatokea?  Je, huwa unatumia  maneno kama  ndiyo  haya  tena,  hili  halitafaulu  kamwe, natamani  ningejua  kwamba  mambo  yatatumbukia nyongo,  na  ninahisi  vibaya juu ya jambo hili? Je, huwa unaamka kila asubuhi ukiwa na furaha na matarajio kwamba Mungu anaenda kutenda kitu cha ajabu maishani mwako? Kuunganika kwa Imani Kuitathmini mioyo yetu  ni shughuli  muhimu wakati  tunapoanza safari hii ya matumaini pamoja, kwa  sababu kumtumaini Mungu na kuwa  na  matarajio  mazuri yana  uhusiano wa karibu sana na imani.  Kwa sababu ya  majadiliano, tunaweza kusema kwa urahisi kwamba  kiwango cha matarajio yako ndicho kiwango  cha imani yako.   Nionyeshe  mtu  mwenye  matarajio madogo, nami nitakuonuyesha mtu anayetumia  imani  haba.  Lakini  nionyeshe mtu  mwenye  matarajio  makubwa, na nitakuonyesha mtu  anayetumia  imani ya  kijasiri. Kumbuka tunaongea  kuhusu kuwa na matarajio  yetu  katika  Mungu. Hilo ni zaidi ya  kuwa na mtazamo  chanya;  ni  kumtegemea  Mungu  akutunze  na  atunze  kila kitu kinachokuhusu wewe. Neno  la  Mungu  linatwambia  kwamba  imani  yetu— matarajio  yetu  chanya,  yenye  matumaini—humpendeza  Mungu  (Waebrania  11:6),  na  mara  kadhaa  katika  Injili,  tunamuona  Yesu akichochewa kutenda jambo kwa sababu ya imani—na matarajio— ya  wale  aliokutana  nao  (Mathayo  9:29,  Marko  5:34,  Luka  7:50 na  Luka  17:19).  Mmoja  wa  miujiza  kama  hiyo  unapatikana  katika Marko  sura  ya  10.  Ninaipenda  hadithi  hii,  na  nafikiri  ina  umuhimu mkubwa  kwako  na kwangu leo  kwa sababu inahusu umuhimu wa matarajio. Marko 10: 46–47 inasema: ...
[Yesu] alipokuwa akiondoka kutoka Yeriko, pamoja na wanafunzi wake, na mkutano  mkubwa, mwana  wa Timayo, Bartimayo, yule mwombaji kipofu, alikuwa  ameketi kando ya njia. Naye  aliposikia ya  kwamba  ni  Yesu  Mnazareti,  alianza  kupaza  sauti  yake,  na kusema, Mwana wa Daudi, Yesu, unirehemu.

Unapofikiria juu ya tukio hilo, utaona kwamba Bartimayo alikuwa na sababu za kutosha za kutarajia  mabaya zaidi. Alikuwa ni kipofu mwombaji aliyekaa kando ya njia kila siku,  akijaribu kuwaomba watu  wampe pesa.

Alikuwa anaishi maisha magumu sana, na ikiwa kuna  mtu ambaye angeshusha  chini  matarajio  yake, basi angekuwa ni  Bartimayo.  Angefikiria  na  kusema  Hii  haina  maana  yoyote.  Haiwezi kufaulu.  Hakuna  kitu kitakachobadilika.  Yamkini  Yesu hata  hataniona.  Kwa nini niwe na matumaini?  Hakuna mtu ambaye angemlaumu. Lakini  Bartimayo  alithubutu  kutarajia  kitu  kizuri  zaidi  katika maisha.  Alianza  kufikiria  juu  ya  kile  ambacho  huenda  kingetokea badala  ya  kufikiria  kile  ambacho  huenda  kisingetokea.  Hakuna kitu  “kilichoshushwa  chini”  kuhusu  kiwango  chake cha matarajio wakati  alipoanza  kupaza sauti  kwa nguvu zake zote, “Mwana wa Daudi,  Yesu,  unirehemu! 

Je,  unaweza  kusikia  msisitizo  huo  katika sauti  yake?  Ni  kana  kwamba  Bartimayo  alikuwa  ameamua  kwa vyovyote  hatakosa fursa hii. Ijapokuwa wengi  waliokuwa katika kundi  lile  la  watu  “walimkemea  ili  anyamaze”  (Marko  10:48), Bartimayo hakukubali kunyamazishwa. Alipaza  sauti  zaidi na zaidi hadi Yesu akasimama na kumwita. Hii  hapa  ni  moja  ya  sehemu  za  ajabu  za  hadithi  hii:  Bartimayo alipoletwa  kwa  Yesu,  Bwana  alimuuliza  swali  ambalo  huwezi  hata kudhani  angeulizwa.  Katika  kifungu  cha  51,  Yesu  alimuuliza  yule kipofu mwombaji, “Wataka nikufanyie nini?” Hilo linaonekana kuwa swali  la ajabu, sivyo? Huenda wanafunzi walikuwa wanajisemea  “Wataka  nikufanyie nini?” Bwana,  si  ni wazi kabisa?  Huyu bwana ni kipofu.  Unawezaje kumuuliza swali kama hilo? Lakini Yesu  alikuwa  anauliza  swali  la  kina  zaidi—Alikuwa  anamuuliza Bartimayo:  Unatarajia  nini?  Je, unatarajia  chakula?  Je, unataka  akushike mkono na kukuelekeza? Je, unatarajia  kupewa kitu?  Mambo hayo yote bila shaka  yalikuwa mambo ambayo Bartimayo alihitaji, na kama angekuwa na imani haba, angetosheka na kimoja cha vitu hivyo. Lakini  Bartimayo  alikuwa  na  kiwango  cha  juu  cha  matarajio. Yesu  alipomuuliza,  “Wataka  nikufanyie  nini?”  Bartimayo  hakusita, hakuwa  na  haja  ya  kuanza  kufikiria  juu  ya  jambo  hilo,  hakushangaa endapo anaomba zaidi ya ipasavyo. Bartimayo alisema kwa  ujasiri, “Mwalimu wangu, nataka nipate  kuona.”  Yamkini  unajua sehemu ya  hadithi  hii  iliyobaki.  Yesu  aliguswa  sana  na  imani  ya  Bartimayo. Kifungu  cha  52  kinasema:    “Yesu  akamwambia,  Nenda  zako,  imani yako imekuponya.

Mara akapata kuona; Akamfuata njiani.” Kwa kuwa Bartimayo alikuwa jasiri kuamini kwamba  atapokea mema  zaidi kutoka kwa Mungu, hivyo  ndivyo  haswa alivyopokea kutoka kwa  Bwana. Hivyo ndivyo ilivyo hata katika  maisha  yako, na hivyo kiwango chako cha matarajio  ni muhimu sana kwa aina ya  maisha utakayoishi. Ikiwa hutarajii  Mungu atende  jambo lolote  kubwa  maishani  mwako,  basi  hatatenda.  Lakini  ukithubutu kupandisha  kiwango chako cha matarajio  na kuanza kutarajia kwamba  Mungu anataka kutenda kitu kizuri katika  maisha yako,  utaanza  kuwa na ndoto, amini, omba, na utende  kwa ujasiri uhodari, huku  ukijua Mungu yuko upande  wako na ana mpango mzuri kwa maisha yako. Kama unauliza ikiwa inakubalika kwa wewe  kutarajia  mambo mazuri kutoka kwa Mungu, tafadhali  soma pole  pole  na utafakari Maandiko haya katika Isaya.

Kwa ajili  ya hayo BWANA atangoja  [kwa bidii],  [akitarajia, akitazamia  na akitamani]  ili awaonee huruma, na kwa ajili ya  hayo atatukuzwa,  ili  awarehemu. Kwa  maana  BWANA  ni Mungu wa  hukumu. Heri  (wana  furaha,  wana  bahati,  wanaweza kuonewa  wivu) wote wamngojao  [kwa bidii],  wanaotarajia na kutazamia  na kumtamani [kwa ushindi  wake, kibali  chake, upendo wake, amani  yake, furaha  yake, na uwepo  wake usio  na kifani, na usioweza kuharibibwa]! Isaya 30:18 Mungu anawatafuta  wale  ambao  anaweza  kuwatendea  mema, na ikiwa unamtafuta  (unamtarajia)  Mungu akutendee  mema, basi unafaa. Mtarajie  Mungu ajitoe  kwako  kwa  sababu yeye ni muhimu kuliko  kitu chochote  kile, lakini kumbuka yeye  ndiye  mwenye mambo mengine yote tunayohitaji. Hatua Tatu Za Kuinua Kiwango Cha Matarajio Yako Huenda  unasoma  sura  hii  na  kufikiria  Joyce, hayo unayosema  ni mazuri sana,  lakini ninapaswa kutarajia mengi  zaidi   kwa njia gani? Ninaharakisha kuhudhuria  mkutano  mmoja  hadi  mwingine,  naona  vigumu kulipa  madeni yangu,  najaribu  kuwalisha  watoto  au  kuendesha  kampuni  ili  isifilisike.  Maisha yangu  yote  nimekuwa  nikifanya  kazi  kwa  bidii  kadri  ya  uwezo  wangu  kufikia hapa  nilipo.

Ninawezaje kuongeza kiwango changu cha matarajio? Ninaweza  kusema  mengi  sana  juu  ya  imani—maelfu  na  maelfu ya  vitabu  vimeandikwa  juu  ya  mada  hii—lakini  ningependa kukupatia  hatua  tatu  rahisi zinazoweza  kukuwezesha kuanza leo. Hatua  hizi tatu  zitakusaidia kupandisha  kiwango  chako cha matarajio:

1.  Amini. Kuna sababu inayofanya wana wa Mungu waitwe “waamini.” Unapojaribiwa  kuwa na  mashaka, unapojaribiwa kukata tamaa,  unapojaribiwa kufa moyo, chagua kuamini.      Kuamini ndio msingi wa imani yako.
Amini.  Neno  la  Mungu.  Amini kwamba ahadi zake, ni za kweli.   Amini anakupenda, na amini ana kitu kizuri kwa  ajili  ya  maisha  yako.  Yesu  alisema Unapojaribiwa kuwa na mashaka, unapojaribiwa kukata tamaa unapojaribiwa kufa  moyo, chagua kuamini. ikiwa tungeamini tu,  basi tungeona  utukufu  wa  Mungu (Yohana  11:40).  Utukufu  ndio  dhihirisho  la  uzuri  wote  wa Mungu.

2.  Omba. Yakobo  4:2  inasema:  “Hamna  kitu  kwa  kuwa  hamwombi.” Utakapochagua  kuamini  kuwa Mungu anaweza  kukimu  kila hitaji  maishani mwako, basi endelea  mbele  na umwombe Mungu akimu mahitaji  hayo. Mshirikishe  ndoto zako. Kama vile  Yesu  alivyomuuliza  Bartimayo,  “Wataka  nikufanyie  nini?” Anakuuliza swali hilo  hilo.  Kuwa  na  ujasiri  wa kumwomba Bwana afanye kitu ambacho yeye peke yake ndiye anayeweza kukifanya. Bila shaka,  sote  tunapaswa kutaka Mungu atende mapenzi yake na tuamini kwamba ikiwa kile tunachomwomba si  kitu kizuri  kwetu,  basi  Mungu hatatupatia lakini badala yake atatupatia kitu kizuri zaidi.

3.  Tazama. Unapoishi  kila siku,  tarajia  kwamba  Mungu  anajibu maombi yako, anakimu mahitaji yako, na kutimiza ndoto aliyokupa Mungu. Hata  ikiwa bado hujaona dhihirisho la  yale unayotamani, au ikiwa  hayajatokea  kama ulivyotarajia,  hiyo haimaanishi  kwamba  Mungu  hafanyi  kazi.  Endelea  kuwa  na mtazamo wa matarajio, na uhakikishe  unatambua kila kitu anachofanya  Mungu. Shukuru kwa ajili  ya  mambo hayo huku ukisubiri kitu unachotamani au kuhitaji sasa hivi. Chochote  unachokitarajia  leo—kuwa  karibu  zaidi  na Mungu,  kulielewa  Neno  la  Mungu  vizuri  zaidi,  kuwa  na ndoa nzuri, kufanikiwa  kifedha,  fursa ya kuongeza kiwango cha  elimu,  nafasi  ya  huduma,  mwanzo  mpya—ikiwa  yako moyoni  mwako  (na  ikiwa  yanaendana  na  Neno  la  Mungu), amini, omba, tarajia, na tazama.
Imeandaliwa na Mtumishi Jimmy J.


No comments:

Post a Comment