- Nafikiri ni salama kusema kwamba vingi ya vile ambavyo ulimwengu hutoa havina ladha…na sizungumzi kuhusu chakula. Kwa mfano, nyingi ya sinema zinazotayarishiwa Hollywood hazina ladha. Maongezi mengi na picha hazina ladha nzuri. Mara nyingi wakati tunapoona tabia yoyote isiyofaa tunakimbilia “kuulaumu ulimwengu.” Twaweza kusema kitu kama “Ulimwengu unakwenda wapi?” Ilhali neno “Ulimwengu linamaanisha watu wanaoishi ulimwenguni.
Ikiwa ulimwengu hauna ladha, ni kwa sababu watu wamekosa ladha katika fikra zao na matendo. Yesu alisema kwamba sisi ni chumvi ya ulimwengu, lakini ikiwa chumvi imepoteza ladha yake (nguvu yake na ubora wake), haifai (angalia MAT. 5:13). Pia alisema kwamba sisi ni nuru ya ulimwengu na hatupaswi kuifunika nuru yetu (angalia MAT. 5:14).
Hebu fikiria hivi: Kila siku unapoondoka nyumbani kwako kwenda gizani, ulimwengu usio na ladha, je, unaweza kuwa nuru na ladha inayohitajika? Unewaza kuleta furaha kazini pako kwa kujitolea kuwa na fikra za kiungu. Kupitia mambo madogo kama vile kuonyesha shukurani badala ya kulalamika kama vile ambavyo watu wengi hufanya, kuwa mvumilivu, mwenye huruma, kusamehe haraka makosa, kuwa mkarimu, na kuwa mtu wa kuwatia moyo wengine.
Hata kuonyesha tabasamu kiasi na kuwa na urafiki ni njia ya kuleta ladha nzuri katika jamii iliyokosa ladha. Sijui kuhusu wewe, lakini mimi sipendi chakula kisichovuti Rafiki yangu alikuwa na tatizo la tumbo wakati fulani na daktari akamshauri atumie chakula kisicho na ladha nzuri kwa siku chache. Kama ninavyo kumbuka, wakati huo hakutaka kula chakula. Ingawa yeye si mtu anayependa kulalamika, lakini katika kila mlo, nilimsikia akisema kila mara, “Chakula hiki hakina ladha kabisa.” Kilihitaji chumvi kidogo, viungo kiasi... na hivyo ndivyo ulimwengu unavyohitaji.
Bila upendo na ubora wake wote, maisha hayana ladha na hayastahili mtu kuishi. Nataka wewe uyajaribu. Hebu fikiria: Ninaenda katika ulimwengu leo na kurekebisha mambo. Kisha jipange akilini mwako kabla ya kutoka kwenye mlango wako kwamba unaenda nje kama balozi wa Mungu na kwamba lengo lako ni kuwa mtoaji, kuwapenda watu unaokutana nao siku nzima. Tabasamu ni ishara ya kukubaliwa na kuidhinishwa jambo ambalo watu wengi ulimwenguni wanahitaji.
Jiweke akiba kwa Mungu na umwamini ili akulinde unapopanda mbegu nzuri kila mahali uendako kwa kufanya maamuzi yatakayokuwa baraka kwa wengine. Mabadiliko Huanza na Wewe Ninatambua kwamba huwezi kufanya kila kitu; Sidadisi jambo hili kabisa. Ni lazima ukatae mambo fulani ama sivyo maisha yako yatajaa mambo mengi na kukufanya kuwa mchovu wa akili kila mara.
Siwezi kujitolea kuwapa mafunzo watoto au kuwapa mlo wakongwe, lakini ninafanya mambo mengine mengi ili kuleta tofauti ifaayo ulimwenguni. Nafikiri swali ambalo kila mmoja wetu lazima ajibu ni, “Ni nini nitakachomfanyia mtu mwingine ili awe na maisha bora?” Na pengine swali bora zaidi ni, Nimefanya nini leo kumfanya mtu mwingine aishi maisha bora?” Somo hili huenda likawa gumu kukisoma wakati mwingine kwa sababu natumai kitaleta maswali yenye utata. Lakini yanahitaji kushughulikiwa na kila mmoja wetu. Hakuna kizuri kinachotendeka kiajali. Ikiwa twataka kuwa sehemu ya Mageuzi, inamaanisha kuwa mambo lazima yabadilike, na mambo hayawezi kubadilika hadi pale watu watakapoyabadili. Kila mmoja wetu lazima aseme: Mabadiliko yanaanza na mimi!.
No comments:
Post a Comment