Thursday, 31 May 2018

Hakuna Mwanaume ambaye ni Kisiwa

Nina hakika  umesikia  mstari maarufu  wa maneno  yaliyosemwa na  John Donne,  kwamba  “hakuna  mwanaume ambaye ni kisiwa.” Maneno haya ni njia ya kueleza ukweli kwamba watu wanahitajiana, yaani kila mmoja anamhitaji mwingine  na kumuathiri  mwingine kwa njia nzuri  au mbaya.  Kama vile  ambavyo maisha ya  ya huyu yaliniathiri mimi  kwa  njia mbaya  na  maisha  ya  Huyu yakaniathiri kwa  njia nzuri, maisha yetu yanaweza  kuwaathiri watu wengine.

Yesu  alituambia tupendane  kwa  sababu hiyo ndiyo njia pekee  ya ulimwengu kufahamu kuwepo kwake (angalia Yohana  13:34-35). “Amri  mpya  nawapa,  Mpendane.  Kama  vile nilivyowapenda  ninyi, nanyi mpendane vivyo hivyo. Hivyo watu wote  watatambua ya kuwa  ninyi  mmekuwa wanafunzi wangu,  mkiwa na upendo  ninyi kwa ninyi.”   Mungu  ni  upendo, na wakati tunapoonyesha upendo katika  maneno yetu na  vitendo,  tunawaonyesha  watu vile Mungu alivyo. Paulo alisema kwamba  sisi  ni  mablozi wa Mungu, waakilishi Wake, na kwamba Yeye Anauhimiza ulimwengu kupitia sisi (angalia 2 KOR 5:20).



Kila wakati ninapofikiria juu ya  maandiko  haya  mimi husema, “Kumbe! Hii ni nafasi kuu na wajibu mkuu.” Kati ya masomo niliyojifunza maishani ni  kwamba singepata nafasi  bila ya  kuwajibika.  Hiyo  ndiyo  moja  ya  matatizo  katika  jamii yetu hivi  leo. Watu wanataka  kile  ambacho  hawanuii kuwa nacho! Uchoyo unasema,  “Nipe mimi. Ninataka  na ninataka  sasa.”Hekima yasema,  “Usinipe  mimi kitu chochote;  sijakomaa  vya  kutosha kukisimamia.”

Ulimwengu kwa  kiwango  kikubwa  hauna  shukurani na,  hivyo ni  kwa  sababu hatutaki tena kusubiri  au kujitolea kwa  chochote. Nimegundua kwamba  mambo niliyo na shukurani nayo ni  yale ambayo nimeyafanyia  bidii   na kusubiri  kwa  muda mrefu.  Mambo tunayopata  kwa  urahisi kwa  kawaida  huwa  hayana  thamani  kubwa kwetu....

No comments:

Post a Comment