Unaposoma kitabu cha Zaburi, moja ya mambo ya kwanza utakayoona ni kwamba Daudi alikuwa mtu aliyejaa matumaini na matarajio. Unaweza kuyasikia haya katika mashairi yake aliyoandika. Hii hapa mifano michache: Iweni hodari, na mpige moyo konde, Ninyi nyote mnaomngoja BWANA! Zaburi 31:24 (imeongezwa msisitizo) Naam, wakungojao hawataaibika hata mmoja... Zaburi 25:3 (imeongezwa msisitizo) Na sasa, ninangoja nini na kutarajia nini, Ee Bwana? Matumaini yangu ni kwako. Zaburi 39:7 (imeongezwa msisitizo)
Iwe alikuwa anachunga kondoo kondeni, au kuongoza kikosi cha askari wasaliti, au kutawala kama mfalme wa Israeli, wakati wote Daudi aliishi akiwa na matumaini kwamba Mungu alikuwa anaenda kutenda kitu cha ajabu maishani mwake. Lakini matumaini ya Daudi hayakumruhusu akae tu bila kufanya kitu chochote. Ukweli ni kwamba, kufanya kitu ndiyo sawa. Matumaini yake yalimchochea awe mtendaji. Daudi aliamini kwamba Mungu alikuwa atatenda kitu cha miujiza, lakini alijua kwamba ana ubia na Mungu na kwamba alihitaji kutii kikamilifu.
Hivyo tunamwona Daudi akimwomba Mungu amwonyeshe njia na kisha kuchukua hatua za imani kwa ujasiri (1 Mambo ya Nyakati 14:10, 1 Mambo ya Nyakati 14:14, 1 Samweli 23:2, 2 Samweli 2:1). Hebu fikira ikiwa Daudi angekaa tu, bila ari, na kukosa nidhamu wakathi alipokabiliana na Goliathi? Mfikirie Daudi akijisemea Mmm, natumaini Mungu ana kitu. Nitakaa hapa tu kwenye mitaro pamoja na hawa wenzangu. Iwe alikuwa anachunga kondoo kondeni, au kuongoza kikosi cha askari wasaliti, au kutawala kama mfalme wa Israeli, wakati wote Daudi aliishi akiwa na matumaini kwamba Mungu alikuwa anaenda kutenda kitu cha ajabu maishani mwake. Lakini matumaini ya Daudi hayakumruhusu akae tu bila kufanya kitu chochote. Ukweli ni kwamba, kufanya kitu ndiyo sawa. Matumaini yake yalimchochea awe mtendaji. Daudi aliamini kwamba Mungu alikuwa atatenda kitu cha miujiza, lakini alijua kwamba ana ubia na Mungu na kwamba alihitaji kutii kikamilifu.
Tuwe na matumaini kwamba Mungu atatuma radi na kuliua hili jitu. Ikiwa angekuwa na mtazamo huo, Mungu angemtumia mtu mwingine kumshinda Goliathi. Mungu alikuwa anatafuta mtu ambaye angekuwa tayari kutekeleza sehemu yake—mtu ambaye matumaini yake yangemchochea kutenda jambo. Daudi alikuwa ndiye mtu huyo! Daudi alipojitokeza mstari wa mbele kuwaletea ndugu zake mahitaji yao, na kusikia lile jitu la Kifilisti likimtukana Mungu na kudhihaki majeshi ya Israeli, hapo hapo, alijawa na matumaini. Aliwauliza wale waliokuwa karibu naye, “Je! Atafanyiwaje yeye atakayemwua Mfilisti huyo, na kuwaondolea Israeli aibu hii?” (1 Samweli 17:26).
Hakuwa anawaza kuhusu kushindwa; hakuwa anawaza kuhusu kutofaulu; hakuwa anawaza yale magumu yaliyokuwa yanawakabili—alikuwa na matumaini kwamba angefaulu na kwamba angevishinda vita hivyo.Matumaini hayo yalimfanya Daudi atende jambo. Kati ya wakati ule alipohisi kuwa na matumaini na wakati ule ushindi ulipopatikana, angalia hatua za utendaji alizozichukua: Daudi alipinga ukosoaji kutoka kwa kaka yake aliyejaribu kumdunisha na kumvunja moyo (kif. 28-30); alimshawishi Mfalme Sauli amruhusu kwenda kupiga vita (kif. 32-37); alijaribu kuvaa silaha za Sauli lakini akaamua kutozitumia (kif. 38-39); alichagua mawe matano kama risasi za kombeo lake (kif. 40); alimdharau Goliathi, na akatabiri ushindi (kif. 45-47); na akakimbia kwenda vitani (kif. 48).
Daudi hakuwa na mtazamo wa Mmm, natumai mambo yatakwenda vizuri. Hebu natusubiri tuone. Alikuwa na mtazamo wa Matumaini yangu ni katika Mungu. Natwende tukashinde vita hivi! Daudi hakuturoka vita au kujificha kama walivyofanya wale askari; alikimbia kwenda vitani akiwa amejaa matumaini na imani kwamba Mungu angempa ushindi dhidi ya lile jitu. Daudi alikuwa na matarajio mazuri kwamba kitu kizuri kitatokea!
No comments:
Post a Comment