Monday, 18 June 2018

Usimzunishe Roho Mtakatifu

Twaweza kumfanya Roho Mtakatifu  ahisi kuhuzunika  kupitia hasira  yetu, kupandwa  na  ghadhabu, kutosamehe,  uchungu, kubishana, na wasi wasi. Biblia inatuhimiza tuwache  mambo mabaya  ya  aina  yoyote.  Inanihuzunisha kufikiria kwamba ninaweza  kumhuzunisha  Roho  Mtakatifu wa  Mungu. Wakati ninapokumbuka jinsi  nilivyokasirika  kwa  urahisi wakati fulani, najua nilimhuzunisha, na sitaki kufanya hivyo tena. Njia pekee ninayoweza  kujiepusha  na  jambo  hili ni kuwa  mkakamavu kuhusu kuachilia hisia mbaya nilizo  nazo  kwa  wengine  mara tu zinaponijia.

Twapaswa  kuwa  watu wenye manufaa,  wa  kusaidia,  na kuwa wakarimu  kwa  wengine, kusameheana na kuwa  huru kama  Mungu katika Kristo alivyotusamehe  (angalia     EFE  4:30-32). “Wala msimhuzunishe  yule  Roho Mtakatifu  wa Mungu;  ambaye kwa  yeye mlitiwa muhuri hata  siku ya  ukombozi. Uchungu wote na ghadhabu na hasira na kelele  na matukano yaondoke kwenu, pamoja  na kila namna ya  ubaya;  tena iweni  wafadhili ninyi  kwa ninyi,  wenye huruma, mkasameheane kama  na  Mungu katika Kristo alivyowasamehe ninyi.” Hasira  yetu humfanya  Roho  Mtakatifu kuhuzunika sio tu kwa  sababu Mungu anatutaka  tupendane  bali kwa  sababu najua inavyotuathiri, na  anataka  tufurahie maisha  ya  uhuru.

Twapaswa kumuiga Mungu na kufuata mfano wake. Yeye si  mwepesi   wa hasira,  ni  mwingi wa  rehema, na husamehe  haraka.  Hasira yetu haiimarishi usafi anaotutaka  Mungu tukae ndani yake. Kama  vile upendo halisi haujalishi jinsi tunavyohisi,  msamaha  wa  kweli pia haujali hisia. Mambo yote haya mawili  yanategemea uamuzi tunaofanya, sio hisia tulizo nazo. Nimejifunza  kwamba  ikiwa nimechagua  kusamehe, hisia zangu  hatimaye zitafuata  uamuzi niliofanya. 

Kuwasamehe wengine  huniwezesha kuongea  nao kuliko kuwanyamazia  na  kuwafungia  nje ya   maisha  yangu.  Huniruhusu kuwaombea  na kuongea baraka  kuwahusu kuliko mambo mabaya, na maovu. Twazingatia sana hisia zetu. Badala  yake, twapaswa kukumbuka kwamba  hisia zetu hubadilika haraka. Kisichobadilika ni upendo.

No comments:

Post a Comment