Kwa sasa hivi, huenda unafikiria, na je, kuhusu mimi? Ni nani atakayenifanyia jambo mimi? Hili ndilo jambo ambalo kwa kawaida hutuzuia sisi kuishi maisha ambayo Mungu anapenda tuishi. Inanirudia “mimi” kila mara. Je, kuhusu mimi, kuhusu mimi? Tumezoea kuona kwamba matarajio yetu yametimizwa, kwamba wazo la kujisahau sisi wenyewe hata siku moja ni la kutisha. Lakini, ikiwa tunaweza kuwa na ujasiri mkuu wa kujaribu, tutashangazwa na uhuru na furaha tutakayopata. Kwa maisha yangu mengi, mimi huamka kila siku na kujilaza kitandani nikifanya mipango yangu.
Nilifikiri juu ya kile nilichotaka na kitakachokuwa bora kwangu na jinsi ninavyoweza kuishawishi familia yangu na marafiki washirikiane nami katika mipango yangu. Niliamka na kumaliza siku nzima nikiwaza akilini mwangu, na kila wakati mambo yalipokuwa hayaendi nilivyotaka, nilikasirika, nilishindwa kuvumilia, nilitatizika na kukasirika sana. Nilifikiri sina raha kwa sababu sikuwa nikipata kile nilichotaka, lakini nilikosa furaha kwa sababu yote nilikuwa nikijaribu ni kupata kile nilichotaka bila kuwajali wengine. Kwa vile sasa nimegundua kuwa siri ya furaha ni katika kuyatoa maisha yangu kuliko kujaribu kuyahifadhi mimi mwenyewe, asubuhi zangu huwa tofauti.
Asubuhi hii, kabla nianze kazi ya kuandika ukurasa huu, niliomba na kisha nikachukua muda wa kufikiria watu wote ninaojua kuwa tutawasiliana nao leo. Kisha nikaomba kupitia Warumi 12:1, “basi, ndugu zangu, nawasihi kwa huruma zake Mungu, itoeni miili yenu iwe dhabihu iliyo hai, takatifu, ya kumpendekeza Mungu, ndiyo ibada yenu yenye maana.” Neno linaloongea kuhusu kujitolea kwetu kwa Mungu kama dhabihu zilizo hai, tutoe uwezo wetu wote wa hali na mali kwake Mola kwa matumizi Yake. Nilipokuwa nikifikiri kuhusu watu nitakaofanya kazi nao ua pengine kuwaona siku ya leo, nilimuuliza Bwana anionyeshe kitu chochote ambacho ninaweza kuwafanyia. Niliweka wazo akilini mwangu niwahimize na niwapongeze. Kwa kweli sote twaweza kupata kitu kizuri cha kumwambia mtu tunayekutana naye. Kujaribu kufanya hivi kutatusaidia kuondoa akili zetu kwenye mawazo ya kujifikiria sisi binafsi. Ninaamini Bwana ataniongoza ninapofanya kazi yangu ya siku ya leo.
Ikiwa unataka kujitoa kwa Mungu ili akutumie kuwapenda na kuwasaidia wengine, ninapendekeza uombe ombi hili. “Bwana, Ninakupa macho yangu, masikio, mdomo, mikono, miguu, moyo, pesa, zawadi, vipawa, uwezo, wakati, na nguvu zangu. Nitumie mimi ewe Bwana, niwe baraka kila mahali niendako siku ya leo.”
Huwezi kujua furaha ya kuishi kama hivi hadi pale utakapojaribu. Ninaiita “tabia takatifu,” na kama tabia zote lazima
itekelezwe kwa vitendo ili iweze kuwa tabia. Siku nyingine huwa ninashikwa na mambo yangu mengi na husahau kutekeleza tabia yangu mpya, lakini ninakumbushwa haraka wakati ninapopoteza furaha yangu na tabasamu ya maisha kwamba kwa mara nyingine nimetoka nje ya mkondo. Nimekuwa nikijaribu kuishi namna hii kwa miaka kadhaa, na yamekuwa ni mapambano. Maisha ya “ubinafsi” yamekita mizizi katika nafsi zetu na hayafi kwa urahisi. Nimesoma vitabu kuhusu upendo, na kusoma tena na tena kile Biblia inachosema kuuhusu na kuomba kuhusu jambo hili. Nimezungumza na marafiki kuuhusu, kuhubiri kuuhusu, na kufanya yote niwezayo kuuhifadhi katika mawazo yangu. Wakati mwingine ninapotambua kwamba nimekuwa mchoyo tena, sikasiriki kwa sababu kujikasirikia kutanifanya nizidi kuwa mimi tu. Ninaposhindwa, Namuuliza Mungu anisamehe na nianze upya; na ninaamini hiyo ndiyo sera bora ifaayo.
itekelezwe kwa vitendo ili iweze kuwa tabia. Siku nyingine huwa ninashikwa na mambo yangu mengi na husahau kutekeleza tabia yangu mpya, lakini ninakumbushwa haraka wakati ninapopoteza furaha yangu na tabasamu ya maisha kwamba kwa mara nyingine nimetoka nje ya mkondo. Nimekuwa nikijaribu kuishi namna hii kwa miaka kadhaa, na yamekuwa ni mapambano. Maisha ya “ubinafsi” yamekita mizizi katika nafsi zetu na hayafi kwa urahisi. Nimesoma vitabu kuhusu upendo, na kusoma tena na tena kile Biblia inachosema kuuhusu na kuomba kuhusu jambo hili. Nimezungumza na marafiki kuuhusu, kuhubiri kuuhusu, na kufanya yote niwezayo kuuhifadhi katika mawazo yangu. Wakati mwingine ninapotambua kwamba nimekuwa mchoyo tena, sikasiriki kwa sababu kujikasirikia kutanifanya nizidi kuwa mimi tu. Ninaposhindwa, Namuuliza Mungu anisamehe na nianze upya; na ninaamini hiyo ndiyo sera bora ifaayo.
Tunapoteza muda mwingi kuhisi vibaya kujihusu kwa makosa tunayofanya na hiyo ni kupoteza wakati.
Ni Mungu pekee anayeweza kutusamehe na yuko tayari kufanya hivyo ikiwa tutamuuliza. Ndio, ninaamini kuwa chanzo cha tatizo ulimwenguni ni uchoyo, lakini inawezekana uishi katika uliwengu huu na ukatae kuwa kama ulimwengu ulivyo. Ikiwa utaungana nami katika kuanza mageuzi ya upendo, ikiwa utabadilika kabisa katika jinsi ulivyokuwa ukiishi na uanze kuishi kwa kupenda kuliko kupendwa, basi unaweza kuwa sehemu ya suluhisho kuliko sehemu ya tatizo. Je, uko tayari kuanza?
No comments:
Post a Comment