Saturday, 30 June 2018

Mavuno Ya Upendo

Kutoa  na  kuishi katika  hali ya  kujitolea kwatoa  mavuno katika maisha yetu. Hakuna makosa ya kutamani na kutarajia mavuno. Motisha yetu  ya kuwasaidia watu wengine  haipaswi kuwa ya kujipatia  kitu fulani  sisi wenyewe, lakini Mungu anatuambia  tutavuna kile  tulichopanda na  tunaweza  kutazamia  manufaa  hayo. Moja  ya  maandiko yanayoelezea  ukweli huu kwa  njia nzuri sana yanapatikana  katika kitabu cha  Luka 6:38; “Wapeni watu vitu, nanyi mtapewa;  kipimo  cha  kujaa  na kushindiliwa,  na kusukwa-sukwa hata  kumwagika,  ndicho watu watakachowapa  vifuani mwenu, Kwa kuwa kipimo kile kile mpimacho ndicho mtakachopimiwa.”(KJV). 

Mungu anaahidi  kuwapa  thawabu wale wamtafutao  kwa  bidii (angalia  EBR 11:6). Neno thawabu katika  maandiko asili ya  Kigiriki ya Agano Jipya,  linamaanisha “ujira unaopokewa katika maisha haya”  au  “fidia.” 

Katika  lugha  ya  kiibrania,  ambayo  Agano  la  Kale iliandikwa, neno thawabu linamaanisha,  “tunda,  mapato,  bidhaa, malipo  au  matokeo.”  Neno thawabu limetumiwa  mara  68  katika Biblia ya  ‘Amplified  Bible’. Mungu anatutaka  tutazamie thawabu za kumuogopa na chaguo zuri. Ikiwa tunawajali wale  ambao  ni  maskini  na walionyanyaswa, Mungu  anaahidi  kwamba “Mwenye  kuwagawia maskini  hatahitaji kitu,  Bali  afichaye  macho  yake  atakuwa  na  laana  nyingi.” (MIT 28:27).  Mwandishi wa  Mithali  hata  anasema  “Amhurumiaye maskini humkopesha  BWANA;  Naye atamlipa  kwa  tendo lake jema”  (angalia  MIT 19:17). Sidhani kuwa  Mungu halipi riba  kuu kwa kile anachokopeshwa. 

Ninakuhimiza ufanye kazi ulete  haki kwa  walioonewa.  Hiyo inamaanisha  kwamba  wakati unapoona  kitu unachojua  kuwa hakiko sawa, unafanya kazi ili kukiweka sawa.

No comments:

Post a Comment