Saturday, 30 June 2018

Fanya Kitu

June Big event  Imefanya kitu,Wakati wengine wakifanya Sherehe kubwa ya kuzaliwa Binafsi,wao waliamua katika siku hiyo maalum kwao watafanya kitu kwaajili ya kusaidia wenye uhitaji na kuleta mageuzi ya Upendo.Wengi wa watu hawaitikii kwa  namna moja.  Kila mmoja anaingiwa  na huruma wakati anapoona  hali ambapo  watu wanaishi  katika  hali mbaya katika  vijiji vya  mashambani nchini Tanzania au  sehemu nyingine  za  ulimwengu. Wengi hulia, na  wengi hutikisa vichwa na  kufikiria hali hizi ni mbaya,  lakini wote  hawaamui  kufanya kitu kubadili hali hizi. Wengi huomba Mungu afanye kitu na wanafurahi  kwamba  huduma ya June Big Event inayoongozwa na Samwel Shan'ga,jimmy John pamoja na Judith Mbondo inafanya  kitu, ilhali hawafikirii kumtafuta Mungu kwa  bidii  kuhusu  kile  wanachoweza  kufanya wao  wenyewe. Ningependa kusema wengi hurejea  nyumbani,  na kujishughulisha  na maisha yao  tena, na mara husahau  kuhusu  kile walichoona. 

  • Lakini namshukuru Mungu kundi la June Big June Event na baadhi  yao  ambao wamejitolea  kutafuta  njia za  kuleta mabadiliko.  Kumbuka:  kutoleta mabadiliko ni  kisingizio, bali upendo  hutafuta njia. Kila  mmoja anaweza kufanya kitu!

Kulala kwenye kochi au kuegemea kwenye kiti maalum kumuuliza Mungu  alinde  kila kitu kinachohitaji  kufanywa  ni  rahisi, lakini inatuwacha  tusiwe na  la  kufanya  na  kutozaa  matunda na  kutuweka wazi  kushambuliwa na muovu. Ikiwa  akili zetu hazina  mawazo mazuri, shetani anaweza kuzijaza  mambo mabaya kwa  urahisi. Ikiwa  tu walegevu na  hatufanyi lolote,  anaweza  kutujaribu kufanya  makosa  na  hata  mambo  machafu. 
June Big Event.
Biblia inatuambia  kila mara tuisome kujikumbusha  na itatuepusha kuwa  walegevu na watu wa  kutozaa  matunda.  Tukifikiria  kwa  bidii  kile  tunachoweza kuwafanyia  watu wengine hakutakuwa  na  nafasi katika  akili zetu ya kuwa na mawazo mabaya. Watu  wasiokuwa  na  lakufanya  huvunjika moyo  kwa  urahisi, hulemewa  kimawazo,  na  kujisikitikia wenyewe.  Wanaweza kuanguka  katika  aina  zote  za  dhambi. Mtume Paulo  hata alisema ikiwa mwanamke aliye  bado kijana amekuwa mjane, anapaswa  kuolewa  tena. Lau  sivyo huenda asiwe na lakufanya na  kuanza  masengenyo  na  kuwa  mdakuzi  wa  mambo  (angalia Timotheo  1 5:11-15). 

Paulo aliendelea  kusema kwamba  baadhi  ya wajane  ambao  bado  wangali vijana  kwa  kutokuwa  na lakufanya tayari walikuwa wameanza kumgeukia shetani. Ina umuhimu gani kuendelea kuwa  imara?  Ninaamini maandiko  ya  Paulo yanathibitisha  kwamba  ni muhimu.  Kwanza,  katika  maandiko Mungu anatuhimiza sisi tusiwe watu wa  kutokuwa  na lakufanya. Nyakati za  Agano  la Kale, wakati mtu alipofariki wana  wa  Israeli waliruhusiwa kuomboleza  mpendwa  wao  kwa  siku  thelathini (angalia  KUM  34:8). Kwanza,  huenda ikaonekana  kuwa  si muhimu, lakini Mungu alifanya  sheria hiyo kwa  sababu alijua kwamba muda  mrefu  wa kuomboleza na kutokuwa na lakufanya unaweza kusababisha matatizo mabaya. Lazima  tukae imara  tusijihusishe  kupita kiasi bali tujihusishe vyakutosha  ili  tuweze kuendelea  katika mwelekeo ufaao. Kujipanga katika  mambo tunayoyafanya  ni muhimu. 

Hatuwezi kutumia muda wetu  wote kusaidia watu wengine, lakini  kwa  upande  mwingine, kutotumia  muda  huo  kulingana  na  mpango  huenda kukasababisha matatizo. Ikiwa  unaweza  kumkumbuka mtu unayemjua asiyekuwa na lakufanya, na ambaye hajishughulishi na jambo lolote pengine pia utatambua kwamba  hawana  furaha  kwa  sababu kutojishughulisha na jambo lolote na kukosa  furaha  mambo haya mawili  huwa pamoja. Miaka  kadhaa  iliyopita  shangazi  yangu  alihitaji kuhamia katika makazi ya kupewa  usaidizi. Kwa  miaka mitatu au minne  ya kwanza  alitaka  kukaa  tu bila kufanya  lolote.  Alihuzunika kwa  vile aliondoka nyumbani  na hakuwa  na nia ya kushiriki  katika maisha mapya  yaliyokuweko.  Ingawa  kulikuwa na  shughuli nyingi   na  hata nafasi za  kusaidia wengine,  hakutaka  kufanya  lolote. Siku baada  ya siku alikaa  tu nyumbani  kwake na alivunjika moyo. Alihisi vibaya mwilini  na  mara  nyingine alikuwa  na  wakati mgumu kukabiliana na hali hii.

Hatimaye alifanya uamuzi kwamba  hangeendelea  kukaa tu  bila kufanya  lolote na  akajihusisha  na  mafunzo  ya  Biblia  na kutembelea  wagonjwa  katika hospitali iliyo karibu na makazi  yake. Alicheza  michezo,  akahudhuria  karamu,  kukutana  na  marafiki wengi. Muda si muda  alikuwa akinieleza  kuwa ana  furaha  zaidi kuliko alivyokuwa  maishani mwake na anahisi vizuri zaidi mwilini. Hali ya  mtu mlegevu huanza  kuwa  mbaya  hadi mbaya  zaidi hadi ulegevu wake unapoanza  kuathiri kila sehemu  ya  maisha  yake. Yeye huruhusu kuyumbushwa  huku na  huko  na  mazingira yake na  hali ilivyo. 
Huwacha  hisia zake zimuongoze,  na  kwavile hajihisi kufanya  lolote,  yeye hutazama  tu na  kulalamika  huku maisha yake yakisambaratika. Anataka  kufanya  mambo mengi, ilhali amezongwa  na  hisia  asizoweza  kuzieleza.  
Anahisi  ulegevu na  hana  mawazo  ya  ubunifu. Anaweza  hata  kuanza  kufikiria kuwa kuna kitu  kilicho kasoro  mwilini  mwake  na hiyo ndiyo sababu  hana nguvu. Kwake yeye, maisha yamekuwa urithi wa matatizo mengi. Kujiruhusu  kukaa  tu bila kufanya lolote mara nyingi  hutokea baada  ya  kupata  pigo  au  msururu wa  mambo  ya  kughadhabisha, au wakati mikasa  inapotokea. Wakati mambo kama  haya yanapotokea, huenda tukataka  kukata  tamaa,  lakini  tunapofanya hivyo, shetani anasubiri kuingia na kuchukua fursa ya hali ilivyo. Hatuwezi kwa  sababu yoyote  kuruhusu ulegevu kumpa nafasi  adui aingie katika  maisha yetu.

Je, unaamini  kuwa  ulimwengu umejaa maovu? Je, unafikiri  jambo fulani  linapaswa  kufanywa kwa  watoto  wanaokabiliwa na njaa? Je, mtu  fulani  anapaswa kuwasaidia watu milioni  1.1 ambao  hawana maji safi ya  kunywa? Je, watu wanapaswa  kuishi barabarani na chini ya  pango za  daraja? Je, familia ambayo umekuwa ukienda nayo kanisani kwa  miaka kadhaa  na kisha halafu ipatwe na mkasa ni  sawa isipopigiwa simu  na mtu  yeyote kujua ni  kwa nini hawajakuwa  wakienda  kanisa  kwa  muda wa  miezi mitatu? Ikiwa kanisa la dhehebu lingine  katika mji  wako limeteketea, je, ni  sawa kuliombea tu na  kutofanya  jambo  lolote kulisaidia? Je,  unaamini mtu fulani anapaswa kufanya kitu kuhusu maovu yaliyoko? Ninafikiri umeyajibu maswali  haya  yote  vizuri,  kwa  hiyo  nina swali moja la mwisho. Utafanya nini?  Je, utakuwa  “mtu  fulani” anayefanya kinachohitajika kufanywa? Ninapouliza  kile utakachofanya,  pengine unahisi hofu kwa  sababu unashangaa “kile utakachofanya”  kitakavyohitaji? Ninaelewa  hisia za  hofu ya  namna  hii. Kwanza,  ikiwa  nitaamua kujisahau mimi  mwenyewe na kuanza  kujaribu kusaidia, ni  nini kitafanyika  kwangu?  Ni nani atakayenijali  mimi  ikiwa sitajijali mwenyewe? Mungu alisema Atakujali,  kwa hiyo  nafikiri tunapaswa kutafuta  ikiwa  kweli  anamaanisha  kile  anachosema.  Kwanini tusistaafu kutokana  na hali ya “kujijali”  na kuona ikiwa Mungu anaweza  kazi bora  kuliko  uliyofanya.  Ikiwa  tutajali  kazi  Yake, ambayo ni kuwasaidia watu wanaoteseka, Ninaamini Atatujali.
Tunahitaji kujua kuwa hisia  zetu zina sauti, na wakati zinapokuwa zimeumia, basi zinaweza kuitikia hali tunayoipitia  kama mnyama aliyeumia. Wanyama walioumia wanaweza kuwa  hatari,  na hisia zilizoumia zinazweza kuwa hivyo pia tukizifuata na kuzitii.Nashukuru Mungu Amemponya mtoto huyu toka kwenye hisia kali za maumivu kupitia Mageuzi ya Upendo.
Mungu awabarikiwi Kundi La June Big Event kwa Kufanya Mageuzi ya Upendo.Wacha  niseme  tena: Ninaamini  kikamilifu  tunahitaji Mageuzi ya Upendo. Sote tumejaribu uchoyo, kuvunjika moyo na kujisikitikia na tumeona matunda yake. Ulimwengu  umejaa matokeo ya mambo haya.  Tuungane  kwa  kukubaliana  kwamba  tutaishi maisha  ya  njia ya Mungu. Kujali kuwa baraka  kwa wengine  (angalia GAL 6:10). Weka upendo (angalia KOL 3:14). Inamaanisha  kuwa imara kwa lengo  la  kuwafikia  wengine.  Tazama  na  omba  upate nafasi;  kuwa jasusi wa  Mungu! Yesu aliinuka kila siku na akafanya  mambo mema (angalia  MDO 10:38). Inaonekana  ni rahisi mno. Ninashangaa  jinsi tulivyoukosa wakati huu wote.Endeleeni Kusonga Mbele.

Mwandishi Jimmy J.

2 comments:

  1. Asante kwa ku share habari hii mtumishi...Barikiwa sana.

    ReplyDelete
  2. Ubarikiwee mtumishi,nimejifunza kitu.

    ReplyDelete