June Big event Imefanya kitu,Wakati wengine wakifanya Sherehe kubwa ya kuzaliwa Binafsi,wao waliamua katika siku hiyo maalum kwao watafanya kitu kwaajili ya kusaidia wenye uhitaji na kuleta mageuzi ya Upendo.Wengi wa watu hawaitikii kwa namna moja. Kila mmoja anaingiwa na huruma wakati anapoona hali ambapo watu wanaishi katika hali mbaya katika vijiji vya mashambani nchini Tanzania au sehemu nyingine za ulimwengu. Wengi hulia, na wengi hutikisa vichwa na kufikiria hali hizi ni mbaya, lakini wote hawaamui kufanya kitu kubadili hali hizi. Wengi huomba Mungu afanye kitu na wanafurahi kwamba huduma ya June Big Event inayoongozwa na Samwel Shan'ga,jimmy John pamoja na Judith Mbondo inafanya kitu, ilhali hawafikirii kumtafuta Mungu kwa bidii kuhusu kile wanachoweza kufanya wao wenyewe. Ningependa kusema wengi hurejea nyumbani, na kujishughulisha na maisha yao tena, na mara husahau kuhusu kile walichoona.
The mission Of Mawaidha Popote is to Prepare the Nations of the world for the coming of Jesus Christ and establishment of the kingdom of God on Earth.our ultimate goal is to achieve a time in history when "the knowledge of the Lord will cover the earth as the waters cover the sea".
Saturday, 30 June 2018
Mavuno Ya Upendo
Kutoa na kuishi katika hali ya kujitolea kwatoa mavuno katika maisha yetu. Hakuna makosa ya kutamani na kutarajia mavuno. Motisha yetu ya kuwasaidia watu wengine haipaswi kuwa ya kujipatia kitu fulani sisi wenyewe, lakini Mungu anatuambia tutavuna kile tulichopanda na tunaweza kutazamia manufaa hayo. Moja ya maandiko yanayoelezea ukweli huu kwa njia nzuri sana yanapatikana katika kitabu cha Luka 6:38; “Wapeni watu vitu, nanyi mtapewa; kipimo cha kujaa na kushindiliwa, na kusukwa-sukwa hata kumwagika, ndicho watu watakachowapa vifuani mwenu, Kwa kuwa kipimo kile kile mpimacho ndicho mtakachopimiwa.”(KJV).
Mungu anaahidi kuwapa thawabu wale wamtafutao kwa bidii (angalia EBR 11:6). Neno thawabu katika maandiko asili ya Kigiriki ya Agano Jipya, linamaanisha “ujira unaopokewa katika maisha haya” au “fidia.”
Je,Kuhusu Mimi...?
Kwa sasa hivi, huenda unafikiria, na je, kuhusu mimi? Ni nani atakayenifanyia jambo mimi? Hili ndilo jambo ambalo kwa kawaida hutuzuia sisi kuishi maisha ambayo Mungu anapenda tuishi. Inanirudia “mimi” kila mara. Je, kuhusu mimi, kuhusu mimi? Tumezoea kuona kwamba matarajio yetu yametimizwa, kwamba wazo la kujisahau sisi wenyewe hata siku moja ni la kutisha. Lakini, ikiwa tunaweza kuwa na ujasiri mkuu wa kujaribu, tutashangazwa na uhuru na furaha tutakayopata. Kwa maisha yangu mengi, mimi huamka kila siku na kujilaza kitandani nikifanya mipango yangu.
Nilifikiri juu ya kile nilichotaka na kitakachokuwa bora kwangu na jinsi ninavyoweza kuishawishi familia yangu na marafiki washirikiane nami katika mipango yangu. Niliamka na kumaliza siku nzima nikiwaza akilini mwangu, na kila wakati mambo yalipokuwa hayaendi nilivyotaka, nilikasirika, nilishindwa kuvumilia, nilitatizika na kukasirika sana. Nilifikiri sina raha kwa sababu sikuwa nikipata kile nilichotaka, lakini nilikosa furaha kwa sababu yote nilikuwa nikijaribu ni kupata kile nilichotaka bila kuwajali wengine. Kwa vile sasa nimegundua kuwa siri ya furaha ni katika kuyatoa maisha yangu kuliko kujaribu kuyahifadhi mimi mwenyewe, asubuhi zangu huwa tofauti.
Friday, 29 June 2018
Kilichotoea Msalabani
Yesu alipokuwa ameangikwa msalabani, alichukua dhambi yetu. Mungu hawezi kukaa kwenye dhambi. Yesu alipochukua dhambi yetu, alitengwa na uwepo wa Babake. Jambo hili lilikuwa limemfanyikia Adamu pia katika bustani ya Edeni. Alipofanya dhambi, uwepo wa Mungu ulimwondokea. Mungu hawezi kuishi na dhambi. Dhambi hujenga ukuta kati ya mwanadamu na Mungu. Yesu alikuwa akibeba dhambi zako na za watu wengine wote alipokuwa akihisi hali hii ya kutokuwepo kwa uwepo wa babake. Alisema “Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha?” (Angalia Mathayo mtakatifu 27:46).
Yesu alijua itatendeka hivi, lakini tisho la kutengwa lilikuwa jambo la kugutusha kupita kiasi alipotenganishwa na uwepo ung’aao wa Mungu Baba, na hilo ndilo jambo lililomfanya kupaza sauti ya kilio hiki. Aliitoa Roho yake kwa Babake na akafa. Kwa hiyo wakauchukua Mwili wake na wakaulaza kaburini na Roho yake ikaenda jehanamu kwa sababu hapo ndipo tungestahili kuenda.
Kumbuka mwanzo wa somo hili, nilisema ukifa, ni mwili wako unaopatwa na mauti. Nafsi na Roho yako huenda mbinguni au jehanamu. Hakuna tumaini la kwenda mbinguni kwa yeyote yule isipokuwa aamini ukweli huu.
Kimbia kwenda Vitani, Usikimbie Vita
Unaposoma kitabu cha Zaburi, moja ya mambo ya kwanza utakayoona ni kwamba Daudi alikuwa mtu aliyejaa matumaini na matarajio. Unaweza kuyasikia haya katika mashairi yake aliyoandika. Hii hapa mifano michache: Iweni hodari, na mpige moyo konde, Ninyi nyote mnaomngoja BWANA! Zaburi 31:24 (imeongezwa msisitizo) Naam, wakungojao hawataaibika hata mmoja... Zaburi 25:3 (imeongezwa msisitizo) Na sasa, ninangoja nini na kutarajia nini, Ee Bwana? Matumaini yangu ni kwako. Zaburi 39:7 (imeongezwa msisitizo)
Iwe alikuwa anachunga kondoo kondeni, au kuongoza kikosi cha askari wasaliti, au kutawala kama mfalme wa Israeli, wakati wote Daudi aliishi akiwa na matumaini kwamba Mungu alikuwa anaenda kutenda kitu cha ajabu maishani mwake. Lakini matumaini ya Daudi hayakumruhusu akae tu bila kufanya kitu chochote. Ukweli ni kwamba, kufanya kitu ndiyo sawa. Matumaini yake yalimchochea awe mtendaji. Daudi aliamini kwamba Mungu alikuwa atatenda kitu cha miujiza, lakini alijua kwamba ana ubia na Mungu na kwamba alihitaji kutii kikamilifu.
Iwe alikuwa anachunga kondoo kondeni, au kuongoza kikosi cha askari wasaliti, au kutawala kama mfalme wa Israeli, wakati wote Daudi aliishi akiwa na matumaini kwamba Mungu alikuwa anaenda kutenda kitu cha ajabu maishani mwake. Lakini matumaini ya Daudi hayakumruhusu akae tu bila kufanya kitu chochote. Ukweli ni kwamba, kufanya kitu ndiyo sawa. Matumaini yake yalimchochea awe mtendaji. Daudi aliamini kwamba Mungu alikuwa atatenda kitu cha miujiza, lakini alijua kwamba ana ubia na Mungu na kwamba alihitaji kutii kikamilifu.
Monday, 25 June 2018
Kuondoa Vikwazo
Bali utafuteni kwanza ufalme wake, na haki yake; na hayo yote mtazidishiwa. Mathayo 6:33
Moja ya silaha za Shetani zenye ujanja zaidi ni kuvuruga. Anajua kama tunapotoshwa na wasiwasi dunia kwamba, kuna uwezekano kwamba, tutaanza kupuuza wakati wetu na Mungu.
Ili kutuweka waaminifu na katika ushirika wa karibu na ushirika pamoja Naye, wakati mwingine Mungu anataka tuondoe vikwazo vinavyotutenganisha naye, hata kama inaumiza.
Mtoe Mungu nje ya Sanduku la Dharura
Hamjui ya kuwa ninyi mmekuwa hekalu la Mungu, na ya kuwa Roho wa Mungu anakaa ndani yenu? 1 Wakorintho 3:16
Nilipenda kutumia muda na Mungu mara moja au wakati maisha yangu yalikuwa shida kubwa. Hatimaye nilijifunza kwamba ikiwa nilitaka kuacha kuishi kutoka kwa dharura moja hadi ya pili, nilihitaji kumtafuta Mungu kila siku kana kwamba nilikuwa na haja kubwa naye.
Ni kweli kwamba Mungu atatusaidia wakati wote tunapokuja kwake. Lakini kama tunataka ushindi wa daima, tunahitaji kumchukua Mungu nje ya sanduku la “dharura tu” na kumwalika katika maisha yetu ya kila siku.
Mungu ndiyo Chanzo Pekee cha kudumu
Nawe utajifurahisha kwa Bwana, Naye atakupa haja za moyo wako. Zaburi 37:4
Kama wanadamu tunaumbwa na Mungu kuwa na furaha na kujisikia vizuri kuhusu sisi wenyewe. Kwa kweli, tunapaswa kujisikia vizuri kuhusu sisi wenyewe, au hatimaye tutaendeleza tabia isiyo ya afya, isiyo na udhibiti ili kupata hisia nzuri tunayotamani.
Kutoa Yote kwa Mungu
Mheshimu Bwana kwa mali yako, Na kwa malimbuko ya mazao yako yote. Ndipo ghala zako zitakapojazwa kwa wingi, Na mashinikizo yako yatafurika divai mpya. Mithali 3:9-10
Watu wengi wanataka kupokea kutoka kwa Mungu, lakini hawana nia ya kujitoa wenyewe kwake. Kweli , ni vizuri kwetu sote kutathmini maisha yetu na hali ya mioyo yetu mara nyingi kutusaidia kukaa makini katika Mungu, tuwe tayari kutoa na kufanya yote anayoweka ndani ya mioyo yetu kufanya.
Upendo wa kweli lazima Upeane
Hili ndilo pendo, si kwamba sisi tulimpenda Mungu, bali kwamba yeye alitupenda sisi, akamtuma Mwanawe kuwa kipatanisho kwa dhambi zetu. Wapenzi ikiwa Mungu alitupenda sisi hivi, imetupasa na sisi kupendana. 1 Yohana 4:10-11
Kila mtu anatamani kupendwa na kukubalika. Lakini wengi wetu wanajaribu kupata furaha kwa njia mbaya. Tunajaribu kuipata katika kupokea, lakini hupatikana katika kutoa.
Upendo wa Mungu ni zawadi nzuri zaidi tunayopewa. Mara tu unapokuja kwetu, unahitaji kuteremka kutoka kwetu hadi kwa wengine; vinginevyo, utakwama.
Mungu anaweza Kukuokoa kutokana na Aibu yako
Badala ya aibu yenu mtapata maradufu, na badala ya fedheha wataifurahia sehemu yao; basi katika nchi yao watamiliki maradufu; furaha yao itakuwa ya milele. Isaya 61:7 Je! Umewahi kujiuliza jinsi maisha yalikuwa kabla Adamu na Hawa kutenda dhambi? Mwanzo 2:25 inatuambia kwamba ingawa Adamu na Hawa walikuwa uchi katika bustani ya Edeni, hawakuwa na aibu.
Naamini kwamba kwa kuongeza kuwa hawakuwa na nguo, maandiko haya pia yanamaanisha kuwa wazi kabisa na waaminifu kwa kila mmoja-si kujificha nyuma ya barakoa yoyote, si kucheza michezo yoyote.Walikuwa huru kuwa wenyewe kwa sababu hawakuwa na hisia ya aibu. Walipofanya dhambi, hata hivyo, walijificha (ona Mwanzo 3: 6-8). Ikiwa si kwa ajili ya kazi ambayo Yesu alifanya msalabani, sote tunapaswa kuishi na aibu kubwa ya dhambi. Lakini kwa sababu ya dhabihu yake, wanadamu wana fursa ya kufurahia uhuru kamili mmoja kwa mwingine na kwa Mungu.
Jifunze kuridhika
Si kwamba nasema haya kwa kuwa nina mahitaji; maana nimejifunza kuwa radhi na hali yo yote niliyo nayo. Wafilipi 4:11
Biblia inatufundisha kuridhika bila kujali hali yetu inaweza kuwa nini. Mtume Paulo aliandika, Sio kwamba ninasema kuwa nilikuwa na matakwa yoyote ya kibinadamu, kwa kuwa nimejifunza jinsi ya kuridhika(yametimizwa kwa uhakika ambako mimi sioni shida au taabu) katika hali yoyote niliyo nayo.
Kuridhika ni uamuzi wa kuwa na furaha na kile ulicho nacho. Kwa bahati mbaya, kwa kawaida tunajifunza kuwa sawa kuishi maisha yasiyopendekezwa kwa muda mrefu na hatimaye kusema, “Bwana, sitaki kuishi tena kwa njia hii tena.” Lakini haipaswi kuwa hivyo.
Unaweza kuchagua kuridhika kila siku. Hii ni ya thamani zaidi kuliko mali zote ambazo unaweza kuzijilia wakati wote wa maisha. Paulo alieleza wazi wakati aliandika katika 1 Timotheo 6: 6 kwamba utakatifu unaongozana na kutosheleza (kwamba kuridhika ambayo ni maana ya kutosha ndani) ni kubwa na faida nyingi.
Sunday, 24 June 2018
Ondoa Vikwazo kwanza
Bali utafuteni kwanza ufalme wake, na haki yake; na hayo yote mtazidishiwa. Mathayo 6:33
Moja ya silaha za Shetani zenye ujanja zaidi ni kuvuruga. Anajua kama tunapotoshwa na wasiwasi dunia kwamba, kuna uwezekano kwamba, tutaanza kupuuza wakati wetu na Mungu.Ili kutuweka waaminifu na katika ushirika wa karibu na ushirika pamoja Naye, wakati mwingine Mungu anataka tuondoe vikwazo vinavyotutenganisha naye, hata kama inaumiza.Kwa mfano, kama kazi zetu au tamaa za fedha au hali ya juu ya kijamii ni muhimu zaidi kwetu kuliko kumpendeza Mungu, tunahitaji kupata vipaumbele vyetu moja kwa moja. Au labda uhusiano unaokuzuia kutumia muda na Mungu na unatafuta tahadhari na kibali cha mtu huyo zaidi ya Mungu.
Cha msingi ni, hali yoyote au tamaa katika maisha yetu ambayo inatuzuia kuongozwa na Roho Mtakatifu au kuishi kwa ajili ya Mungu ni vurugu mbaya ambayo haifai kwetu.
Mungu anataka tuongozwe na Roho Wake, sio kwa vikwazo. Kwa hiyo leo, piga marufuku vikwazo za maisha na umzingatie kwa makusudi Mungu. Unapomtafuta Mungu kwanza kwa moyo wako wote, utampata. Yeye daima yuko pale akikusubiri.
Tuesday, 19 June 2018
Uko Hai au Umekufa...??
Mungu alimwambia Adamu kwamba ikiwa angalikula tunda la mti wa ujuzi wa mema na mabaya basi hakika atakufa. (Mwanzo 2:17.)
Alimaanisha watakufa ndani sio miili yao. Alimaanisha uhai ulio ndani yao utakufa. Nuru itaondoka na watakuwa giza.
Hivi majuzi mtu mmoja aliyeishi maisha ya uovu mwingi alikuwa anafanyiwa upasuaji. Alidhani atakufa, na alitaka kulainisha maisha yake na Mungu. Tulipokuwa tukizungumza naye mimi pamoja na Chris rafiki yangu, alisema “Nahisi nimekufa ndani.” Hebu litafakari jambo hili. Alitaka kuzaliwa mara ya pili kwa sababu alikuwa anahofu atakufa kimwili akiwa angali anafanyiwa upasuaji hata ingawa ukweli ni kwamba alikuwa mfu ndani yake maisha yake yote, na aliyakiri hayo kwa kinywa chake mwenyewe.
Monday, 18 June 2018
Usimzunishe Roho Mtakatifu
Twaweza kumfanya Roho Mtakatifu ahisi kuhuzunika kupitia hasira yetu, kupandwa na ghadhabu, kutosamehe, uchungu, kubishana, na wasi wasi. Biblia inatuhimiza tuwache mambo mabaya ya aina yoyote. Inanihuzunisha kufikiria kwamba ninaweza kumhuzunisha Roho Mtakatifu wa Mungu. Wakati ninapokumbuka jinsi nilivyokasirika kwa urahisi wakati fulani, najua nilimhuzunisha, na sitaki kufanya hivyo tena. Njia pekee ninayoweza kujiepusha na jambo hili ni kuwa mkakamavu kuhusu kuachilia hisia mbaya nilizo nazo kwa wengine mara tu zinaponijia.
Twapaswa kuwa watu wenye manufaa, wa kusaidia, na kuwa wakarimu kwa wengine, kusameheana na kuwa huru kama Mungu katika Kristo alivyotusamehe (angalia EFE 4:30-32). “Wala msimhuzunishe yule Roho Mtakatifu wa Mungu; ambaye kwa yeye mlitiwa muhuri hata siku ya ukombozi. Uchungu wote na ghadhabu na hasira na kelele na matukano yaondoke kwenu, pamoja na kila namna ya ubaya; tena iweni wafadhili ninyi kwa ninyi, wenye huruma, mkasameheane kama na Mungu katika Kristo alivyowasamehe ninyi.” Hasira yetu humfanya Roho Mtakatifu kuhuzunika sio tu kwa sababu Mungu anatutaka tupendane bali kwa sababu najua inavyotuathiri, na anataka tufurahie maisha ya uhuru.
Sunday, 17 June 2018
JE, UNAFAA KUAMINI NINI?
Amini kwamba Yesu alifanya kile Biblia inasema. Amini kwamba ni kweli yeye ni Mwana wa Mungu, aliyezaliwa na bikira. Aliichukua dhambi ya mwanadamu. Alikuwa dhabihu yetu na akafa Msalabani. Hakubaki kwa wafu. Alikaa kaburini siku tatu. Wakati huo aliingia jehanamu na kumshinda Shetani. Haya yote aliyafanya kwa hiari yake mwenyewe kwa sababu alimpenda Babake (Mungu) na kwa sababu Mungu na Yesu walitupenda wewe na mimi sana kiasi ya kwamba ncha ya mpango wowote wa kuleta wokovu ungefi kiwa katika harakati za kuleta ukombozi.
Haikujalisha ni hatua gani iliyostahili kuchukuliwa, mradi tu watu wa Mungu wawe huru tena. Hilo ndilo jambo lililokuwa muhimu kabisa. Yesu alilipa deni ya dhambi zetu msalabani na kwenda Jehanamu kwa niaba yetu. Hatimaye, sawa na jinsi Mungu alivyokuwa ameahidi, siku ya tatu, Yesu alifufuka kutoka kwa wafu.
UAMUZI MUHIMU ZAIDI UTAWAHI KUFANYA
Ningependa kuzungumza nawe kuhusu uamuzi muhimu zaidi. Kusema kweli, huu ndio uamuzi muhimu kabisa ambao utawahi kukabiliana nao. Uamuzi huu ni muhimu zaidi kuliko chaguo la shule utakayoenda, chaguo la kazi, ni nani utakayeoa, au ni wapi utakapoishi.
Uamuzi huu unahusu mahali utakapokuwa milele. Hebu lifi kirie jambo hili. Milele ni muda mrefu, mrefu sana. Watu wengi wanajishughulisha tu na mambo ya leo, au ya miezi michache.
Wengi wanashughulikia swala la watakapostaafu.Ningependa kuzungumza zaidi ya hayo. Ningependa kuzungumza kuhusu “maisha baada ya kufa.” Je unashughulikia swala hilo? Je, wajua kwamba wewe sio nyama na mifupa tu, damu na misuli? Wewe ni roho, una nafsi na unaishi katika mwili. Utakapokufa, ambalo ni jambo litamkumba kila mmoja wetu, mwili wako utalazwa kaburini. Utaharibika na kuwa majivu na mavumbi. Lakini je ni vipi kuhusu “yule wewe wa kweli” – wewe uliye ndani, utu wako, akili, hiari na hisia? Sehemu yako ya kiroho ni sehemu ile ya utu wako ambayo haionekani kwa macho ya miili yetu. Sehemu yako hii ndiyo itakayoishi milele.
Thursday, 14 June 2018
Amini kilicho Bora
Ikiwa tunataka kuwapenda watu, lazima tumwache Mungu abadilishe jinsi tunavyofikiri kuhusu watu na mambo wanayofanya. Twaweza kuamini mabaya na kushuku kila kitu watu wengine wafanyacho na kusema, lakini upendo halisi kila mara unaamini kilicho bora.Kile tunachofikiria na kuamini ni chaguo. Chanzo cha dhiki yetu nyingi katika maisha ni kuwa hatudhibiti au kunidhamisha mawazo yetu. Kwa kutochagua kunidhamisha mawazo yetu, huwa moja kwa moja twachagua kuamini mabaya ya mtu au kushuku.
Nabii Jeremiah aliwauliza watu haya, “ *Mawazo yako mabaya yatakaa ndani yako hata lini? (angalia YER 4:14).* Mawazo waliyochagua kufikiria yalikuwa mabaya kwa Mungu. Wakati tunapochagua kuamini kilicho bora, twaweza kuacha kila kitu kiondoke hasa kile ambacho chaweza kudhuru uhusiano wetu mzuri. Nimeokoa nguvu nyingi ambayo ingetumiwa na hasira kwa kusema, “Ingawa wanachosema au kufanya huniumiza, nachagua kuamini moyo wao uko sawa.”
Thursday, 7 June 2018
Jifunze Kusikiliza
Rafiki yangu mmoja alikuwa akiongea nami kuhusu mwanaume mmoja kijana katika kanisa lake ambaye alikuwa na meno yaliyokaa vibaya. Yalikuwa yamekaa vibaya hivi kwamba alikataa kutabasamu kwa sababu alifedheheka wakati mtu yeyote alipoyaona. Kiukweli Nilimhurumia wakati niliposikia hadithi yake na sikuweza cha kufanya.
Ni mara ngapi tunaposikia kuhusu kitu kama hicho, tunaposikia huruma na kisha tukaondoka bila hata kufikiria iwapo au la twaweza kufanya kitu cha kusaidia? Nafikiri si mara nyingi. Twahitaji kuelimishwa na kufunzwa mara kwa mara. Twahitaji kubuni tabia mpya. Badala ya kudhani kuwa hakuna kitu tunachoweza kufanya, twapaswa kufikiri kuhusu hali hiyo. Kumbuka, Waraka wa kwanza wa Yohana 3:17 inasema: “Lakini mtu akiwa na riziki ya dunia, kisha akamwona ndugu yake ni mhitaji, akamzuilia huruma zake, je! Upendo wa Mungu wakaaje Ndani yake huyo?.
Tuesday, 5 June 2018
Mungu, Huu sio wakati Mnzuri
Biblia inaelezea hadithi kuhusu mwanaume mmoja ambaye hakumfuata Mungu kwa sababu kufanya hivyo lilikuwa ni jambo la usumbufu kwake. Mwanaume huyu aitwaye Feliki, alimtaka Paulo aje na amhubirie injili. Lakini wakati Paulo alipoanza kuzungumza naye kuhusu maisha yaliyonyooka, usafi wa maisha, na kudhibiti hamu alizo nazo, Feliki alishangaa na kuogopa. Alimwambia Paulo aende zake na kwamba atamwita wakati ufaao zaidi (angalia MDO 24:25). “Na Paulo alipokuwa akitoa hoja zake katika habari ya haki, na kuwa na kiasi na hukumu itakayokuja, Feliki akawa na hofu akajibu, Sasa enenda zako, nami nikipata nafasi nitakuita.”
Ninashangazwa mno na jambo hili, sio kwa sababu linafurahisha, bali kwa sababu laonyesha wazi jinsi tulivyo. Hatujali kusikia kuhusu jinsi Mungu alivyo na upendo mwingi kwetu na kuhusu mipango mizuri aliyo nayo katika maisha yetu, lakini wakati anapoanza kutulaumu kwa makosa tunayofanya au kuturekebisha.
kwa njia yoyote, tunajaribu kumwambia kwamba “sasa” sio wakati mzuri. Nina shaka kuwa Yeye huchagua wakati tunaodhani, “ni mzuri,” na nafikiri hufanya hivyo kwa kusudi lake! Wakati wana wa Israeli walipokuwa wakisafiri kupitia jangwani, waliongozwa na Mungu ndani ya wingu mfano wa nguzo wakati wa mchana na ndani ya moto mfano wa nguzo wakati wa usiku. Wakati wingu lilipoenda, pia nao walienda na wakati liliposimama, walikaa mahali walipofika. Jambo la kufurahisha ni kwamba hakukuwa na mtindo au mpango waliofahamu kuhusu ni wakati gani wingu hilo litaenda. Walilazimika kuondoka wakati wingu linaenda (angalia HES 9:15-23).
Monday, 4 June 2018
Kukaa Bila kufanya kitu humwalika Adui
Watu wasiokuwa na lakufanya huvunjika moyo kwa urahisi, hulemewa kimawazo, na kujisikitikia wenyewe. Wanaweza kuanguka katika aina zote za dhambi. Mtume Paulo hata alisema ikiwa mwanamke aliye bado kijana amekuwa mjane, anapaswa kuolewa tena. Lau sivyo huenda asiwe na lakufanya na kuanza masengenyo na kuwa mdakuzi wa mambo (angalia Timotheo 1 5:11-15). Paulo aliendelea kusema kwamba baadhi ya wajane ambao bado wangali vijana kwa kutokuwa na lakufanya tayari walikuwa wameanza kumgeukia shetani. Ina umuhimu gani kuendelea kuwa imara? Ninaamini maandiko ya Paulo yanathibitisha kwamba ni muhimu.
Kwanini Mwili ni Mlegevu...?
Kwa roho zetu twaweza kuunidhamisha na kuutawala mwili, lakini haihitaji juhudi. Inahitaji ushirikiano na Roho Mtakatifu Anayetupa nguvu sisi na kutuwezesha kufanya mambo mazuri. Paulo anasema hatuhitaji kuuwekea mahitaji mwili na ninaamini njia moja ambayo tumeuwekea mwili mahitaji ni kukaa bila kufanya kitu! Kukaa bila kufanya chochote ni mazoea mabaya.
Kadiri tunavyokaa bila kufanya lolote, ndivyo tunavyotaka kutofanya lolote. Nina hakika umewahi kukaa nyumbani siku nzima na kupata kuwa kadiri unavyolala hapo kitandanii, ndivyo unavyohisi ugumu kuinuka. Unapoinuka kwanza, kila kitu huwa kigumu na kuhisi uchovu, lakini unapoendelea kujilazimisha kuondoka, nguvu inakurudia. Leo niliamka nikiwa sina furaha. Nilifanya kazi juma zima kufanya mkutano na bado nahisi uchovu kiasi.
Hakuna Kizuri Kitendekacho Kiajali
Hakuna mageuzi yaliyoubadilisha ulimwengu yaliyotendeka kiajali. Katika baadhi ya mageuzi, yalianza na watu wachache tu waliojadili kuhusu mabadiliko yanayohitajiwa. Iwapo matukio haya ya kihistoria yalizaliwa na ghasia za kawaida au yalipangwa, hayakufanyika tu. Yalifanywa maksudi, kwa kunuiwa, kupendwa na kwa mkakati maalum. Yalianza hivi kwamba mtu fulani alikataa kufanya kitu, mtu fulani “akaachilia mambo yafanyike,” mtu fulani alikataa kusikiza na akapuuza ilhali maovu yalikuwa yamezidi. Mageuzi hutokea kwa sababu mtu fulani huamua kuchukua hatua.
Biblia imejaa maagizo yanayotuhitaji sisi kuyatekeleza. Agizo la kutekeleza badala ya kusikiza ni rahisi, lakini mamilioni ya watu hupuuza. Pengine wanafikiri mambo yatakuwa bora wakijitegemea. Hayawezi. Hakuna kizuri kitendekacho kiajali. Wakati fulani nilijifunza kwamba maisha yangu yamebadilika na kuwa bora. Kutamani kitu hakutoi matokeo tunayotarajia, bali lazima tuwe wakakamavu kufanya kile kinachohitajiwa kufanywa ili kuyapata tuyatakayo. Hatutampata mtu aliyefaulu ambaye katika maisha yake alitarajia kufaulu na hatimaye akafaulu. Vile vile, hatutampata mtu asiyefanya jambo lolote na kisha akafaulu maishani. Mfano huu pia unahusu kuwa sehemu ya Mageuzi ya Upendo.
Wajibu wa mkristo kwa muislam.
Baadhi ya Wakristo wanaona kwamba Huduma ya Injili kwa muislam
ni jambo la ziada tu lakini si lalazima lakini Huduma ya Mkristo yeyote
Yule ni kumfanya Yesu Kristo kujulikana kwa wao wasio mjua,wawe wanaishi
mbali au karibu kwake. Kuhama kwa watu toka nchi za Kiislamu hadi nchi
zenye Wakristo wengi imefungua fursa mpya kwa huduma ya Kikristo katika
maisha yetu ya kila siku.
Kama mwaamini na kushiriki Injili, utapata uwepo unao endelea wa Bwana Yesu Kristo: Kwa sababu hii, enendeni ulimwenguni mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi, mkiwabatiza kwa Jina la Baba na la Mwana na la Roho Mtakatifu, nanyi wafundisheni kuyashika mambo yote niliyowaamuru ninyi. Hakika Mimi niko pamoja nanyi sikuzote, hadi mwisho wa nyakati Kuhusu Kristo na cha kuzingatia ni hapa sasa, huduma ya Kikristo kushikilia katika tarajio ni Muhimu sana kwa maisha yote, matarajio, na utu wa upeo wa Kiislam.Walakini, watu wengi hawajui jinsi ya kushiriki Injili kwa Waislam au wameogopa kufanya hivyo. Kwa ukurasa huu kuna baadhi ya miongozo jinsi ya kushiriki nao.
Kama mwaamini na kushiriki Injili, utapata uwepo unao endelea wa Bwana Yesu Kristo: Kwa sababu hii, enendeni ulimwenguni mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi, mkiwabatiza kwa Jina la Baba na la Mwana na la Roho Mtakatifu, nanyi wafundisheni kuyashika mambo yote niliyowaamuru ninyi. Hakika Mimi niko pamoja nanyi sikuzote, hadi mwisho wa nyakati Kuhusu Kristo na cha kuzingatia ni hapa sasa, huduma ya Kikristo kushikilia katika tarajio ni Muhimu sana kwa maisha yote, matarajio, na utu wa upeo wa Kiislam.Walakini, watu wengi hawajui jinsi ya kushiriki Injili kwa Waislam au wameogopa kufanya hivyo. Kwa ukurasa huu kuna baadhi ya miongozo jinsi ya kushiriki nao.
KUPATA UPONYAJI KUTOKA KWA PIGO AU MSIBA
“Roho wa Bwana yu juu yangu, kwani amenipaka mafuta niwahubirie maskini Habari Njema. Amenituma niwatangazie mateka watapata uhuru, vipofu watapata kuona tena; amenituma niwakomboe wanaoonewa. Luka 4:18
Haijalishi kilichotokea katika maisha yako kusababisha huzuni na upweke, unaweza kuwa na uhakika kwamba Mungu atakuongoza katika kupokea uponyaji wako. Naye atakuonyesha wakati ambapo utakuwa unakubalia hisia zako kwenda mrama au kupoteza usawa wako - iwapo utakubali kumsikiza Roho wake. Haiwezekani kwetu kukadiria kiasi cha wakati ambao unafaa kutumika katika kuomboleza kwa sababu hali na watu ni tofauti. Lakini, hata kama itachukua muda mrefu kiasi gani, kutakuwa na wakati ambapo Bwana atasema, “Sasa ni wakati wako wa kuamka na uendelee mbele. Ni lazima uachane na hayo ya kale nawe umalize mbio ambayo nimekuwekea katika maisha yako.
Je Quran Imetoka wapi?
Niseme mapema kwamba nimechoka na
kelele ambazo waislam wamekuwa wakitupigia masikioni mwetu na kututaka
kutuaminisha kuwa Quran ni kitabu cha Mwenyenzi Mungu,jambo ambalo
siwezi kulikubali bila kulifanyia utafiti,maana waislam wamekuwa
wakiongea kama waimba taarabu, yaani kuongea bila kuleta udhibitisho wa
kile wanachokisema jambo ambalo mkristo yeyote makini hawezi kukubali
jambo bila kupata udhibitisho hakinifu.
Lakini jambo moja la kushangaza waislam wenyewe wamekuwa wakwanza kutojua hata kitabu chao wanachokiamini, kama woote tunavyofahamu kuwa dunia ziko dini nyingi sana na zote zina vitabu vyake vitakatifu vinavyodaiwa kuwa ni Neno la Mungu na kuwa ndio mamlaka ya Mwisho ya Dini hizo wahindu wanakitabu chao kiitwacho
Lakini jambo moja la kushangaza waislam wenyewe wamekuwa wakwanza kutojua hata kitabu chao wanachokiamini, kama woote tunavyofahamu kuwa dunia ziko dini nyingi sana na zote zina vitabu vyake vitakatifu vinavyodaiwa kuwa ni Neno la Mungu na kuwa ndio mamlaka ya Mwisho ya Dini hizo wahindu wanakitabu chao kiitwacho
Kwanini Yesu aitwe Mungu?
Kupitia Qur’an Na Biblia.
Kelele nyingi zimesikika miongoni mwetu, Waislam wakijaribu kutuaminisha juu ya kile wanachoamini, Wanaendelea kushikilia mitazamo yao kuhusu Uungu wa Yesu,Chanzo cha maswali yote wanayouliza juu ya Bwana Yesu kinaanzia mara tu Yesu alipovaa mwili wa kibinadamu tendo hilo kwa fikra za haraka tu linaweza kudhaniwa kuwa ndilo linaloshusha mamlaka yake ya asili kama Mungu. Pamoja na hayo mimi binafsi nichoelewa ni kuwa tendo hilo kamwe halishushi mamlaka bali linafunika mamlaka aliyokuwa nayo kwa kadri ya sababu Ifuatayo:-
Mungu aliwahi kujifunua wazi katika nyakati za nyuma na wanadamu wakaangamia
Fuatilia:- kutoka 19:20-21 Bwana akaushukia mlima, juu ya kilele cha mlima; Bwana akamwita Musa aende hata kilele cha mlima; Musa akapanda juu. Ndipo Bwana akamwambia Musa, Shuka chini, uwaonye watu wasije wakapasua njia waje kwa Bwana kutazama, kisha wengi miongoni mwao wakaangamia.
Kelele nyingi zimesikika miongoni mwetu, Waislam wakijaribu kutuaminisha juu ya kile wanachoamini, Wanaendelea kushikilia mitazamo yao kuhusu Uungu wa Yesu,Chanzo cha maswali yote wanayouliza juu ya Bwana Yesu kinaanzia mara tu Yesu alipovaa mwili wa kibinadamu tendo hilo kwa fikra za haraka tu linaweza kudhaniwa kuwa ndilo linaloshusha mamlaka yake ya asili kama Mungu. Pamoja na hayo mimi binafsi nichoelewa ni kuwa tendo hilo kamwe halishushi mamlaka bali linafunika mamlaka aliyokuwa nayo kwa kadri ya sababu Ifuatayo:-
Mungu aliwahi kujifunua wazi katika nyakati za nyuma na wanadamu wakaangamia
Fuatilia:- kutoka 19:20-21 Bwana akaushukia mlima, juu ya kilele cha mlima; Bwana akamwita Musa aende hata kilele cha mlima; Musa akapanda juu. Ndipo Bwana akamwambia Musa, Shuka chini, uwaonye watu wasije wakapasua njia waje kwa Bwana kutazama, kisha wengi miongoni mwao wakaangamia.
Sunday, 3 June 2018
SUBIRA,TAFADHALI!!
Biblia inasema katika Waebrania 6:12 kwamba tunarithi ahadi zake kwa imani na uvumilivu. Kupokea urithi hakuhitaji bidii yoyote kutoka kwetu. Tunahitaji kungoja tu, mpaka wakati ulioteuliwa.
Kwa mfano unaweza kuamini, au kuwa na imani kwamba jamaa yako fulani amekuwosia urithi fulani, lakini ni lazima uwe na uvumilivu na kusubiri wakati ufaao kufika ili upokee urithi ule. Imani na subira ni hushirikiana katika kutimiza jambo lolote. Zinafanya kazi pamoja kutimiza lengo linalotarajiwa. Yakobo 1:2, 3 (Tafsiri ya AMP) inasema kuwa yafaa tufurahi “tunapoangukia majaribu ya kila aina”, tukijua kwamba “kuthibitishwa kwa imani yetu” huleta saburi. Na saburi ikishafanya kazi yake kikamilifu, tutakuwa watu ambao “wamekomaa kikamilifu … wasiopungukiwa na neno.”
Jamani! Andiko la ajabu hili!
Jamani! Andiko la ajabu hili!
WAKATI UFAAO KUAMINI
“Nilikuamini, na kukutegemea, na kuwa na uhakika ndani Yako, Ee Bwana. Nilisema, Wewe ndiwe Mungu wangu. “Nyakati zangu zimo mikononi mwako; nikomboe kutoka kwa mikono ya adui zangu na wale wanaonifuatia na kuniletea dhiki.” Zaburi 31: 14,15 AMP Katika sura hii, mwandishi wa Zaburi ansema kwamba alimtumainia Mungu kumkomboa, na alimtegemea kufanya hivyo kwa wakati uliofaa. Kumtumainia Mungu kunahitaji tuseme, “Nyakati zangu zimo mikononi Mwako.”
Nimejifunza kwamba tegemeo linatuhitaji kukubali kwamba kuna maswali mengine ambayo yatabaki yakiwa hayana majibu na hivyo basi kuweka nyakati zetu mikononi mwake Mungu – tukiamini kwamba japo hatuyajui majibu yote, Yeye ayajua. Anao wakati unaofaa kikamilifu kwa kila jambo maishani mwetu.
Nimejifunza kwamba tegemeo linatuhitaji kukubali kwamba kuna maswali mengine ambayo yatabaki yakiwa hayana majibu na hivyo basi kuweka nyakati zetu mikononi mwake Mungu – tukiamini kwamba japo hatuyajui majibu yote, Yeye ayajua. Anao wakati unaofaa kikamilifu kwa kila jambo maishani mwetu.
MSIMU MWAFAKA
Mambo Ya Walawi 26:4 inasema, “Nitazinyezesha mvua zenu kwa nyakati zake.” Wagalatia 6:9 kwa tafsiri ya AMP inasema ni lazima “…tusife moyo na kuwa wachovu na kuzimia katika kutenda kiungwana na kutenda yaliyo ya haki, maana kwa wakati wake na kwa msimu ulioteuliwa tutavuna, kama tusipouachilia na kupunguza ujasiri wetu na hapo kuzimia.”
Friday, 1 June 2018
VIWANGO SABA VYA KUOMBOLEZA
Mtumaini Mungu kwa moyo wako wote, wala usitegemee akili zako mwenyewe.Umtambue Mungu katika kila ufanyalo, naye atazinyosha njia zako. Mithali 3:5-6 Baada ya mtu kupatwa na msiba au pigo fulani, karibu kila mmoja wetu hupitia hali ya kuomboleza. Kwa kawaida, kuna viwango saba katika kuomboleza. Hebu tuvichunguze viwango hivi kwa makini na tujaribu kupata ufahamu ni nini kinachokuwa kikitendeka katika nafsi zetu na kile tunachoweza kufanya ili kupitia kiwangi hicho kitufaidi kikamilifu.
Kiwango Cha 1: Kushtuka na Kukataa Mara nyingi, mambo haya mawili huwa ndiyo ya mwanzo kutokea tunapopatwa na pigo au msiba. Mungu huyatumia kutulinda ili tusivunjike kabisa. Kushituka: Mshituko ni hali ambayo inagutusha nia na hisia zetu kwa pigo kubwa mno ambalo halikutarajiwa. Kuweza kushtuka ni hali tunayozaliwa nayo ndani yetu. Hutupatia muda wa kuweza kukubaliana na mabadiliko yaliyotukia. Hutuzuia kukumbana na ukweli mara moja.
Kiwango Cha 1: Kushtuka na Kukataa Mara nyingi, mambo haya mawili huwa ndiyo ya mwanzo kutokea tunapopatwa na pigo au msiba. Mungu huyatumia kutulinda ili tusivunjike kabisa. Kushituka: Mshituko ni hali ambayo inagutusha nia na hisia zetu kwa pigo kubwa mno ambalo halikutarajiwa. Kuweza kushtuka ni hali tunayozaliwa nayo ndani yetu. Hutupatia muda wa kuweza kukubaliana na mabadiliko yaliyotukia. Hutuzuia kukumbana na ukweli mara moja.
Subscribe to:
Posts (Atom)