[Matumaini haya] tuliyo nayo kama nanga ya roho, yenye salama, yenye nguvu... Jimmy J
Waebrania 6:19 Tunahitaji matumaini wakati wote, lakini hasa wakati tunapokuwa tunaumia.
Matumaini huonekana vigumu kupatikana wakati tunaposongwa na mambo magumu au tunapokumbwa na aina yoyote ya uchungu Hata hivyo, si lazima utumie maneno “napitia wakati mgumu” kama kisingizio cha kuvunjika moyo kufadhaika, na kukosa matumaini. Ingawa ni vigumu zaidi, ni muhimu zaidi wakati wote kuwa na matumaini wakati unapopitia magumu. Mungu anataka tuwe salama, si kutuacha tukiwa tumekwama.
Tunapopata hasara fulani, natukabiliane na hasara hiyo na, katika mchakato huo tusijipoteze wenyewe. Tunapopatwa na janga natuomboleze vizuri na tusiache roho ya huzuni iweze kubadilisha maisha yetu yote kuwa janga.
Tunapovunjika moyo, natuteuliwe tena. Tunapofadhaika, natutazame juu kwa sababu sote tutahisi vizuri ikiwa tutatembea kifua mbele. Kila kitu juu ya Yesu kiko juu! Alitoka Mbinguni, akarudi Mbinguni wakati alipokamilisha kazi yake duniani, na tunaahidiwa kwamba atarudi tena mawinguni na kila jicho litamwona. Anainua vichwa vyetu, roho zetu, na maisha yetu.
Kwa upande mwingine, tuna adui aitwaye Lusifa, Shetani, mwongo mkuu, au ibilisi, na kila kitu anachotoa ni kitu cha kutushusha chini. Anatoa mfadhaiko, kuvunjika moyo, simanzi, magonjwa, kukata tamaa, kukosa matumaini, talaka, kifo, na kadhalika. Ninatangaza vita dhidi ya kukosa matumaini, na ninakuomba uungane nami katika vita hivi. Kila mmoja anayejituma kutangaza matumaini kila mahali anapokwenda atakuwa sehemu ya jibu linalohitajiwa na ulimwengu.
No comments:
Post a Comment