Monday, 23 July 2018

MATUMAINI WAKATI UNAUMIA

[Matumaini  haya] tuliyo nayo kama  nanga  ya  roho, yenye salama, yenye nguvu... Jimmy J
Waebrania 6:19 Tunahitaji  matumaini  wakati  wote,  lakini hasa wakati  tunapokuwa tunaumia.

Matumaini  huonekana vigumu kupatikana  wakati tunaposongwa na mambo magumu au tunapokumbwa na aina yoyote  ya  uchungu Hata  hivyo, si lazima  utumie  maneno “napitia wakati mgumu”  kama  kisingizio  cha kuvunjika  moyo kufadhaika, na kukosa matumaini. Ingawa ni vigumu zaidi, ni muhimu zaidi wakati  wote  kuwa na matumaini wakati  unapopitia  magumu.  Mungu  anataka  tuwe salama, si kutuacha tukiwa tumekwama.
Tunapopata  hasara  fulani,  natukabiliane  na hasara  hiyo na, katika mchakato huo tusijipoteze wenyewe.  Tunapopatwa na janga natuomboleze  vizuri na tusiache  roho ya  huzuni iweze  kubadilisha maisha yetu  yote  kuwa janga.


Tunapovunjika  moyo, natuteuliwe tena.   Tunapofadhaika, natutazame  juu kwa  sababu sote tutahisi vizuri ikiwa tutatembea kifua mbele. Kila  kitu  juu  ya  Yesu  kiko  juu!  Alitoka  Mbinguni,  akarudi Mbinguni wakati  alipokamilisha kazi yake duniani, na tunaahidiwa kwamba atarudi tena  mawinguni  na kila jicho litamwona. Anainua vichwa vyetu,  roho zetu,  na maisha yetu. 

Kwa upande  mwingine, tuna  adui  aitwaye  Lusifa,  Shetani,  mwongo  mkuu,  au  ibilisi,  na  kila kitu anachotoa ni  kitu cha kutushusha  chini.  Anatoa mfadhaiko, kuvunjika  moyo, simanzi, magonjwa, kukata  tamaa,  kukosa matumaini, talaka, kifo, na kadhalika. Ninatangaza  vita  dhidi  ya  kukosa  matumaini,  na  ninakuomba uungane nami katika vita hivi.  Kila mmoja anayejituma kutangaza matumaini kila mahali anapokwenda atakuwa sehemu ya jibu linalohitajiwa na ulimwengu.

No comments:

Post a Comment