Friday, 27 July 2018

Ukahaba wa Vijana

Makala```

Uza mwili  wako ili  kuwafurahisha wanaume waovu  au ufe njaa.  Ni chaguo baya  sana  ambalo  mtu hapaswi kufanya.
Ingawa  ana  umri  wa  miaka  kumi  na tisa,  Suzi amefanya chaguo  hili tangu  akiwa  na  umri wa  miaka  kumi na  minne. Na  kwa  kila chaguo, moyo wake huvunjika  sana  na roho yake inaharibiwa.  Kwa  yote  aliyopitia,  ni miujiza kwamba bado anahisi chochote.

Anapata  nguvu wakati anapoangalia  macho  ya  bintiye wa  umri wa  miezi  saba,  Aamina,  maana  yake ni “salama,” na Suzi ameamua kuwa atafanya chochote  awezacho kuweka ahadi yake ya kumweka binti yake salama. Hauzi mwili  wake kwa  tamaa  au kujifurahisha.  Anauza mwili wake ili aishi. 


 Anaishi  na  kufanya  kazi  yake katika chumba cha upana wa futi nne na urefu wa futi tisa. Amefanya kazi  kwa  miaka  mitano…  hana  siku za  kupumzika… Anafunga macho yake na kumfikiria Aamina, ilhali wanaume wapatao  kumi na  watano  kwa  siku huudhulumu  mwili wake ili  kuridhisha tamaa  zao  mbovu.
Uchungu huo haufikiriki, lakini ndiyo njia pekee anayojua  ya  kumpa chakula  na mahali pa  kulala. 

Wakati anapofikiria  kuhusu  jinsi  anavyompenda Aamina,  hawezi kuelewa  jinsi mama  yake alivyomtelekeza wakati alipokuwa na umri wa miaka mitano. Kabla  ya  kuja  kwa  kile kinachojulikana  kama  wilaya  ya taa  nyekundu ( yaani  eneo la  ukahaba) , alikuwa  anakufa  njaa.    “ Nilikuwa na tumaini, lakini tumaini hilo liko  mbali  nami.  Ninajua Mungu  yuko  nami na ananipenda. Sijui njia nyingine  yoyote  ya kuishi.”
Tumaini  linaloonekana kwa  mbali likidumu  kwa  siku moja  wakati maisha yasipomgharimu moyo wake, roho yake, na kuuharibu mwili wake. Hivi  leo, matumaini hayo yatahitaji  kusubiri.  Mteja wake mwingine amewasili sasa hivi. Takwimu zasema:

•  Umri  wastani  wa  kuingia katika  ukahaba  kote ulimwenguni  ni miaka  kumi  na mitatu hadi miaka  kumi na minne.

•  Asilimia  75 ya makahaba wako chini  ya umri  wa miaka Ishirini na tano.

Nilipelekwa kwenye danguro moja  lenye vyumba vitatu vidogo vikiwa na vitanda  vitatu kila chumba.  Hakukuwa na faragha  kwenye sehemu  ya  vitanda  hivi hata kidogo. Wasichana  au wanawake waliwahudumia wanaume katika vyumba hivi vidogo  hasa  wakati wa  usiku, wakitumai  kupata  pesa za  kutosha kuweza kula na kuwalisha watoto  wao  ikiwa walikuwa nao,  na  wengi wao walikuwa nao. Watoto wao walikuwa wapi wakati wao  wakifanya  kazi?  Ama  pengine walikuwa  wakicheza   karibu na ukumbi  ambako wanaweza  kufika kwa  urahisi kwenye vyumba vya mama zao waliko au  walipewa pombe  ili  kuwafanya walale ili  wasiwajali mama  zao.

Bila  ya  msaada,  wengi wa  watoto  wa  kike…wasichana wadogo…wataingizwa  katika  maisha  ya  ukahaba  mara  tu wanapokuwa  wakubwa.  Wanawake  hawa hawaishi namna hii  kwa sababu wanataka  kuwa hivyo; hawana  lingine  la kufanya.  Hawana elimu  na wamelelewa  katika hali ya umaskini  ambao  wengi wetu hatuwezi kuelewa ulivyoanza. Baadhi yao kwa kweli wanasimamiwa na  wanaume ambao,  kwa  malengo  yao,  huwafanya  kuwa  kama wafungwa na kuwapiga ikiwa hawaleti pesa za kutosha.

Ninaweza kuongeza kwamba baadhi ya wanawake waliokomaa waliokwama katika ukahaba ni  wajane. Ama  waume zao  wamefariki au kuawa  katika baadhi  ya visa na kuwaacha  bila chochote  cha kuwasaidia,  kwa  hiyo  kwa  mara  nyingine tena  wakalazimika kufanya kile wanachofikiria kinaweza kuwapa pesa. Twaweza  kujifunza kufanya  kilicho sawa  ili kuwasaidia walionyanyaswa  ulimwenguni. Kile  tunachohitaji ni habari  na  ari na twaweza  kuleta tofauti ifaayo katika  maisha  ya  watu wengi. Ikiwa kila mmoja wetu atafanya sehemu  yake twaweza kuanza  mageuzi ya upendo.

Tafakari

Jiunge na mwana Mageuzi.

Jimmy J.

No comments:

Post a Comment