"baba yangu alinidhulumu mimi kingono kwa miaka mingi na matendo yake ya uovu yaliharibu roho yangu na kuniacha nimejeruhiwa na siwezi kufanya kazi kama kawaida hadi Yesu aliponiponya. Kusahau yale aliyonifanyia na kuweza kumsamehe kabisa lilikuwa jambo gumu kabisa. Kwanza, nilifanya uamuzi nisimchukie tena kwa sababu Mungu alinifanya nifahamu kwamba kumpenda Yeye na kumchukia baba yangu mzazi hakungekaa katika moyo mmoja."
"Nilimpokea Yesu kama Mwokozi wangu nikiwa na umri wa miaka tisa, lakini sikuelewa nilichokuwa nacho ndani Yake au jinsi ya kuwa na uhusiano Naye kungebadili maisha yangu kwa sababu sikuwa na “elimu ya kuendelea” katika maswala ya kiroho. Nyumba niliyolelewa haikuwa ikifanya kazi. Baba yangu alikuwa mlevi, asiye mwaminifu kwa mama yangu huku akiwa na wanawake wengi, na alikuwa mtu mkali mwenye fujo na hasira. Kama nilivyotaja hapo awali, pia alinidhulumu kingono kila mara.Annah
"Nilimpokea Yesu kama Mwokozi wangu nikiwa na umri wa miaka tisa, lakini sikuelewa nilichokuwa nacho ndani Yake au jinsi ya kuwa na uhusiano Naye kungebadili maisha yangu kwa sababu sikuwa na “elimu ya kuendelea” katika maswala ya kiroho. Nyumba niliyolelewa haikuwa ikifanya kazi. Baba yangu alikuwa mlevi, asiye mwaminifu kwa mama yangu huku akiwa na wanawake wengi, na alikuwa mtu mkali mwenye fujo na hasira. Kama nilivyotaja hapo awali, pia alinidhulumu kingono kila mara.Annah
"Orodha hii inaendelea, lakini nina hakika umeipata picha hiyo. Annah anaendelea kusema " Nilimpenda Mungu na nilitaka kujifunza, kwa hivyo nikajiunga na masomo ambayo hatimaye yaliniruhusu kuthibitishwa katika dhehebu na kwenda kanisani kila mara.
Nilijifunza kuhusu upendo wa Mungu na neema, na vile vile nikajifunza imani mbali mbali za kikanisa ambazo ni muhimu kwa msingi wa imani. Nilipofika umri wa miaka thelathini na miwili, Nilijipata nimetatizika sana kwa sababu Ukristo wangu haukuonekana kunisaidia katika matendo yangu ya kila siku maishani.
Niliamini ningekwenda mbinguni wakati nitakapokufa, lakini nilikuwa na haja sana na msaada ili niweze kuendelea kila siku duniani kwa amani na furaha. Roho yangu ilijazwa na uchungu kutokana na kudhulumiwa nilipokuwa mtoto na niliuongeza uchungu huo kila siku katika fikra zangu na kutokuwa na uwezo wa kudumisha uhusiano mwema."
Neno la Mungu latuambia kwamba ikiwa tutamtafuta Mungu kwa bidii tutampata (angalia MIT 8:17). " Nilianza kumtafuta Mungu mimi mwenyewe kwa chochote nilichokosa, na nilikutana naye na hiyo ikanifanya niwe karibu Naye. Mara moja alionekana kuwepo sana katika maisha yangu ya kila siku na nikaanza kuchunguza kwa bidii ili Nimjue vyema zaidi. Ilionekana kuwa kila mahali nilikogeuka, nilisikia kuhusu imani. Nilijifunza kwamba ningetumia imani katika hali nyingi, ambazo zingefungua mlango kwa Mungu kuhusika na kunisaidia. Niliamini na moyo wangu wote kwamba mambo niliyojifunza yalikuwa sawa, lakini bado nilipata matatizo makuu kwa sababu Nilikuwa nimepata ufanisi mkubwa, lakini bado nilihisi katika moyo wangu kwamba kuna kitu kilichokosekana, kwa hiyo kwa mara nyingine tena nikaanza kumtafuta Mungu kwa bidii zaidi. Kupitia kumtafuta kwangu na kuchunguza kwa undani zaidi nilijifunza kwamba nimekosa funzo kuu ambalo Yesu alikuja kutufunza: kumpenda Mungu, kujipenda sisi wenyewe, na kuwapenda wengine (angalia MAT 22:36-39). Nilijifunza mengi kuhusu imani nilivyokuwa nikitembea na Mungu, lakini sikuwa nimejifunza kuhusu nguvu ya upendo....."
Biblia inasema kwamba Mungu alitununua kwa gharama kubwadamu ya Mwanawe, Yesu Kristo (angalia 1 KOR 6:20, 1 PET 1:19, UFU 5:9).
Kitendo hiki cha kushangaza cha uzuri kiliondoa uovu wa shetani aliofanya na kufungua njia kwa watu wote kusamehewa dhambi zao na kufurahia uhusiano wa kibinafsi na Mungu. Kama nilivyoeleza, baba yangu alinidhulumu mimi kingono kwa miaka mingi na matendo yake ya uovu yaliharibu roho yangu na kuniacha nimejeruhiwa na siwezi kufanya kazi kama kawaida hadi Yesu aliponiponya. Kusahau yale aliyonifanyia na kuweza kumsamehe kabisa lilikuwa jambo gumu kabisa. Kwanza, nilifanya uamuzi nisimchukie tena kwa sababu Mungu alinifanya nifahamu kwamba kumpenda Yeye na kumchukia baba yangu mzazi hakungekaa katika moyo mmoja.* Nilimuuliza Mungu anisaidie na akaniondolea chuki kutoka moyoni mwangu. Hata hivyo, bado sikutaka kufanya mambo mengi na baba yangu na nilikaa mbali sana naye.
Afya ya akili ya mama yangu iliendelea kuzorota kwa miaka kadhaa alikuwa na ugonjwa wa akili kutokana na kujua kile ambacho baba yangu alinifanyia na bila kujua jinsi ya kukabiliana nacho. *Alimfumania akinidhulumu wakati nilipokuwa na umri wa miaka 14, lakini kama nilivyosema, hakujua kile anachoweza kufanya, kwa hiyo hakufanya kitu.
Kutofanya kitu kuligeuka kuwa uamuzi mbaya kwetu sote. Kwa miaka miwili, alitibiwa matatizo ya mshutuko wa akili na matibabu hayo yaliondoa mawazo ya kukumbuka matendo ya kudhulumiwa kingono niliyofanyiwa na sikutaka kufanya kitu ambacho kingelisababisha akumbuke tena, kwa hiyo ingawa ilikuwa vigumu kwangu kuwa karibu na baba yangu, familia yangu ilinitembelea wakati wa likizo na wakati mwingine ambao tungepaswa kufanya hivyo tu. Hatimaye wazazi wangu waliondoka mjini na kurejea katika mji mdogo ambako waliendelea kuishi. Ulikuwa karibu umbali wa maili mia mbili kutoka mahali nilikokuwa nikiishi na nilifurahi kwa sababu kuondoka kwao kulimaanisha singewaona sana. Nilifaulu kumsamehe baba yangu kwa kiasi fulani katika miaka hiyo, lakini sikuwa nimemsamehe kabisa.
Nilisoma kila maandiko niliyopata kuhusu kuwapenda adui zako, kuwa mkarimu kwa wengine na kuwafanyia hisani. Hii ilinigusa kweli:
Bali wapendeni adui zenu, tendeni mema, na kukopesha msitumaini kupata malipo, na thawabu yenu itakuwa nyingi; nanyi mtakuwa wana wa Aliye juu, kwa kuwa Yeye ni mwema kwa wasiomshukuru, na waovu. (LK 6:35).
Kifungu hiki chasema tusifikirie kuwa tumepoteza kitu na kukata tamaa kuhusu chochote. Kabla nielewe jambo hili, niliangalia utoto wangu kama miaka iliyopotea, sasa Mungu alikuwa akiniuliza niione kama ujuzi nilioupata ninaoweza kuutumia kwa wengine.
Luka pia alisema twapasa kuuliza baraka kwa wengine na kuwaombea wale wanaotudhulumu na kututumia vibaya (angalia LK 6:28). Hii inaonekana si haki, lakini tangu hapo nimejifunza kwamba ninaposamehe ninajifanyia hisani mimi mwenyewe. Wakati ninapo- samehe, najiweka huru kutokana na matokeo yote ya uongo niliyofanyiwa na kisha Mungu anaweza kukabiliana na hali yote hiyo. Ikiwa adui yangu hajaokoka, huenda nikanunua roho.
Baba yangu alishangazwa mno na ukarimu tuliomfanyia mimi na mume wangu. Miaka mitatu baada ya kufanya kile Mungu alichotuuliza tufanye, baba yangu alitubu kwa machozi na akamkubali Yesu kuwa Mwokozi wa maisha yake. Lilikuwa ni jambo la kushangaza. Alilianza jambo hili yeye mwenyewe. Alituomba tuje nyumbani kwake, na akaomba msamaha..
Mwandishi
Jimmy J.
Jimmy J.
No comments:
Post a Comment