Kutumia muda mwingi pamoja na mtu au kitu fulani, huleta uhusiano wa karibu na mtu au kitu hicho. Kama wanadamu, sisi ni roho, tuna nafsi, na tunaishi katika mwili. Nafsi inaweza kuelezwa kama nia, hisia na hiari yetu. Tunapojihusisha na mtu au kitu, sisi hutumia muda mrefu kumfikiria, kuwaza juu ya mtu au jambo hilo na kufanya mipango inyayohusu uhusiano huo. Kwa kawaida, mazungumzo yetu huwa juu ya mambo ambayo tunahusika nayo katika nia zetu, mapendekezo yetu na hisia zetu.
Ukiliwazia jambo hili, utaona jinsi ‘nafsi’ zetu zinavyohusika zaidi na watu au vitu tunavyotumia muda na nguvu zetu kushughulikia. Iwapo mkono wangu ungelifungwa kwenye mwili wangu na kukaa pale kwa muda wa miaka mingi bila ya kufanya chochote, basi matokeo yanaweza kuwa ya kutisha. Iwapo ungelifunguliwa mara, basi ungekuwa umenyauka, bila nguvu, na tena umelemaa. Singeweza kuutumia mpaka uweze kupata nguvu tena na uwezo wa kufanya kazi. Ingenibidi nitafute njia mpya za kuufanyisha mazoezi ili misuli ambayo imedhoofika iweze kupata nguvu.
Hivi ndivyo ilivyo kuhusu nafsi zetu. Wakati tunapohusika na mtu, mahali au kitu fulani kwa muda mrefu, nafsi zetu “hufanganishwa” na jambo hilo.
Wakati mtu au kitu kile kinapochukuliwa kutoka kwetu, sisi huwa katika hali ya kutaka kuendelea na maisha kana kwamba kingali kupo. Kama mkono ambao ulikuwa umefungwa kwa muda mrefu, hata ingawa umefunguliwa, unaendelea kuhisi kana kwamba ungali umefungwa. Haufanyi kazi vizuri hadi baaada ya muda ambapo umefanyishwa mazoezi ili uweze kurejea hali yake ya kwanza. Hata wakati tunapoamua kuachana na mtu au jambo fulani, nafsi yetu inaweza kutamani kuendelea kukaa pale.
Hisia zetu zina nguvu mno, nazo zinaweza kutuletea dhiki na uchungu mkuu. Ni lazima tugundue kuwa tunaweza kutumia “hiari” yetu kuamua kukubali au kukataa kufanya jambo fulani. Uamuzi thabiti wa hiari yetu, unaweza kushinda hisia mbaya hata zinapokuja kwetu zikiwa na nguvu nyingi. Kuna “vifungo vya nafsi” vibaya, na kuna vingine vizuri. Vifungo vyema hufikia hali ya usawa baada ya muda. Lakini vile vibaya huhitaji kukabiliwa na kuondolewa.
Haijalishi unalishughulikia jambo gani sasa hivi, lisipotatuliwa kwa njia inayofaa, huenda likakufunga zaidi, hata kukuletea ulemavu katika sehemu hiyo ya maisha yako. Hata hivyo, Mungu anajua jinsi ya kukufungua! Iwapo umeumia kutokana na ajali, pengine itabidi ujifundishe kutembea tena.
Ikiwa umempoteza mwenzi wako katika kifo au kwa sababu ya talaka, inaweza kukubidi ujizoeze kuishi peke yako. Labda itakubidi ujifunze kufanya kazi fulani ambazo ulikuwa umesahau jinsi zinavyofanywa, au ambazo hujawahi kufanya hapo mbeleni. Inaweza kukubidi utafute kazi au ujifunze kupika na kuwashughulikia watoto au kuamua mambo ambayo hujayazoea au hata huyafahamu kabisa.
Iwapo umepoteza kazi, inaweza kukubidi ujifunze kuomba kazi au hata kuhama kwenda mji mwingine. Wakati unapofanya mambo haya yote, unaweza kuwa bado una uchungu rohoni, lakini unaweza kufarijika unapojua kuwa unasonga mbele. Kila siku unapiga hatua.
Mungu ameahidi kuwa pamoja nawe wakati wa dhiki.
Mungu ameahidi kuwa pamoja nawe wakati wa dhiki.
Wakati unapoendelea kumsubiri akukomboe, unaweza kufarijika kwa kutambua kuwa yu pamoja nawe na anaendelea kufanya kazi kwa niaba yako hata ingawa pengine huoni kwa macho yako yale anayofanya.
Katika Mathayo 28:20, Biblia inasema, “…na hakika mimi nipo pamoja nanyi siku zote, hadi mwisho wa dunia…”
Jimmy J.
No comments:
Post a Comment