Wednesday, 18 July 2018

Mungu Hutumia Vyombo Vilivyovunjika

Huenda  unasoma sura hii na unafahamu kwa uchungu ni mara ngapi  umekosea wakati  ulipokuwa unachukua hatua  hapo zamani. Huenda  kulikuwa na  wakati  ulipata  nafasi ya  kuchukua hatua huku ukiwa na malengo  makubwa, na ari  ya  kuchukua hatua  kwa ujasiri na kutimiza  jambo fulani, lakini  mambo  yakaenda mrama. Ikiwa  hivyo ndivyo unavyohisi,  ninaweza kuelewa  kule unakotoka. Mara nyingi nimejaribu kufanya kadri nilivyoweza, lakini badala ya kuyafanya mambo kuwa  mazuri zaidi, nilihisi kana kwamba  niliyaharibu mambo  kabisa. 

Nadhani  sote  tumewahi kupitia  siku  kama  hizo.  Lakini  hatupaswi kuruhusu kushindwa  kwetu  wakati  wa nyuma kutuzuie kujaribu tena siku zijazo. Mungu anajua  kwamba  tunayo mapungufu  na  udhaifu. Kushindwa kwetu  hakumshangazi, na hakumzuii  kufanya kazi katika  maisha yetu.  Kusema  kweli,  mara  kwa mara  Mungu hutumia mapungufu  yetu  kudhihirisha  nguvu  zake.  Niliwahi  kusoma  hadithi moja inayoonyesha vizuri vile ninavyosema:

  • Mchukuzi  wa maji huko India alikuwa amebeba mitungi miwili  mikubwa  na  ilikuwa  inaning’inia  mwishoni  wa  ufito alioubeba  shingoni  mwake. Mmoja wa mitungi  hiyo ulikuwa hauna kasoro na haudondoshi  maji yoyote  mwishoni  mwa safari  ndefu  kutoka mtoni hadi nyumbani kwa bosi wake. Ule  mtungi  mwingine  ulikuwa  una  ufa,  na  kufikia  wakati wa  kufika  kule  ulikokuwa  unapelekwa,  ulikuwa  umejaa nusu tu. Hali ilikuwa hivyo kila siku  kwa kipindi  cha miaka miwili.  Yule  mchukuzi  wa  maji  alifikisha  kwa  bosi  wake mtungi  mmoja uliojaa  maji  na mwingine uliojaa  nusu. Bila shaka,  ule  mtungi  mzuri  ulijivunia  mafanikio  yake—ulikuwa mkamilifu  hadi  mwisho  wake  ambao  ulifinyangwa  kwa  huo. Maskini  ule  mtungi  uliokuwa  na  ufa  uliona  aibu  kwa sababu ya mapungufu yake na mateso  kwamba uliweza  kutimiza nusu  tu  ya  kazi  uliyofinyangiwa.  Baada  ya  miaka  miwili  ya ule  mtungi usiokuwa  mkamilifu  kuona  unashindwa vibaya, ulimwambia  yule  mchukuzi  wa  maji  na  kusema,  “Ninaona aibu na ningependa kukuomba msamaha.” Yule  mchukuzi  akauliza,  “Kwa  nini?  Unaona  aibu  kwa nini?” Mtungi  ukasema, “Kwa  kipindi cha miaka miwili  iliyopita, nimeweza  kubeba  maji nusu kila siku  kwa sababu huu ufa ulio  ubavuni mwangu unadondosha maji  wakati  wote,  maji yanavuja  hadi  nifike  nyumbani  kwa  bosi  wangu.  Kwa  sababu, ya kasoro zangu, huna budi kufanya kazi  hii yote  bila kupata faida inayoendana na bidii zako.” Yule  mchukuzi  wa  maji  aliusikitikia  ule  mtungi  wenye  ufa, na katika huruma zake akasema, “Tunapokwenda  nyumbani kwa bosi wetu,  nataka  utazame  uone maua mazuri kandoni mwa  njia.”  Na  kweli,  walipokwea  mlima,  ule  mtungi  wenye ufa uliyaona yale  maua mazuri ya mwituni kando ya njia. Lakini  walipofika  mwisho  wa  safari,  bado  ule  mtungi  uliumia maana nusu ya maji yalikuwa yamevuja tena. Kisha yule  mchukuzi  wa maji akauambia ule  mtungi, “Je, umegundua kwamba kulikuwa na maua  upande  wako wa njia tu  na  si  upande  mwingine  wa  mtungi?  Ni  kwa  sababu  nilijua kasoro yako na nikatumia  fursa hiyo kupanda maua  upande wako  wa njia. Kila tulipokuwa  tukitembea  kutoka  mtoni, ulimwagia  maji  ile  mbegu,  na  kwa muda  wa  miaka  miwili nimekuwa  nikichuma  maua haya mazuri na kuipamba  meza ya bosi wetu. 

Bila  wewe  kuwa jinsi ulivyo, bosi hangekuwa amepata maua haya yote ya kupambia nyumba yake.”1 Wewe  pia,  kama  ule  mtungi,  unaweza  kukamilisha  mambo  mazuri sana. Haijalishi  kuwa  wewe una kasoro na mapungufu. Usiache kile  unachokiona kuwa udhaifu kikuzuie kupiga hatua  za ujasiri zinazochochewa  na  matumaini.  2  Wakorintho  12:10  inasema:  “... Maana  niwapo dhaifu ndipo nilipo na nguvu.”  Je, hilo halifariji sasa?  Hata  wakati unapokuwa dhaifu, ndipo ulipo na nguvu  kwa sababu Mungu yuko  pamoja nawe. Anatumia kila sehemu ya maisha yako—hata nyufa—ili kuumba kitu cha kupendeza.

No comments:

Post a Comment