Thursday, 26 July 2018

Uchoyo

Ni dhahiri katika mawazo  yetu kuonekana tuko hali bora  kuliko wengine  au kufanya vyema kuliko wanavyofanya. Uchoyo ni  kuhusu  kuwa wa  kwanza katika kila jambo, na ingawa hakuna makosa ya kutaka  kufanya vyema  zaidi,  ni makosa  kufurahia  kuwaona  wengine wakikosa kufaulu ili sisi tufaulu.Ninaamini  kwamba  uchoyo wa aina yote ni  mbaya na kwamba unasababisha matatizo.

Katika  sehemu  hii, nataka  niyalete mawazo yako kwa  aina tatu maalum za  uchoyo ambao  kwa  kawaida unapatikana  katika  ulimwengu wa  leo na  matokeo  mabaya yanayotokana na uchoyo huo. 


Dhuluma  za  kingono:  Annah  ana  umri  wa  miaka kumi  na mitatu. Baba  yake humwambia yeye ni mwanamke sasa  na kwamba wakati umefika kwake kufanya  yale ambayo  wanawake hufanya.Anapomaliza  kumuonyesha  kile anachomaanisha  kuwa  yeye ni mwanamke, yeye huona haya,  huwa  na hofu na kujiona mchafu. Ingawa  baba  yake humhakikishia kwamba  kile  anachofanya  ni jambo zuri, yeye hushangaa  ni  kwa  nini  humtaka aliweke jambo hilo kuwa siri na ni kwa nini linamfanya ahisi vibaya. 

Huku  miaka  ikiyoyoma  na  baba  yake akiendelea kumdhulumu na  kumbaka,  Annah hufunga  hisia zake kwa  hiyo  hahitaji  kuhisi uchungu tena. 
Baba yake Annah ameuiba utoto  wake, ubikira  wake, uhalali wake, na bila ya  mwingilio kutoka  kwa  Mungu, ataiba maisha yake ili kupata kile alichokitaka.

Nachukizwa  mno  na visa vya kina-baba kuwabaka  watoto wao  na  visa  vya  watu  wa  familia kujamiiana  tunavyosikia,  lakini ukweli  ni  kwamba  asilimia 90-95 ya visa hivyo haviripotiwi.
Nilidhulumiwa  kingono  na  baba  yangu  mzazi  kwa  miaka  mingi. Nilijaribu mara  mbili  tofauti  kumwambia  mtu fulani  kilichokuwa kikitendeka  kwangu  na kwa  vile  hawakunisaidia,  niliendelea kuteseka peke yangu  hadi nikawa  mtu mzima na  hatimaye nikaanza kuzungumza  hadithi yangu  na  watu wengine na  nikapokea uponyaji kutoka  kwa  Mungu.Baba yangu  alifariki akiwa  na umri  wa  miaka  themanini  na sita  bila ya  kuadhibiwa  kwa  uhalifu alionitendea. Watu aliofanyakazi  nao  na  aliohudhuria nao  karamu na  dhifa mbali mbali hawakujua  alikuwa  akimbaka  bintiye tangu alipokuwa msichana mdogo.-Annah.

Twaona yale watu wanayofanya na kuwa haraka kuwahukumu, lakini  tunajua ```chanzo  cha  tabia zao?``` 
Wanawake wengi tunaowahukumu kuwa “matatizo  katika  jamii”  ni wahasiriwa  wa kubakwa na baba zao au watu wa familia zao. Kwa mfano:
```•Asilimia 66 ya makahaba wote ni  wahasiriwa  wa  dhuluma za kingono walipokuwa watoto.

•Asilimia 36.7 ya wanawake walio gerezani nchini Tanzania walidhulumiwa walipokuwa watoto.

•Thuluthi  moja ya watoto  walio dhulumiwa  na kutelekezwa baadaye huwadhulumu  na kuwatelekeza  watoto  wao wenyewe.

•Asilimia 94 ya  wahasiriwa  wa  dhuluma za  kingono  huwa chini ya umri wa miaka kumi na miwili wanapodhulumiwa.

Uchungu unaosababishwa  na visa vya  kina baba  kuwabaka watoto  wao  na watu wa  familia kujamiiana na dhuluma za  kingono ulimwenguni ni mkubwa  mno na  yote  yalianza  kwa  sababu watu  ni wachoyo na hawakujali ni  nani  atakayeumia  ilimradi  wamepata kile wakitakacho. Ndio,  pengine hutaua,  hutaiba,  hutadanganya,  wala  kutenda vitendo vya  dhuluma  dhidi  ya  watoto, lakini kuna uwezekano kwamba  u mchoyo  katika  njia fulani.

Ikiwa  tutakuwa  na  msamaha wa  uchoyo  wetu kwa  kuwaelekezea  kidole cha  lawama  wale ambao  uhalifu  wao  ni  mbaya kuliko wetu, hatutafaulu kukabiliana na matatizo haya katika jamii hivi  leo.
Kila mmoja wetu  lazima achukue jukumu  la kukabiliana na tabia yetu ya uchoyo, haijalishi ni wa kiwango gani  au kwa njia ipi tunayoueleza..

Jimmy J.

```Mwana Mageuzi.```

No comments:

Post a Comment