Wengi wetu hutumia muda mwingi kufikiria, kuongea na kufanya mipango yetu wenyewe. Ingawa ninafunza kwamba twapaswa kujipenda sisi wenyewe katika njia ya uwiano, siamini kuwa tunapaswa kujipenda sana hivi kwamba tuwe katika ulimwengu wetu na kujali tu kile tunachotaka tupate. Kwa njia zote lazima tujitunze kwa sababu sisi ni wa thamani kuu kwa mpango wa Mungu hapa duniani.
Alitupa uhai kwa hivyo lazima tuufurahie (angalia Yohana 10:10). Kwa hivyo tunahitaji kuutafuta, lakini lazima tusikose kutambua kwamba njia ya kweli ya kupata furaha ni kuyatoa maisha yetu kuliko kujaribu kujiwekea maisha hayo sisi wenyewe. Yesu anasema kwamba ikiwa tunataka kuwa Wanafunzi wake, lazima tujisahau, tukose kujionea sisi wenyewe na maslahi yetu yote na tumfuate Yeye (angalia Marko 8:34). Sasa nakubali kuwa hili ni wazo la kutisha, lakini nina nafasi maana nimeishi kwa muda mrefu wa kuweza kulijaribu na nimegundua kuwa linafanya kazi.
Yesu kadhalika anasema kwamba ikiwa tutayatoa maisha ya “chini” (maisha ya uchoyo) tutapata maisha ya “juu” (maisha yasiyo ya uchoyo), lakini tukiyaweka maisha ya chini tutapoteza maisha ya juu (angalia Marko 8:35). Anatupatia chaguo kuhusu jinsi tutakavyoishi. Anatuambia kile kitakachotufaa na kisha kutuacha tuamue iwapo tutafanya au la. Ninaweza kuendelea kuwa mchoyo na pia wewe waweza kufanya hivyo, lakini habari njema ni kwamba si lazima tufanye hivyo.
Tuna nguvu ya Mungu ya kutusaidia kuyapita mambo yetu na kuishi maisha ya kuwafanya watu wengine waishi maisha bora.
Safari
Uchoyo si tabia ya kujifunza, tunazaliwa nayo. Ni sehemu ya maumbile yetu. Biblia inautaja uchoyo kuwa “maumbile ya dhambi.” Adamu na Hawa walifanya dhambi kwa Mungu kwa kufanya kile alichowaamuru wasifanye na dhambi kuu waliyoifanya ilipitishwa kwa kila mtu ambaye alizaliwa. Mungu alimtuma Mwanawe Yesu afe kwa ajili ya dhambi, na kutukomboa kutokana na dhambi hiyo. Alikuja kutangua kile ambacho Adamu alikifanya. Tunapomkubali Yesu kuwa Mwokozi wa maisha yetu, Yeye huingia na kukaa pamoja nasi katika roho zetu na ikiwa tutaruhusu sehemu hii iliyofanywa upya katika nafsi zetu ili kuyatawala mawazo yetu, twaweza kuishinda dhambi ambayo imo milini mwetu.
Uchoyo si tabia ya kujifunza, tunazaliwa nayo. Ni sehemu ya maumbile yetu. Biblia inautaja uchoyo kuwa “maumbile ya dhambi.” Adamu na Hawa walifanya dhambi kwa Mungu kwa kufanya kile alichowaamuru wasifanye na dhambi kuu waliyoifanya ilipitishwa kwa kila mtu ambaye alizaliwa. Mungu alimtuma Mwanawe Yesu afe kwa ajili ya dhambi, na kutukomboa kutokana na dhambi hiyo. Alikuja kutangua kile ambacho Adamu alikifanya. Tunapomkubali Yesu kuwa Mwokozi wa maisha yetu, Yeye huingia na kukaa pamoja nasi katika roho zetu na ikiwa tutaruhusu sehemu hii iliyofanywa upya katika nafsi zetu ili kuyatawala mawazo yetu, twaweza kuishinda dhambi ambayo imo milini mwetu.
Dhambi huwa haiendi mbali, lakini Yule mkuu anayeishi ndani yetu hutusaidia kuishinda kila siku (angalia Wagalatia 5:16). Hii haimaanishi kwamba hatufanyi dhambi, lakini tunaweza kuimarika na kupata ufanisi katika maisha yetu. Siwezi kusema kabisa kabisa kwamba nimeushinda uchoyo, na sidhani kama kuna mtu yeyote ambaye ameushinda kabisa uchoyo. Kusema hivi ni kama kusema kwamba hatufanyi dhambi, kwa sababu dhambi yote inaanzia na aina fulani ya uchoyo. Sijashinda uchoyo kabisa kabisa, lakini nina matumaini ya kuimarika kila siku. Niko safarini na ingawa huenda sitawasili, nimejitolea kwamba wakati Yesu atakapokuja kunichukua kurudi nyumbani, atanipata ninaendelea kusukuma lengo hili (angalia Wafilipi 3:12-13). Mtume Paulo alisema maneno yafuatayo: “Nimesulubiwa pamoja na Kristo; lakini ni hai; wala si mimi tena, bali Kristo yu hai ndani yangu; na uhai nilio nao sasa katika mwili, ninao katika imani ya Mwana wa Mungu, ambaye alinipenda akajitoa nafsi yake kwa ajili yangu (Wagalatia 2:20). Paulo alimaanisha kwamba haishi tena kwa ajili yake mwenyewe na mapenzi yake, bali kwa Mungu na mapenzi ya Mungu. Nilitiwa moyo sana siku moja wakati nilipogundua kupitia mafunzo ambayo Paulo alisema maneno haya miaka ishirini baada ya kuokoka kwake. Kujifunza kuishi bila uchoyo ndiyo iliyokuwa safari yake, kama ilivyo kwa kila mmoja wetu. Paulo pia alisema “Nina kufa kila siku (ninakabiliwa na kifo kila siku na kufa ndani yangu).” (1 Wakorintho 15:31). Kwa maneno mengine kuwatanguliza wengine kwanza vilikuwa vita vya kila siku na kulihitaji uamuzi wa kila siku.
Kila mmoja wetu lazima aamue jinsi tutakavyoishi na kitakachotufanya tuishi kwacho, na hakuna wakati bora wa kufanya hivyo kuliko sasa. Wewe na mimi tuna wakati mmoja wa kuishi na uhai mmoja wa kutoa, kwa hivyo swali ni: “Je, tutaishi vipi?” Ninaamini kabisa kwamba ikiwa kila mmoja wetu atafanya sehemu yake kuyatanguliza maslahi ya watu wengine kwanza basi twaweza kuona na kuwa sehemu ya mageuzi yenye uwezo wa kubadili ulimwengu.
Mtumishi.
No comments:
Post a Comment